Tuesday, October 31, 2017

MWANAMKE MWENYE MIAKA 120 ANAASA WANANCHI KUTOSHABIKIA VITA .

Mwanamke Mwenyeumri wa miaka zaidi ya  120  mkazi wa Peramiho B wilayani Songea mkoani Ruvuma ambaye huenda  akawa mmoja wa wa watu wenye umri mkubwa duniani Bi. Sophia Haule ambaye alishuhudia vita  ya kwanza ya dunia ,ya pili na vita vya maji maji anaiasa jamii kutoshabikia vita.
Ni simulizi ya kusisimua ya bibi. Sophia haule mwenye umri wa miaka  120  ambaye alishuhudia vita ya kwanza ya dunia mwaka 1914-1918, vita ya pili ya dunia mwaka 1939 hadi mwaka 1945 na vita vya maji  maji na kuona machungu ya vita na  anasema vita si vya kuvikimbilia.
Varelia ngonyani ni mwenye miaka 77 ni mtoto wa bibi  sophia haule pamoja na kueleza changamoto za kumtunza mzee huyo menye  umri mkubwa zaidi lakini anaeleza mambo aliyosimuliwa na mama yake yaliyokuwa yakifanywa na machifu likiwemo la kuzikwa na binadamu akiwa hai pindi chifu anapozikwa.
Jimbo la Peramiho limebarikiwa kuwa na watu walioishi umri mkubwa wa miaka 90 hadi 100 ambapo mwenyekiti wa kijiji cha peramiho b anasema anajivunia jambo hilo.
CHANZO: ITV


 

2 comments:

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Hebu weka vizuri picha ya kigoli huyu lau tupate vitu vyake sawa sawa.

MARKUS MPANGALA said...

Hii ni rekodi kwa kweli.