Showing posts with label zao la kakao. Show all posts
Showing posts with label zao la kakao. Show all posts

Tuesday, October 11, 2011

SAFARI YETU YA NYUMBANI TANZANIA HATUKUKOSA KUWASALIMIA MARAFIKI/WENYEJI WETU PIA:SHAMBA LA KAKAO HAPA NI MATEMA BEACH

Hapa ni mwenyeji wetu Mr. Mgaya ,akitutembeza katika moja ya shamba lake la kakao. Kwa sisi ilikuwa ni mara ya kwanza kuona ZAO hili la kako ni vipi linalimwa na linaonekana vipi. Maana tulikuwa tunaona kako ipo kwenye kopo tu tayari kwa kunywewa.

Na hapa ni mti wa kako na hizo unazoona zimeningínia ndizo kakao zenyewe hapo bado hazijaiva bado.
Ukimwa mdadisi basi utajifunza mengi ...Yaani nina maana tuliuliza kama kakao zinaliwa kkama zilivyo ..hapo ni matokeo yake tukatafutiwa maoja iliyoiva ikabanguliwa na tukaonja ..sikuwahi kuonja kakao freshi maishani ...ulikuwa msafara ambao tulijifunza mengi sana....

Hapa ni kako zimeanikwa na baadaye zitakuwa tayari kwa kuwa kakao ya unga ..tulishindwa kusubiri mpaka kunywa...Safari nyingine labda.... tembea uone mengi, uliza jifunze mengi nk nk, haya ndio maisha ... kuna mengi yanakuja!!!