Katika maongezi na Mzee wa changamoto tukaingia kwenye mada hii, yaani kuchapa watoto viboko. Yeye alisema haoni kosa kuchapa watoto viboko. Ndo nikapata wazo la kuandika mawili machache. Haya wasomaji tusaidiane.
Mnajua katika nchi nyingi dunianai wanaona si kitu cha ajabu kuchapi/kupiga watoto. Wanaona ni moja ya malezi. Kama Mzee wa C TUNAWEZA KUBADILI/KUACHA KUPIGA WATOTO
Jana nilikuwa naongea na Mzee wa Changamoto na baadaye katika maongezi tukaingia katika mada hii ya kuchapa watoto viboko. Yeye alisema haoni kosa kuchapa watoto viboko. Ndo nikapata wazo la kuandika mawili machache. Haya wasomaji tusaidiane.
Mnajua katika nchi nyingi dunianai wanaona si kitu cha ajabu kuchapi/kupiga watoto. Wanaona ni moja ya malezi. Kama Mzee wa changamoto anavyosema. Ila mimi ni kinyume na Mzee Changamoto pia watu wote wanaoona ni haki watoto wapigwe viboko.
Lakini tukumbuke kila mtoto ana haki ya malezi yenye usalama. Inabidi tukazane kwani mpaka sasa, yaani leo hii kuna nchi 24 tu ambazo ni marufuku kupiga watoto.
Nadhani karibu kila mtu anakumbuka jinsi tulivyopata viboko, yaani nyumbani pia shuleni. Ndugu zanguni wasomaji tujaribu kusaidiana kuzuia kuchapa/kupiga watoto kwani viboko sio dawa ya malezi. Jinsi mimi ninavyoona/fikiri mtoto akishazoea kupigwa viboko kila siku anakuwa sugu(hasikii) anaona kawaida tu na pia akili yake inadumaa. Najua ni jambo (somo) ambalo wengi hawatakubaliana nalo lakini ni LAZIMA tuanze. Tuache kupiga watoto nyumbani na pia shuleni. Wazazi wawe huru kwa malezi ya watoto wao wakati wote na pia wawe na haki sio kuwapiga piga.
Sio kufuata sheria tu pia wazazi na walimu wanaweza kusema /kuona ni nini na aina gani ya malezi yanatakiwa.
hangamoto anavyosema. Ila mimi ni kinyume na Mzee Changamoto pia watu wote wanaoona ni haki watoto wapigwe viboko.