Wednesday, October 31, 2018

BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO IMECHAGUA HII PICHA IWE YA MWISHO WA MWEZI....USALAMA BARABARANI...

Tuwe waangalifu tuwapo barabarani hii ni hatari sana kwa mwendesha pikipiki na mteja pia wapita njia.
NACHUKUA NAFASI HII KUWASHUKURUNI KWA USHIRIKIANO WENU MZURI DAIMA NA HASA MWEZI HUU ULIOISHA NA PIA TUUKARIBISHE MWEZI WA KUMI NA MOJA KWA FURAHA. PIA TUSISAHAU KUKUMBUKANA:-)...Kapulya.

Monday, October 29, 2018

MAPISHI YA LEO KANDE, MAHINDI NA UGALIWA KUCHOMA/KUOKA

 Katika chungu ni kande zikipikwa na pembeni yake mahindi yakichomwa yaani raha hasa kipindi kile cha masika.
Ugali uliolala usitupe, choma/oka ni kitafuno kizuri saba kwa chai asubuhi....jaribu utaona utamu wake.... panapo majaliwa ttutaonana tena karibuni.

Thursday, October 25, 2018

PICHA YA LEO:- MARA NYINGI NIKIPITA NJIA HII YA IRINGA NI LAZIMA NISIMAME HAPA KUNUNUA SAMAKI

Ukiwa njiani utakutana na wachuuzi wa samaki, kama huyu mama ...picha kwa hisani ya Mjengwa.

Monday, October 22, 2018

WIKI ILIYOPITA TULIKUWA SONGEA MKOANI RUVUMA TUKIANGALIA MILIMA LEO TUENDELEE MBELE KIDOGO MPAKA MBINGA ILI KUANGALIA MANDHARI NZURI YA KIJIJI CHA LITEMBO

 NIMEYAPENDA HAYA MAZINGIRA
 Ebu angalia kulivyokuwa kwa kijani mpaka raha hata kama unapita tu lazima utasimama

Hapa nahisi ni Ofisi kama wasoma kibao/bango

Friday, October 19, 2018

ASILI YA KABILA LA WANGONI SEHEMU YA KWANZA


Wangoni ni kabila la watu wa Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Ruvuma, hasa upande wa Kusini wa Songea. Pia wako Msumbiji. Lugha yao ni Kingon

Wednesday, October 17, 2018

LEO TUTEMBELEE KWETU SONGEA KIJIOGRAFIA

 Huu ni mlima MATOGORO uliopo kkaribu na kijiji cha MAHILU kilichopo Songea
 Hapa ni magharibi ya kijiji cha Mhukuru twakutana na mlima kipululu
 Mlima Litimbanjuhi uliopo karibi na kijiji cha Namatuhi
 Hapa pia ni mlima Manolo uliopo kijiji cha Namatuhi pia
Kama  watoka Wino kuelekea Iringa utaona mandhari hii nzuri ya milima

Monday, October 15, 2018

JUMATATU HII TUTEMBELEE MJI WA IRINGA

Napenda kuwatakia Jumatatu njema na kila la kheri kwa chochote  mtakachofanya.  PAMOJA DAIMA

Wednesday, October 10, 2018

UTALII WILAYANI NYASA:- LEO TUFANYA UTALII KWENYE UFUKWE ULIOPOMJINI LIULI

     

Utalii ni sekta inayokua kwa kasi sana Duniani. Imechangia katika kukua kwa uchumi wa nchi nyingi sana, imeongeza ajira nyingi sana, zipo zile za moja kwa moja na zingine ambazo si za moja kwa moja.

Sehemu zinazo wavutia sana watalii si mbuga za wanyama, si milima, si mapango bali fukwe nzuri na tulivu za bahari na maziwa.
Uswisi inajulikana kama 'the playing ground of europe' kutokana na ziwa dogo la Geneva, Visiwa caribean, Zanzibar, Mombasa na kadhalika zimekuwa zikiwavutia sana watalii kutokana kuwa na fukwe zinazovutia.
Ziwa Nyasa ni moja ya maziwa safi bado halijaharibiwa na shughuli za kibinadamu.Lina fukwe nzuri,safi na salama,maji meupe kwa ajili ya michezo mbalimbali...kama mashindano ya kuogelea, mbio za madau au maboti.
Watu wa Nyasa, ili nionekane mkweli kuhusu fukwe zetu mimi naonesha mfano-Ufukwe wa LIULI.
Na John Joseph, Liuli
 

Wednesday, October 3, 2018

TANGU WAKIWA WADOGO HUPENDA KUJITUMA, LAKINI JAMII HAIWAAMINI

Wiki hii tuanze na picha hii..yaani kama ujumbe usemavyo hapo juu....NAPENDA KUWATAKIENI WIKI NJEMA NA PIA JUMATANO NJEMA....KAPULYA WENU!!