Hii kazi hii ilikuwa kazi ya karibu kila siku maana usipotwanga mihogo hakuna ugali...basi hapo unapomaliza kutwanga uso mzima ni kama vile umemwagiwa unga...Tulikuwa tukipaka usoni kama poda mweeeeee...kaaaazi kwelikweli. Nimekumbuka sana enzi zila na pia nimetamani ugali wa muhogo na kisamvu chake...si unajua hakitupwi kitu maganda ni chakula cha nguruwe mmea mzuri sana huu
Showing posts with label ugali wa muhogo. Show all posts
Showing posts with label ugali wa muhogo. Show all posts
Tuesday, October 28, 2014
Sunday, May 4, 2014
JUMAPILI YA LEO NIMETAMANI KWELIKWELI DAGAA WA ZIWA NYASA...NYUMBANI LUNDO
LUNDO:- Nimekumbuka sana leo, ugali wa mhogo, dagaa, kisamvu, matembele(mbwaka) bila kusahau samaki wa aina mbalimbali ndicho chakula kilichonikuza. Dagaa hawa ni watamu zaidi pale uwapatapo tu yaani wabichi ..hasa lile wanaota (lighanda) ikiwa na maana zilizochomshwa na kukaushwa maji yote usisahau chumvi na kapilipili kwa mbaliiii....Duh! najitesa bure hapa ngoje niache ila nitazile muda si mrefu Mungu akipenda:-) JUMAPILI NJEMA!
Subscribe to:
Posts (Atom)
