Monday, October 30, 2017

TUANZE JUMATATU HII YA MWISHO WA MWEZI HUU NA UJUMBE HUU....PUNGUZA MZIGO, PUNGUZA MARAFIKI WANAFIKI,PUNGUZA KABISA TENA WAPUNGUZE SANA TU, WAPUNGUZE ILI UWE MWEPESI



*Punguza marafiki ambao ukiwaambia unataka kufanya kitu wanakujibu "utawezaaa?" Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki ambao kutwa wanataka mchafue meza bar. Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki ambao umeongea nao kitu mkiwa wawili mwisho wa siku unakikuta kimeenea sehemu nyingine. Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki ambao wako sahihi kila siku wenyewe hawataki kuambiwa wamekosea. Punguzaaaa!* 

*Punguza marafiki ambao wakija kwako wao urafiki unahamia kwa mumeo au mkeo aliyekaa sebuleni wakati wewe kakuacha nje. Punguzaaaa!* 

*Punguza marafiki ambao wanakuwa na urafiki na maadui zako kwa ukaribu zaidi. Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki wa kwenye raha tu ukiwa na shida unajikuta peke yako. Punguzaaaa!* 

*Punguza marafiki wanaokusifu huku wakijua umekosea. Punguzaaaa!*

*Punguza marafiki ambao kila ukiwapigia simu na wao utawasikia yaani nilitaka kukupigia sasa hivi. Punguzaaaa!*

*PUNGUZA MIZIGO ISIYOKUWA NA UMUHIMU*
JUMATATU NJEMA  MAANA WIKI IJAYO ITAKUWA JUMATATU YA MWEZI MPYA WA KUMI NA MOJA:-)

No comments: