Thursday, June 18, 2009

TUENDELEE NA MAMBO YA USAFIRI WETU



Je? unadhani huyo mbuzi hapo anajisiaje je wewe ungependa kusafiri hivyo?

4 comments:

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

wewe mbona unakula nyama yake? unadhani anafurahia kuuwawa na kuliwa?

chib said...

Ukatili huo kwa wanyama

Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) said...

Nadhani Kamala ameuliza swali la msingi. Vipi kuhusu kuwachinja na kuwala? Hapa Marekani imefikia hatua sasa hata kumgusa mnyama mtu inabidi uwe mwangalifu. Juzi hapa rais Obama kamuua NZI aliyekuwa anamsumbua na jamaa wanaoshughulika na haki za wanyama wamemtumia kadi ya kiutani ingawa lengo lao nadhani lilikuwa ni kusema kwamba kwa vile yeye ni rais basi asingefanya hivyo na anaonyesha mfano mbaya.

Kuna wanaoiamini Biblia kwamba wanyama waliumbwa ili wamtumikie binadamu naye ni mtawala wao (ingawa siungi mkono kuteswa kwao ingawa nawala pia) Huyu jamaa angetafuta tenga akamtia huyo mbuzi humo na kumsafirisha kwa raha na akishamfikisha huko anakomplekea basi amchinje kwa usalama na kumla!

Anonymous said...

Ipo siku wanyama wataja kuandamana kama unyanyasaji kama huu utaendelea ,huku kwetu Tanzania wabunge wapo katika mchakato wa kupitisha sheria itakayowabana wananyasaji wa wanyaka kama huyu bwana ,picha nzuri nimeipenda sana
By Francis Godwin,Iringa kusini mwa Tanzania