Tuesday, June 30, 2009

USAFIRISHAJI WA HARAMU WA WATU/BIASHARA YA WATU

Tatizo ni lipi?
Hiki ni kitendo cha kinyama sana kumuamisha mtu kutoka kwenye jumuiya yake na kwenda sehemu nyingine ndani au nje ya nchi kwa ahadi za uongo. Matokeo yake ni kunyanyaswa na kutumikishwa kwa kupita kiasi bila ya ujira kwa faida ya mtu mwingine. Hii hujulikana kama utumwa mamboleo na ni moja ya matishio makubwa ya haki za binadamu. Inasemaekena usafirishaji na biashara haramu wa watu huwatokea zaidi wanawake na watoto, Ingawa pia huwatokea wanaume kwa kiwango kidogo sana ukilinganisha na makundi hayo mawili.

Usafirishaji na biashara haramu ya watu hutokea duniani kote na unyonyaji wa watu kutofautiana kati ya nchi na nchi. Kwa mfano huko Afrika Magharibi hususana Togo watoto wanatumikishwa na kunyanyashwa katika mashamba ya kokoa yaliyopo huko Ghana. Wasichana huko Colombia wanalazimishwa ukahaba huko Japan nk, nk.

Pia tatizo hili halijaziacha nchi za afrika mashariki na kati zikiwemo Malawi,Burundi, na Rwanda, Jambo hili linaonekana linazidi kutapakaa sana ndani kwa ndani na linalenga zaidi watoto wanotumikishwa kazi za ndani maarufu kama house Girls.

Inasemekana Tanzania inatumiwa na wafanyabiashara hawa haramu kama nchi ya kupitishia wahanga hawa kutoka nchi za Ethiopia na Somalia na kupelekwa Afrika kusini.

Kwa watoto mara nyingi au kwa kawaida hutolewa vijijini. Kwa kuahidiwa MAISHA bora na ELIMU mjini na ndugu zao wa karibu au watu wanaoaminiwa na wazazi wao. Wakati mwingine watoto hao hutolewa na wazazi wao kwa ndugu kwa mategemeo watoto wao watapata MAISHA BORA wakiwa mjini.

Lakini wakati hali huwa sio kama walivyotegemea. Unyonyaji ni pamoja na kulazimisha muhanga kufanya ukahaba, kazi za ndani, biashara za mitaani, kuosha magari, na bila kupewa nafasi ya elimu na matibabu na mbaya zaidi bila kupewa chakula hata kidogo. Kunyanyaswa kwa jinsia, kutukanwa kupigwa, kutishiwa na kufanyishwa kazi bila ya ujira. Watoto wengi hufanikiwa kutoroka na mwisho huishia mitaani.

Sababu
Nadhani elimu itakuwa ni moja ya sababu kubwa. Upatikanaji mkubwa wa elimu mjini huvutia vijana wa kike na kiume kutoka vijijini. Wahanga wengi waliosaidiwa na Internatinal Organization for Migration (IOM) ni watoto walioacha shule au hawajawahi kwenda shule kabisa vijijini kwao. Watoto waliosaidiwa na IOM ni kutoka Uganda, Tanzania, Kenya Burudi pia Oman na nchi nyingine za uarabuni. Mpaka kufikia leo, zaidi ya wahanga 118. Taarifa nyingine zinasema IOM imefanikiwa kuwasaidia wanawake 115 na watoto wahanga wa usafirishaji na biashara haramu ya watu kurudi na kuungana na familia zao toka Uganda.Pia kupoteza wazazi wote wawili. Hali hii husabisha watoto kulazimika kutegemea walezi.

Aina ambayo inatambulika zaidi, zaidi Tanzania:-
Watoto:- vijana wa kike na kiume husafirishwa katika biashara haramu kutoka vijijini kwenda mjini kwa ajili ya utumishi wa ndani ya nyumba (house girl and house boys). Wasichana husafirishwa katika biashara haramu na kuletwa mjini na katika maeneo ya kitalii.

Ebu tujiulize maswali:-
1. Je nini hatima au mustakabali wa mtoto huyu ambaye amehamishwa toka katika jamii yake kwa sababu ameahidiwa au familia yake imeahidiwa kuboreshewa maisha?

2. Je ni namna gani jamii na serikali kwa ujumla inaweza kuwajibika ili kutokomeza tatizo hili ambalo inaonekana kuwa kikwazo kwa ustawi wa vijana wetu ambao inasemekana kuwa ndio taifa la kesho?

HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA EDO


Napenda kuchukua nafasi hii na kukutakia siku nzuri katika siku hii muhimu kwako. Ni hayo tu na tutafika tu. HONGERA Edo

Monday, June 29, 2009

TUENDELEE KUANGALIA NINI KINAWEZA KUTOKEA BAADA YA KUACHANA (NDOA KUVUNJIKA)

Kwa vile nishaanza kuongelea kuhusu -WANAWAKE UGHAIBUNI(SWEDEN)basi nimeona si vibaya kama pia tukijua:-

Baada ya kuachana mume na mke ambao walikuwa wanaishi pamoja. Unakuja mzozoz sasa kila kitu kichokuwa ndani ya nyumba ni lazima kugawana sawa.
Pia kama mlikua na nyumba ni lazima kuiuza na kugawana pesa, au kama mmoja wenu anataka kuishi katika nyumba hiyo. Basi ni lazima wewe umlipe yule atayeondoka nusu ya thamani ya nyumba. Gari pia vivyo hivyo kama nyumba.

Na halafu kitu kingine ambacho wengi wetu mtaona ni kinyume na Afrika kwetu (Tanzania). Najua Afrika hasa Tanzania watu au niseme mke na mume wakiachana watoto ambao ni wakubwa wanabaki kwa baba. Isipokuwa wale wadogo yaani ambao bado wananyonya ndio mama ataondoka nao/naye.

Hapa Sweden HAKUNA hiyo watoto wanakuwa mali ya mama mpaka watakapokuwa 18 ambapo wanaweza kuamua wapi wanataka kuishi. Lakini uzuri wake wakati huu wote watoto au mtoto anakuwa na mawasiliano na wote baba na mama. Huwa wazazi hawa wanawekeana zamu wiki moja au mbili kwa baba na nyingine kwa mama. Kama nilivyosema kwenye ile mada iliyopita ya KUOA BILA MAHALI au ile ya mke kuwa na sauti zaidi ndani ya nyumba. Hapa inawezekana kabisa mwanamke akawapa watoto jina lake la ukoo lakini hii inatokea hasa kama hawajafunga ndoa. MAMA AU MKE ANAKUWA NI MUAMUZI

Miaka hii ya karibuni imegundulika ya kwamba kutokana na hili jambo la kuachana achana limeongezeka kwa idadi kubwa. Na kwa mtindo huo watoto wengi wamekuwa na mafanikio /matokea dhaifu shuleni. Wanasema wao wanapata HUZUNI na pia wanapata MSONGO kiasi kwamba wanashindwa kumuda masomo. Ninachotaka kusema ni kwamba watoto katika maisha wanahitaji malezi ya wazazi wote wawili, wakiwa katika nyumba moja. Nyumba yenye amani na upendo. Kwani wazazi wakiwa na FURAHA, WATOTO pia watakuwa na FURAHA pia AMANI.

Sunday, June 28, 2009

MATUNDA NI MUHIMU KATIKA MWILI LAKINI BEI MBAYA MNO!!!!


Mti wa matunda damu. Matunda haya hapa Sweden moja unalipa 12kronor ni sawa na 2000Tsh
Halafu kula embe hapa embe moja inauzwa 9.90kronor ni sawa na 1584Tsh, pia papai bei yake ni kama 20,000Tsh. kwa hiyo ndio maana watu wengi wakija Afrika wanakula sana matunda kutokana na bei kuwa nafuu.

NAWATAKIENI WOTE JUMAPILI NJEMA

NAWAOMBEA
Nawaombea Yalo Mema
Kwa Usiku Na Mchana

Ziwaepuke Lawama
Kwa Watu Wenye Hiyana

Awajaalie Ukarimu
Kwa Nia zenu Njema

Awaepushie Lawama
Binaadamu Siwema

Tuesday, June 23, 2009

KUOA BILA KUTOA MAHARI (POSA)

Kutokana na maoni ya msomaji mmoja katika mada ya WANAWAKE UGHAIBUNI (SWEDEN). Nimeona ni vizuri mkijua ya kwamba:-

Maisha ya ndoa ya Afrika na hapa Sweden kila ninapojaribu kuwaelezea watu kuwa. Sisi waAfrika tunapokaribia umri wa kuoa kitu cha kwanza ni kutafuta mchumba na ukishampata zinaanza shughuli za kupanga mahari (posa). Lakini wao wanashangaa sana hata hawaelewi kabisa kwa nini tunatoa MAHARI(POSA). Wao wanadai ya kwamba tunauzwa, kama kuku. Yaani mzazi wa msichana anamuuza binti yake. Wanasema kama tunatoa mahari (posa) kwa kuwashukuru wazazi wa upande wa kike je? kwa nini na wazazi wa upande wa kiume wasipongezwe kwa kazi nzuri ya kumtunza kijana wao. Hata kama ukiwaambia ni njia ya kuonysha respect pia hawaelewi kabisa.
Hapo zamani hapa Sweden ilikuwa hivi , msichana akiolewa yaani anapoenda kuanza maisha kama mke. Alikuwa anachukua vitu toka kwao kama vile shuka, vyombo nk. Ni kama nyumbani TZ
Lakini siku hizi hiyo haipo hapa wanaoana/ishi tu hivihivi. Hakuna kutoa mahari ( posa) .
Naomba niseme hivi inaonekana kama watu wengi wanafikiri ukitoa MAHARI (POSA) basi ndio utakuwa mtawala. Yaani wanaume wengine wanakuwa na kasumba, wanajiona wakubwa wa nyumba, na mke anakuwa hana sauti. Anasema mi nimetoa MAHARI (POSA) kwa ajili yako.
Ndugu wasomaji kusema kweli sisi wanadamu tunaishi katika mila na desturi tofauti kabisa. Kwani hapa wao hili jambo la ndoa halihusishwi kabisa kwa wazazi. Ni baina ya kijana na msichana. wanaelewana wao wawili tu kama kufunga ndoa au kuishi hivihivi Naweza nikasema hii ni moja ya sababu ndoa zao hapa hazidumu muda mrefu. Haya wasomaji je kuna maelezo zaidi ya kuwaeleza watu hawa. Naomba MCHANGO basi.

Sunday, June 21, 2009

NAPENDA KUWATAKIENI WOTE JUMAPILI NJEMA KWA SALA HII

Mungu nakuomba unisaidie niwakumbuke wenye njaa ninapokuwa na chakula, wagonjwa nianpokuwa na afya nzuri, wote wanaoteseka kwa sababu ya vita ninapokuwa na amani, wasio na nyumba ninapokuwa nimelala na pia kuwa ndani ya nyumba yenye joto, pia nakuomba unisaidia niwakumbuke yatima kila ninapokuwa na wazazi wangu.

Na pia nakuomba:

Bikira Maria mama wa msaada na uibariki familia yangu, kaka zangu, dada zangu, wazazi wangu na watu wote dunia hii katika dhambi: AMINA

Saturday, June 20, 2009

NYIMBO ZETU (ZA TAIFA LETU LA TANZANIA)

Mungu ibariki Tanzania


Tanzania, Tanzania nakupenda kwa moyo wote


UJUMBE WA LEO:-WANAWAKE UGHAIBUNI (SWEDEN)

Kama waSwahili wasemavyo tembea uone, basi nimeona.
Kwani nakumbuka, pia najua ya kwamba wanawake Afrika ni wanyeyekevu mno kwa waume zao.

Lakini kwa muda nilioishi hapa Sweden. Nimeona ni kinyume, yaani nikinyume kabisa. Hapa ni wanawake ndio wanaamua /maamuzi yote ya ndani ya nyumba. (Wana amri sana kwa waume zao)

Nategemea uasili wangu utakuwa kama nilivyofunzwa yaani sitaambukizwa na hali hii. Kwani jambo hili limesababisha hapa Sweden kuwa na asilimia kubwa ya kupeana talaka
Au nisema wanawake wengi wanaona


Kitu kingine kwamba waswidi wengi wanaona sababu kubwa ya kuachana ni kwa sababu hakuna ubaguzi, yaani kikazi wanawake na wanaume. Wanawake wengi wanafanya kazi na wana mshahara ambao unatosheleza, Pia hata kama hawafanyi kazi kuna misaada mingi wanawake wanaweza kupata kutoka katika serikali ya kijiji kwa mtindo huu ndio maana wanaona hawawategemei sana waume zao kwa kuweza kuishi na kupata chakula.

Friday, June 19, 2009

HAPA SWEDEN LEO NI MIDSUMMER(MIDSOMMARAFTON)


HISTORIK
Traditionen kam från Tyskland på 1500- 1600 talet.
Seden var först förknippad med förstamajfesten.
Ordet majstång kommer av att man lövade (majade)sina hem
Flyttades från maj till midsommar av klimatskäl.

Nitajaribu kutafsirikwa kiswahili:-

KIHISTORIA KUHUSU HII MIDSUMMER NI HIVI:-

Kihistoria, mila na desturi hii imetokea Ujerumani karne ya 1500 - 1600.
Mila hii inauhusiano na sikukuu ya wafanyakazi
Neno Majstång linatokana na au niseme, watu hapo zamani walikuwa wanapamba majani kwenye nyumba zao.
Kwa hiyo wakaamua kuacha kusema (maj) na kusema (midommar)"midsummer" kutokana na hali ya hewa.

Labda niongezee ni hivi wengi walikuwa wanaamini kuwa kutokana na idadi ya hiyo miviringo inaonyesha watoto wangapi wamezaliwa kwa mwaka.

Thursday, June 18, 2009

TUMSAIDIE MTANZANIA WENZETU

Dear Friends and well wishers,
I humbly write to you in connection to above mentioned lady who is a daughter of The late Richard Muro who passed away sometimes in 2002.I received a call from Gaborone regional Immigration Office sometimes in June last year regarding Neema. They wanted to know why She was not transported back to Tanzania by the time ATB transported her father's body. They had tried to deport Neema back to Tanzania but she threatened to commit suicide if they do so. That's when they tried to contact ATB to assist. By the time of Muro's death it happened that he was renting at Mrs Naledi Mookinyana's mother's compound in Molepolole. So they all knew Neema and she bacame like a daughter to them. This bond made Naledi to volunteer to stay with Neema after her father's death. She accomodated, fed and supported her until she completed primary education in 2006 at Naledi Secondary School in Gaborone. By God's Grace she perfomed extremely well in her standard seven exams with All 8 A stars. She! was then selected to join Pre-Medical at the University of Botswana. Then the drama started. UB claimed that she was not Naledi's daughter nor legal dependant so she will need a student permit and then pay as a foreign student, about P35,000 a year. When Naledi went to immigration to enquire for the student permit they threatened to charge her for horbouring a foreigner illegally for so many years. They wanted to deport Neema.

I then managed to locate Neema's mother in Tanzania through mama Shine who happened to be knowing her uncle. The mother is financially unstable. I then realised that Neema was not Muro's biological daughter, rather his late brother's daughter. Even Muro had no legal right as Neema's guardian. Muro had decided to bring Neema to Botswana after realising that she was suffering where she was squattering after her father's death. The mother got married to another man in Mwanza town. Unfortunatelly the new husband died as well. He left a house and a small shop to her in Mwanza town which later got burnt down. So She was also squettering. I guess thats why Neema was not ready to go back there alive. I got touched.

I then asked the mother to send legal documents of which she did but the immigration turned it down because Neema had passed the age of adoption which is 16 years. She was then 19 years. After several correspondences and meetings between my office (ATB) and Immigration office, The Immigration Board was convinced and issued a student permit. The DVC-SA was the only person who had authority to change the student status from foreign to local. I wrote several letters with supporting documents and I had several meetings with The Directors of Finance and Student Affairs. The DVC-SA was then convinced and approved the change to local student, meaning she would pay about P13000 a year. She joined UB and started classes sometimes Sept last year. She has finished her first year and again performed very well, with all A's (all subjects). She will be starting clinical trials at Marina Hospital on 8th June 2009. Naledi Mookinyana managed to pay tuition fees, accomodation and books, ! about P15000.00 last year.

I reported the matter to ATB annual general meeting in sept last year of which they requested me to work and try to legalise her stay in Botswana, request UB to change her student status to local and then request all well wishers and friends to contribute towards her studies. Naledi is workin as records attendant at Local goverments, worker's wellfare. The husband works for a security company in Gaborone. Naledi has 6 children of her own and 2 from her husbands previous relationship. She is therefore not a rich lady, just a poor lady with a rich heart. She will therefore not afford to continue paying all school expennses on her own.

Thats why I write to you to humbly request for your contributions towards assisting this poor but very hardworking and God Blessed child. There will be a register in circulation please indicate the kind of assistance you will provide and hand the contribution to any ATB executive member or you can deposit the money into ATB's account no. 325515 barclay's House and then inform the atb's treasurer, Mr Mbekomize (+267 71449964) , or his deputy Mrs Nkabila (+267 71754374) or myself +267 7.... Our target is to raise about P25,0000.00 which will cover for her tuition fees, accomodation and books for second year which starts August 2009.

Naomba tuendeleze mshikamano wetu kama kawaida kwani watanzania wa Botswana tunajulikana kama watu wenye upendo na wenye kusaidiana. Tunakaribisha hata wenzetu walioko nje ya Botswana kama kina Mwasekaga, Mdoe, Nchimbi, Mama Mbeko, Mama Msuya, Rwezaura, Mh Mathayo, Prof Nkoma, Mwakalebela, Maggid, Kissaka, Kisa, Benard Mhando, na wengineo tunaomba mtuunge mkono. Nitakuwa natoa taarifa ya michango kwenu mara kwa mara. Ujumbe huu umeletwa kwako kwa kuwa unajali, Tafadhali foward email hii kwa wasamaria wema.

Natanguliza shukrani.

Nieman Kissasi
eMail: kissasi@lycos.com
Mwenyekiti,
Association of Tanzanians In Botswana (ATB)

TUENDELEE NA MAMBO YA USAFIRI WETU



Je? unadhani huyo mbuzi hapo anajisiaje je wewe ungependa kusafiri hivyo?

Wednesday, June 17, 2009

SAFARI YA SONGEA MWAKA 2009

Najua wengi mnakumbuka mwaka huu mwanzoni kabisa nilikuwa nyumbani Tanzania. Ni kwamba baada ya wiki moja, nilikwenda madukani kununua vyombo ilikuwa siku ya Ijumaa. Si mnajua Ijumaa ni siku ya watu kupita madukani kuomba. Songea ni hivyo sijui sehemu nyingine Tanzania pia. Basi nikiwa katika harakati za kulipa akaja mtu mmoja au niseme alikuwa (kijana)au pia naweza kusema alikuwa na "changamoto za kifikra" (mentaly challenged)?
Alivyoonekana alikuwa kichaa. Akamwambia mwenye duka naomba hela akamjibu leo hakuna.

Akageuka kwangu we dada je? naomba hela nami nikamwambia sina. Akanipiga kofi na akaondoka zake. Kwa kweli nilishikwa na mshangao sana. Nimeandika hii kufananisha na mambo anayofanya dada Koero ninavyoamini mimi angekuwa pale angeacha kununua vyombo na angempa yule mwombaji. Nimejifunza mengi sana katika mada zake dada Koero asiyesoma basi chukuni muda na someni. Koero Mkundi hasa hii mada ya ANITA NA MIKASA YA DUNIA .Nashukuru Mungu ametuumba tofauti. Ni hayo tu kwa leo ni mada fupi lakini ina ujumbe wake.

Tuesday, June 16, 2009

KUNA USALAMA HAPA KWELI?


Nani atafika salama gari, watu au mzigo? kazi kwelikweli hapa.

Monday, June 15, 2009

TUNAWEZA KUBADILI/KUACHA KUPIGA WATOTO

Katika maongezi na Mzee wa changamoto tukaingia kwenye mada hii, yaani kuchapa watoto viboko. Yeye alisema haoni kosa kuchapa watoto viboko. Ndo nikapata wazo la kuandika mawili machache. Haya wasomaji tusaidiane.

Mnajua katika nchi nyingi dunianai wanaona si kitu cha ajabu kuchapi/kupiga watoto. Wanaona ni moja ya malezi. Kama Mzee wa C TUNAWEZA KUBADILI/KUACHA KUPIGA WATOTO
Jana nilikuwa naongea na Mzee wa Changamoto na baadaye katika maongezi tukaingia katika mada hii ya kuchapa watoto viboko. Yeye alisema haoni kosa kuchapa watoto viboko. Ndo nikapata wazo la kuandika mawili machache. Haya wasomaji tusaidiane.

Mnajua katika nchi nyingi dunianai wanaona si kitu cha ajabu kuchapi/kupiga watoto. Wanaona ni moja ya malezi. Kama Mzee wa changamoto anavyosema. Ila mimi ni kinyume na Mzee Changamoto pia watu wote wanaoona ni haki watoto wapigwe viboko.

Lakini tukumbuke kila mtoto ana haki ya malezi yenye usalama. Inabidi tukazane kwani mpaka sasa, yaani leo hii kuna nchi 24 tu ambazo ni marufuku kupiga watoto.

Nadhani karibu kila mtu anakumbuka jinsi tulivyopata viboko, yaani nyumbani pia shuleni. Ndugu zanguni wasomaji tujaribu kusaidiana kuzuia kuchapa/kupiga watoto kwani viboko sio dawa ya malezi. Jinsi mimi ninavyoona/fikiri mtoto akishazoea kupigwa viboko kila siku anakuwa sugu(hasikii) anaona kawaida tu na pia akili yake inadumaa. Najua ni jambo (somo) ambalo wengi hawatakubaliana nalo lakini ni LAZIMA tuanze. Tuache kupiga watoto nyumbani na pia shuleni. Wazazi wawe huru kwa malezi ya watoto wao wakati wote na pia wawe na haki sio kuwapiga piga.
Sio kufuata sheria tu pia wazazi na walimu wanaweza kusema /kuona ni nini na aina gani ya malezi yanatakiwa.
hangamoto anavyosema. Ila mimi ni kinyume na Mzee Changamoto pia watu wote wanaoona ni haki watoto wapigwe viboko.

Saturday, June 13, 2009

KAAZI KWEELIKWELIII!!!

Hii sasa kali
Kwa nini kukodi gari ulipe nauli yako, ulipie na mzigo pia????

TUSIWASAHAU WATOTO WIMBO HUU UNAITWA SIMAMA KAA

Kwanza namshukuru Kaka Kamala kwa kunikumbusha nyimbo alizoandika kibarazani kwake. Kwa hiyo nami nnimeona niweke hii, kwani kuna wazazi, wazazi watarajiwa ambao wanahitaji kuwaimbia watoto wao. Wimbo huu nadhani wengi mnakumbuka haya soma hapa au imba:-

Simama kaa, simama kaa
Ruka ruka ruka simama ka
Kimbia tembea tembea tembea
Kimbia tembea tembea tembea
Simama kaa simama kaa
Ruka ruka ruka simama kaa.

Friday, June 12, 2009

IJUMAA YA LEO NAWAKARIBISHENI SAMBUSA ZA NYAMA ASIYEKULA NYAMA ZIPO ZA MBOGA PIA KARIBUNI SANA

VIPIMO
(Manda ya sambusa ya tayari Kiasi zinavyouzwa
Kiasi cha sambusa 40-50)
Mafuta ya kukaangia Kiasi
Nyama ya Kusaga kilo moja na nusu 3LB (Pounds)
Thomu na tangawizi iliyosagwa 2 Vijiko vha chai
Pilipili mbichi iliyosagwa 1 Kijiko cha chai
Pilipili manga 1 kijiko cha supu
Garam masala 1 kijiko cha supu
Chumvi Kiasi
Vitunguu maji vilivyokatwa
(chopped) 3 Vidogo au 2 Vikubwa
Kotmiri iliyokatwa (chopped) Kiasi

NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA

1. Pika nyama ya kusagwa kwa kutia chumvi, thomu na tangawizi, pilipili na ndimu.
2. Kabla haija kauka tia Garam masala.
3. Zima moto acha kidogo ipoe tia vitunguu na kotimiri.
4. Funga sambusa katika manda kama kawaida.
5. Pika sambusa katika mafuta ya moto hadi ziwe nyekundu na zikiwa tayari kuliwa.

Thursday, June 11, 2009

MALI NA FEDHA NI KITU GANI KWA MWANAMKE?

Kuna jambo moja leo nataka kulizungumzia, nalo sio jingine bali ni hili la wanaume kutokujua hasa sisi wanawake tunawapendea nini katika ndoa au mahusiano.
Katika maisha yangu ya ndoa nimekuja kugundua mambo mengi sana ambayo huenda wanaume wengi hawayafahamu juu yetu sisi wanawake.

Kuna ujinga mkubwa sana ambao huwa unawasumbua wanaume. Wanaume wengi, sijui ni kutokana na malezi huwa wanadhani kwamba sisi wanawake tunahitaji fedha na mali ili kufurahia maisha ya ndoa au mahusiano.

Na dhana hii ambayo mimi naiona kama ni potofu, huwafanya wanaume kuamini kwamba wakiwa na fedha watakuwa wamemaliza matatizo yote ya mwanamke, na hivyo kuwa na ndoa au mahusiano yenye amani na utulivu.

Na kwa kuwa wanaamini hivyo, basi wakiishiwa ndani hapakaliki, wanahangaika kutafuta fedha ili kuzihami ndoa zao au mahusiano yao na wapenzi wao, kwani wanaamini kuwa bila fedha kutakuwa hakuna upendo tena kutoka kwa wake zao aua wapenzi wao.
Katika kipindi hicho cha ufukara ndipo mwanaume atakuwa karibu zaidi na mke au mpenzi wake kwa hofu ya kuogopa kuachwa, lakini baadae akizipata anakuwa hana muda na (bize)unajitokeza kwani wanakuwa na imani kuwa fedha ipo kwa hiyo uwezekano wa kuachwa na wake au wapenzi wao nao unakuwa haupo.

Sikatai wanaume kutafuta fedha kwa bidii ili kuondokana na umasikini na kuweza kijikimu kifamilia, lakini inapokuja kuonekana kuwa sisi wanawake tunawapenda wanaume kutokana na kuwa na fedha, hilo nalipinga kabisa.
Tuachane na zile dhana zilizojengeka siku hizi kuwa, wanawake wa siku hizi eti wanafuata pesa tu (after money) na wanathamini sana wanaume wenye fedha. Hilo inawezekana lipo lakini hebu tujiulize, hivi mwanamke anayempenda mwanaume kwa ajili ya fedha, hata akiolewa, unadhani atakuwa na amani kweli?

Kama mwanaume huyo atakuwa (bize) hana muda na shughuli zake, halafu anadai kuwa ana amani, basi labda atakuwa anaipata mahali pengine na sio kwa mume huyo, na hiyo ni hatari sana.
Kuna haja ya wanaume kujiangalia mienendo yao, je wanakuwa na muda na wake au wapenzi wao? Na wanatenga muda maalum wa kuzungumzia matatizo ya familia yao na kutafuta suluhu kwa pamoja?

Kuna haja ya wanaume kujikagua na kuangalia upya mahusiano na wake au wapenzi wao yakoje kabla mambo hayajaharibika

Wednesday, June 10, 2009

UNYANYASAJI WA WANAWAKE UNAZIDI DUNIANI

Huu ni ujumbe wa leo ambao unaeleza mengi na mengi yanaonekana, haya karibuni msikie na muone.


Kama unataka kunywa pombe basi kunywa kwa starehe yako lakini sio unakunywa pombe na kuanza kupiga wengine au mke wako. Kwa nini kunyanyasana kama unaona ukinywa pombe akili inachafuka basi acha kunywa maji.

Tuesday, June 9, 2009

KWELI HII NI HAKI?

Haya na maoni ya msomaji kwa picha hizo hapo chini.

Hii niliwahi kusikia imetokea Uganda mabapo mzee mmoja, alikuwa akimlazimisha mke wake anyonyeshe watoto wa mbwa ambaye mama yao alifariki. Kwani kabla mama yao hajafariki alikuwa na ng'ombe ambao walikuwa akitoa maziwa kwa ajili ya hao mbwa. Na hao ng'ombe huyo mzee alitoa mahari ya huyo mama hivyo mbwa wakawa hawana sehemu ya kupata maziwa ndipo yule baba akawa anamlazimisha mke wake awanyonyeshe hao mbwa. Kwani yeye alikuwa ni muwindaji, na hao mbwa walikuwa wakimsaidia katika shughuli zake za uwindaji. Lakini watoto wa huyo mama mmoja alifariki kwa ugonjwa ambao unakisiwa ni kichaa cha mbwa, na yule mmoja aliebaki nae alianza kukuhoa kama mbwa, na mama chuchu zake zilikuwa na madonda kwa ajili ya kung'atwa na mbwa wakati akiwanyonyesha, lakini kwa india ni mambo ya kawaida. Ikiwa ni pamoja na kuuza viungo vya mwili na kupandikizwa mimba za watu wengine kwa ujira.

Hapa bado sijaelewa yeye huyo mzee alijisikia raha gani. Na pia kweli alimpenda mke wake na watoto au aliwapenda zaidi mbwa. Kumsaidia kuwinda, labda wenzangu mnisaidie hapa. Kwali kumlazimisha mkw wako knyonyesha mbwa hivi wanaume wanakiri wao ni akina nani kuwatesa wanawake kiasi hiki?

KWELI NI HAKI AU INAWEZEKANA KWELI?

Je? ni huruma au?


Na hapa je?

Picha hizi zinatoka kwa kaka Mjengwa. Ama kweli duniani kuna mambo!!!!

Monday, June 8, 2009

MWANZO WA BINADAMU, MASWALI NI MENGI KULIKO MAJIBU. JE UKWELI NI UPI?

Nimelala leo na kufikiri kwa nini watu tupo tofauti. Lilikuwa swali la kwanza kumuuliza mume wangu leo badala ya kusema umeamkaje? Na baadaye nikakumbuka hii mada ya kaka Shabani Kaluse nikaona ni vema niiweka hapa ili nipate jibu. Kwani hili jambo linanipa utata sana kwa nini kuna waafrika, wazungu, wahindi, waarabu, nk. Kama kweli ni kweli mwanzo wote tulikuwa waafrika bado sijaelewa. Labda sasa nitapata jibu Asante kaka Kaluse kwa mada hii.


Kama nilivyosema wakati nafungua huu mjadala kuwa nadharia ya uwepo wa binadamu imejaa utata mtupu.
Katika dini tulifundishwa kwamba binadamu wa kwanza kuumbwa alikuwa Adam na Eva, na nilipokuwa shule, napo nilifundishwa kuwa chanzo cha binadamu ni nyani, halafu akawa anabadilika hadi kufikia kuwa binadamu.

Lakini bado kuna Maswali najiuliza, hivi ni kwa nini, nyani wengine wamegoma kubadilika hadi leo? Yaani wamebaki kuwa nyani badala ya binadamu.
Je na sisi kwa nini tumesita kuendelea kubadilika?

Kama tulikuwa kama nyani, halafu tukabadilika na kuwa binadamu, inakuwaje tusiendelee kubadilika zaidi na zaidi? Au kulikuwa na mipaka ya kwamba tukifikia mabadiliko kama haya tuliyonayo iwe ndio basi?

Kama ingekuwa binadamu aliumbwa kama nyani na kubadilika kufuatana na mazingira labda na mambo mengine, mbona basi leo hii uhusiano wa kinasaba kati ya binadamu na nyani sio mkubwa kama ule uliopo kati ya binadamu na panya weupe?
Yaani wale panya niliowaeleza awali katika makala iliyopita kuwa ndio wanotumika kufanyia utafiti masuala mengi yenye kumgusa binadamu, kwani kinasaba panya hawa wanakaribiana na binadamu.

Basi kuna haja ya kuamini kwamba binadamu wa kwanza alikuwa ni panya kisha akabadilika na kuwa kama alivyo leo.
Lakini bado najiuliza kwa nini huyu panya asiendelee kubadilika, amefungwa na kitu gani?


Hivi karibuni wakati naperuzi peruzi katika mtandao nimekutana na mijadala mikali kuhusu asili ya viumbe hai.
Kwa mfano nchini Marekani mjadala huu umeingia mashuleni ukiwa na nguvu mpya, kutokana na vijana wengi nchini humo kupambazukiwa na kukataa kukaririshwa elimu za wanasayansi wa kale zisizo na mashiko.

Vitabu vingi vya Baiolojia vilikuwa vikisema kwamba asili ya viumbe hai ni mwendelezo wa mabadiliko (Evolution)
Walimu wengi wa nchini Marekani na Ulaya ambako jambo hili limeshika nguvu wanapinga nadharia hii ya mabadiliko na wanaamini kwamba viumbe hai viliumbwa na kitu, jambo au nguvu yenye akili.
Wataalamu wa mabadiliko nao wanapinga na kusisitiza kwamba nadharia yao ni ya kisayansi na ya wale wanaopinga ni ya kidini.

Hivi sasa hata wale waumini wa nadharia ya mabadiliko iliyoasisiwa na Charles Darwin wameanza kuitilia mashaka nadharia hiyo kiasi cha kuitupilia mbali ili kutafuta nadharia mbadala.

Kwa mfano, Mwanabaiolojia mashuhuri kutoka nchini Sweden, Sren Lvtrup, ameweka wazi kwamba, anaamini siku moja nadharia hii ya Darwin ya mabadiliko itakuja kuwekwa wazi kwamba ni nadharia ya uongo kupita kiasi katika historia ya sayansi.

Lakini Nadharia hii ya mabadiliko inaendelea kufundishwa katika mashule yetu ambayo yanahudumiwa na kodi za walalahoi, huku nadharia hii ikiendelea kutiliwa mashaka kila uchao.

Kwa kuwa nadharia ya kidini ina msimamo wake tofauti na ule wa sayansi, sasa kwa nini wanafunzi wasifundishwe nadharia zote mbili, kila moja ikiwa na ushahidi wake ili waweze kupembua ubora na udhaifu wa kila nadharia na kuwawezesha kwa ridhaa yao wenyewe kuamua nadharia ipi kati ya hizo mbili ina ushahidi bora kuzidi nadharia nyingine?

Bado napata kizunguzungu katika kujadili hii mada, kwani kila ninavyozidi kutafuta ukweli nakutana na nadharia zinazopingana, ingawa kila moja haitoi ushahidi unaojitosheleza.

Je wenzangu mnayo maoni gani juu ya hili?

Nahisi mada hii inaelekea kunishinda, naomba msaada wenu.

Saturday, June 6, 2009

LEO HAPA SWEDENI NI SIKUKUU YA TAIFA KWA HIYO NIMEONA LABDA TUSIKILIZE WIMBO WA TAIFA HA PA SWEDEN

Wimbo wa taifa wa hapa sweden


Värmlands visan = wimbo wa mkoa niishio hapa Värmland


Baada ya kuona hivi nimeona si vibaya nikijipendelea pia.Wimbo wetu wa Taifa:-)

Friday, June 5, 2009

CHIMBA KISIMA CHAKO MWENYEWE By Faustin Munishi:


Uchimbe kisima wewe mwenyewe unywe maji yako peke yako na usiyashiriki nao wengine ni hatari kubwa eeh!
Maji ya kisima cha watu wengi yameingiliwa na mdudu ukiwa na kiu usiyaonje utaambukizwa eeh.
Na kiu ya maji imeongezeka watu wanayanywa kila wakati na yanauzwa kote barabarani nani atapona eeh?
Kwa sababu maji yana mdudu yanapatikana kirahisi ukipita kote utayaona wacha kuyachota eeh.


Ukiwa na njaa ni ya chakula huwa ni vigumu upatiwe lakini sigara na hata pombe watakupatia eeh.
Unajua kwa nini?
kwa sababu pombe na sigara zinaua wanataka na wewe ufe na wao wanakupatia eeh.
Tena na siku hizi na hayo maji yaliyo yaliyoingiwa na mdudu utapewa bure bila kuomba ili mfe wote eeh.
Yapo kwenye chupa kubwa na ndogo watu wanazipenda zile ndogo wanafikiliria zipo salama wamedanganyika eeh.
Wanazifunika nusunusu wamefanya hivyo makusudu ili waamushe kiu ya maji usidanganyjike eeh!

Ndugu jihadhari na maji ya rahisi kachimbe kisima wewe mwenyewe ukiwa na kiu uyanywe maji uliypoyachimba heri.
Dawa ya mdudu hawajaipata wanaitafuta kotekote umwamini Yesu akuokoea amalize kiu

Unaweza kusikiliza wimbo hapa chini



Mithali 5: 15 – 19
Unywe maji ya birika lako mwenyewe, na maji yenye kububujika kwenye kisima chako.
Chemichemi yako ibarikiwe nawe umfurahia mke wa ujana wako!

Asante Kaka Lazarus Mbilinyi

Thursday, June 4, 2009

KUMUAHIDI MTOTO ZAWADI NI KUMFUNDISHA AU KUMUHARIBU?

Kuna tabia ya sisi wazazi kuwaahidi watoto kwamba tutawapa zawadi fulani kama watafanya kitu fulani. Tatizo la kwanza linalojitokeza hapa ni kwa mtoto kushindwa kujua kwamba anapaswa kufanya mambo mazuri hata kama hakuna zawadi.

Kila wakati mtoto atakuwa akifanya jambo au mambo mazuri kwa matarajio ya zawadi na endapo kutakuwa hakuna zawadi hataona sababu ya kufanya hivyo

Mtoto anapoambiwa kwa mfano kwamba akiwa wa kwanza darasani atapatiwa viatu, anakuwa anajengewa dhana kwamba viatu sio haki yake bali ni mpaka afikie matarajio fulani ya mzazi wake ili aweze kupata viatu.

Kuna wazazi ambao huwaahidi watoto wao zawadi kama nguo, midoli, baskeli na vitu vingine vinavyofanana na hivyo, ambavyo kimsingi ni haki yake.

Wengi wetu tumelelewa katika mazingira ya aina hii. Tulipokuwa wadogo wazazi wetu walishindwa kujua kwamba viatu, nguo, midoli na kadhalika ni haki yetu, bila kujali kama tumefanya vizuri darasani au tumefanya jambo lolote tulilopaswa kulifanya kwa ustadi mkubwa, kama walivyotarajia.

Kwa mtindo huo wa malezi wametufanya tuamini kwamba ili tupate haki zetu ni lazima tufikie matarajio ya wazazi.
Na sisi tumejikuta tunatumia mbinu hiyo hiyo katika kuwalea watoto wetu.
Je? malezi ya aina hii yana athari gani katika ustawi wa watoto wetu?
Labda hilo niwaachie wasomaji mtoe maoni yenu, kwani mimi hili linanitatiza….

Wednesday, June 3, 2009

HAPPY BIRTHDAY OUR SON AND LITTLE BROTHER


Tarehe hii ya leo imepita miaka nane tangu huyu kijana azaliwe. Sisi Familia yake tunapenda kumpa pongezi kwa siku hii. Hongera sana kwa siku yako ya kuzaliwa ni Baba, Mama na dada yako ndio wanakupengeaza. Uwe na siku njema Erik.

Tuesday, June 2, 2009

KISWAHILI

Mara nyingi huwa nakasirishwa kuona / kusikia watu wanatumia vibaya baadhi ya maneno ya kiswahili. Hapa nimechukua au nataka kutoa mfano haya maneno matatu. Karibu, Jambo na Habari

Karibu: Ni kuto kuwa mbali kwa wakati au mahali, kiasi cha kukadria. Lakini watu wengi wanaelewa zaidi karibu ni tamko litumikalo kuitikia hodi au wakati mtu anapokaribishwa au kupokewa mahali fulani.

Jambo: Watalii wengi wanafikiri wanaweza kiswahili, kusalimia wasemapo jambo hawajui kwamba Kiswahili sananifu hutamkwa hujambo/haujambo/hamjambo? kwani ukisema hivi anashindwa kuitikia sijambo. Si afadhali hata wangefundishwa kusema hali yako.....

Habari: Neno habari limekuwa linanitatanisha sana. Kama kawaida maneno mengi ya kiswahili yana maana mbili azu zaidi. (1) Habari ni melezo ya jambo fulani lililotokea, taarifa, ujumbe na ripoti.
2) Habari hutumika katika kuamkiana na kuulizana hali. Lakini inaonekena wengi hatuwazi sana tunapoongea hili neno litumikeje.

NANI AMESEMA MA-TRACTOR HAYABEBI WATU ULAYA? HII NI KUTOKA UINGEREZA

Monday, June 1, 2009

JE? NI VIGUMU KUISHI BILA NGONO?

Wengi tunajua/pia tunajadili ukimwi na ngono, lakini tunahitaji kukumbuka kuwa sio waTanzania wote ama binadamu wote ni hivyo. Cha muhimu ni kuelewa kuwa ugonjwa huu unaua binadamu, na kwamba, hawa binadamu wanatokea katika kila sekta ya maisha, wanadini, wapagani, wasio na elimu, wenye elimu, wamjini, wanavijiji, nk.
Je? kuna ubaya gani kuwaelimisha wengine kuhusiana na matumizi ya ndomu?

Tukumbuke ya kwamba baada ya Hawa na Adam kula lile tunda baya, sote tulizaliwa madhambini, na tunashawishika kirahisi. Yaani, hata Hawa na Adam , ghafla waligundua ya kuwa wako uchi, nadhani mle bustanini kulikuwa kuzuri na kulikuwa na hewa bora yaani jua lilikuwa haliwachomi, majani hayakuwakata.Walipofukuzwa ndio walilazimika kuvaa nguo kwa sababu ya jua kali, mavumbi, miiba nk. Hakuna aliyewaamrisha kuvaa nguo.

Ngono inashawishiwa maishani kwa mbinu nyingi ambazo ni vipofu tu wasioziona. Katika magazeti, mavazi, sinema, hadithi za waliojaribu, umbea nk. Ni kama vile Hawa na Adamu, walivyoshawishika kula lile tunda hata walivyojua Mungu wao aliwakataza, lakini sisi wengine tunashawishika kirahisi kula hili tunda liitwalo "ngono". Wote tunajua tukishalionja tunda hata yeyote akikuambia "basi acha" wengi tunacheka ana kushangaa? Hii in kama vile mtoto akishaonja pipi, halafu ategemewe kutotamani pipi mbeleni.

Pipi zitakuwepo duniani kwa miaka mingi, vishawishi vya ngono vitakuwepo duniani kwa miaka mingi. Hii ndio sababu tunahitaji kuelimishwa kuwa pipi si nzuri kiafya. Lakini pia tunahitaji kuelimishwa kuwa wale watakao tamani basi wale nyingi na wasisahau kupiga mswaki. Naamaanisha, ujumbe wa kuacha ngono uambatane na ujumbe wa kupunguza kufanya ngono na watu wengi NA elimu ya kutumia ndomu.