Showing posts with label nywele. Show all posts
Showing posts with label nywele. Show all posts

Thursday, February 9, 2017

BLOGG YA MAISHA NA MAFANIKIO IMECHAGUA HII PICHA KUWA PICHA YA WIKI....

Hakuna kupoteza muda hapa...nimeipenda hii safi sana UMOJA NI NGUVU UTENGANO NI UDHAIFU....AU MNABISHA?

Wednesday, May 7, 2014

NIMEIPENDA PICHA HII..NA NDIYO BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO IMECHAGUA IWE PICHA YA WIKI!!

Nimependa jinsi walivyojipamba:-Nywele, vidani, na bila kusahau tabasamu/Mapozi na halafu ngozi zao nyororo. PAMOJA DAIMA!!

Wednesday, July 10, 2013

BAADA YA MASAA MATANO NA HUU NDIO MWANEKANO MPYA WA KAPULYA!!!

 Hapa ni kichwa kizima, picha imepigwa kwa juu kuonyesha mwonekano wote...masaa matano nimekaa bila kuinuka na matokeo ndio haya..
Na hapa ni kwa mbele...mnaona kapulya alivyochoka si mchezo lakini nimefurahi nimeweza kusukwa maana zile nilisuka mwezi februari:-)..Dada Natalie kutoka Kongo  ni mwepesi ajabu...Sijui hizi nitakaa nazo muda gani:-)
 
 
Haya nawatakieni jioni njema ..Panapo majaliwa tutaonana tena...Kapulya ndani ya poziiii:-)

PICHA ZA WIKI:- KAPULYA NA NYWELE ZAKE!!

Hapa ni ijumaa wakati nasaka msusi...na ghafla jumamosi akanipa taarifa atanisuka kwa hiyo kazi sasa ni kufumua hizo nywele za kimasai...kazi ikaanza jumamosi..
 ..na jumatatu mzigo umekwisha sasa kazi kuchana eeeh bwana wewe si unaona hapa na afro yangu..leo jumatano ndo naenda kusuka ...nikirudi nitawaonyesha vipi imekuwa...Haya basi baadae:-)

Thursday, April 12, 2012

PICHA YA WIKI HIII:-NYWELE


Baada ya wiki kadha mdada huyu kufikiria afanye nini na nywele zake, leo amepata msusi na sasa anajiandaa kwenda kusuka........

....baada ya masaa tisa anaonekana hivi...bahati mbaya msusi wangu hakutaka kuwa katika picha ni mdada kutoka Kongo....Nimesuka rasta (tena) ila si za wamasai ..hahahaha...Oh! halafu nimesahau kusema bei yake ni 500 kr. Maana nimesoma maoni ya Da´Mija ameuliza ni shiling ngani kusuka hivi?

Saturday, March 17, 2012

MWONEKANO MPYA WA KAPULYA....

Hapa ilikuwa mwaka huu 2012/5/1 nilipopiga picha hii nikiwa nimesuka nywele za kimasai ......
...na hapa ni leo nimefumua zile nywele za kimasai na sasa nipo naturel /yaaani na nywele zangu nilizozaliwa nazo. Watoto wangu wameshangaa kwani nilifumua zile rasta minywele yangu ilikuwa mirefu si kawaida baada ya kuosha zikashiling/rudi na kuwa fupi...Yakajia maswali umenyoa mama?...ila wote wamependa mwonekano wangu mpya . Je wewe unayeangalia ni mwonekano upi unaupenda niendelee nao? JUMAMOSI NJEMA KWA WOTE....NA KUMBUKENI WOTE MNAPENDWA :-)

Friday, December 3, 2010

PICHA YA WIKI HII:- MTINDO WA NYWELE!!!!

SIJUI ANAFANYA NINI?
Wiki hii tuangalie mtindo wa nywele. Ebu angalia wanadada hawa ni wanandugu au? labda marafiki? au labda imetokea tu kuwa hivyo? Maana wanafanana hadi jinsi ya kuweka nywele.
IJUMAA NJEMA WANDUGU!!!

Thursday, June 17, 2010

Picha ya wiki hii!! Je? Unajua mwanamtindo huyu ni nani?

Nimeipenda hii picha na nimeona iwe picha ya wiki hii. Rangi za mavazi ni rangi ambazo zinawakilisha nchi yetu Tanzania. Na pia nimependa mwanamtindo huyu kwa mtindo wake wa nywele..

Na sasa ngoja tusikiliza kibao hiki ambacho kinawakilisha ujumbe murwaaaaaaaaaaaaaaaaaNi "Reggae sasambua sytle" iliyoimbwa na Dada Saida Karoli kuhusu sweet Tanzania

Thursday, December 17, 2009

DUH! NIMERUDI KUTOKA KUSUKA LEO 17/12-09

Mwanadada /mwanamama karudi toka kusukwa!!!
Kazi kweli kweli nilianza kusukwa hizo nywele saa sita mchana na ilipofikia saa kumi na moja jioni ndo kazi iliisha. Bahati mbaya msusi amekataa kuwa kwenye picha la sivyo mngeona jinsi nilivyopata mateso. Lakini ndo hivyo kuna msomo unasema:- Ukitaka kupendeza lazima uvumulie mateso:-) (Vill vara fin får du lida pin) Na kizuri zaidi picha hii ya leo kapiga binti yangu.

Wednesday, December 16, 2009

NGOJA TUANGALIE PICHA ZA LEO!!!!!


Hapa ni Septemba 2009 mwanadada ana manywele ya ajabu kichwani kwake. Na inaonekana kama anafanya kazi ya kublog.

Na hapa ni 16.Desemba 2009 yaani leo Jumatano mwanadada anaonekana ni mwafrika/mTanzania mwanaafro KABISA:-)
Swali je? picha ipi ni bora kuliko nyingine? au tuseme mwanadada awe na nywele za aina gani?

Thursday, August 7, 2008

AGOSTI 7,2008 NYWELE




The Sixties were the era of long hair.As long as the hippies were wearing their hair long and bein' against war and stuff, Black people decided they wanted to do it, too. Hippy hair hung down, Black people's hair went in every direction. This was known as the Afro.
This looked so neat that white people started getting perms so they could have Afros, too. But then Michael Jackson turned white, so Black people decided maybe they'd do corn rows instead.