Showing posts with label karibu. Show all posts
Showing posts with label karibu. Show all posts

Saturday, July 6, 2013

UNAMKUMBUKA MZEE WA UTAMBUZI KAKA SHABAN KALUSE? BAADA YA KIMYA KIREFU KARUDI KWA KASI KUBWAAA ..KARIBU KAKA!!!

Habari zenu ndugu zangu....Nimerudi jana jioni baada ya wiki moja kuwa kwenye kasafari kidogo...Nimerudi kuja kuvuna mboga zangu, kuangalia mazingira nk. Baada ya kutembeatembea katika vibaraza na kuona kama kuna kipya au? Nimekutana na mzee wa UTAMBUZI  baada ya kimya kirefu amerudi kwa kasi. Ukipata kaupenyo mtembelee HAPA ufaidi mambo. KAKA KARIBU SANA TENA KATIKA ULIMWENGU HUU WA KUBLOG. PANAPO MAJARIWA TUTAONANA KESHO DOMINIKA....Ngoja niendelee na usafi wa mazingira na kupalilia mboga zangu.

Monday, January 9, 2012

HUU NI MLO WANGU WA MCHANA WA LEO KARIBUNI NI SUPU YA KAROTI!!


HAPA NI KAROTI AMBAZO TAYARI ZIMEMENYWA KWA AJILI YA SUPU
Karoti 6-8 kubwa,
Vitunguu 2
Vitunguu swaumu/saumu vipande 3,
Kijiko 1 cha siagi,
Vijiko 2 vya tangawizi iliyokunwa.
Lita 1 ya maji.
Vikombe 2 vya cream,
Vikombe 2 vya maziwa,
Kijiko1 chumvi
Pilipili kidogo/kadili upendavyo.
Jinsi ya kufanya:-
Menya karoti, vitunguu na vitunguu saumu/swaumu. Kisha kata vipande vipande. Yeyusha siagi na kaanga kwa dakika 3-5 kwenye sufuria kubwa. Weka tangawizi , kisha tia maji. Pika supu kwa joto la chini huku umefunika hadi karoti ziwe laini. Weka cream, maziwa na pilipili. Kisha unamixa na blender ya mkono mpaka kuwa laini. unawezawa kuongeza maji au maziwa kama unaona supu ni nzito. KILA LA KHERI NA UPISHI HUU:-)


Friday, September 30, 2011

NIMEONA NISIWE MCHOYO:- KARIBUNI TUJUMUIKE MLO WA MCHANA HUU AMBAO NI SUPU YA SPINACHI!!!

Nimerudi toka kazini huku nikawa na hamu kweli kweli ya supu...baadaye nikakumbuka nina spinachi. Kwa hiyo hapa, ni supu ya spinachi ambayo ni:- spinachi, maji, na chumvi. Inaandaliwa kwa dakika 10...Kwa anayetaka anaweza kuweka nusu kikombe cha maziwa au cream. na katika kula unaweza kula na kipande cha mkate pia yai moja la kuchemsha. Ila Kapulya hapendelei sana vitu hivyo kwa hiyo anakula kama ilivyo. KARIBUNI SANA TUJUMUIKE!!!!

Friday, September 2, 2011

CHAKULA NILICHOANDAA na KULA JIONI LEO/IJUMAA HII KARIBUNI TUJUMUIKE!!

Kwenye sahani hii ni :- Wali (mchele wa kutoka nyumbani tena kule kunakosemekana ni mchele bora kuliko yote hasa Tanzania sio kwingine tena ni KYELA).... mshikaki wa kuku na kachumbali ..kitelemshio ni maji lakini usiogope kuna vinyaji vingine kwa anayependelea. KARIBUNI TUJUMUIKE ..JIONI NJEMA...

Wednesday, April 20, 2011

SASA HAPA SIJUI ITAKUWAJE?



Kaaazi kweli kweli, sasa hapa nafasi itapatikanaje?

Wednesday, March 16, 2011

Sunday, May 23, 2010

TUMKARIBISHE DADA MAISTARA NA BLOG YAKE TEGELEZENI KARIBU SANAAA!!


Napenda kumkaribisha dada Maistara Wastara na blog yake iitwayo Tegelezeni zaidi ingia hapa http://maisarawastara.blogspot.com/

Thursday, February 11, 2010