Showing posts with label maua. Show all posts
Showing posts with label maua. Show all posts

Saturday, April 12, 2014

MAUA MAZURI YAPENDEZA...NAPENDA SANA MAUA NIMEPATA HILI KAMA ZAWADI NA....:-)

NIKAONA NILIIMBIE NA HUU WIMBO TULIOKUWA TUKIIMBA ENZI ZILEEEE je nawe unakumbuka kama hukumbuki basi ni hivi kuimba!!!
1. Maua mazuri yapendeza x 2
    Ukiyatazama utachekelea
    Hakuna mmoja asiyeyapenda x 2

Kwa kutaka kuimba bila kukosea basi fuata hii hapa:-)
 Au pia tusiwasahau na watoto, si mnakumbuka na huu wimbo  haya wazazi waimbieni watoto wenu  kwa raha zote ni kama vile umsomeapo/msimuliapo hadithi :-
2.Mtoto msafi apendeza x 2
Ukimtazama utachekelea
Hakuna mmoja asiyependeza x 2
 
3. Mtoto mtii apendeza x 2
Ukimtazama utachekelea
Hakuna mmoja asiyempenda x 2

JUMAMOSI IWE YENYE UPENDO, FURAHA  JUU YA KICHEKO. SI MNAJUA KUCHEKA/KICHEKO NI DAWA ISIYOLETA MADHARA.
KUMBUKENI TUPO PAMOJA!!


Thursday, May 16, 2013

MAANDALIZI YA BUSTANI ZA MBOGA NA MAUA YAMEANZA...ANGALIEANI WENYEWE...KARIBUNI TUJUMUIKE!!!!

 Hapa ni baadhi ya matu ya bustani yangu ...maandalizi yameanza..leo mnaona udongo tu hapa baada ya wiki mtaona mimea....
 Katika maisha inabidi uwe mtundu hapa nilikwisha andaa baadhi ya miche kama vile NYANYA na Miche ya mboga ZA MABOGA,,ujanja eeeehhh
Mdada/kapulya hapendi shughuli za bustani za mboga tu ni mpenzi sana wa bustani sana wa bustani za maua kama mnavyoona hapa na mawe pia....kwa hiyo msione nipo kimya nipo ...daima pamoja...anayejisikia kuja kusaidia anakaribishwa..majembe yapo mengi tu:-)

Thursday, May 3, 2012

MTU NA MAZINGIRA:- MAMBO AMBAYO NIYAPENDAYO KATIKA MSIMU HUU NI BUSTANI YA MAUA NA BUSTANI YA MBOGAMBOGA!!!

 Kwa hiyo mkiona sionekani hapa basi nipo nje naongea na maua yangu. maua haya leo nimeyapatia kulikuwa na jua kwa hiyo mchana yanachanua ikifika jiona/jua lizamapo nayo hufifia. Jina sijui ...nitatafuta nikijua nitawajuza....
 Hapa napo hili ua rangi zake nazipenda sana ila nalo jina sijui kwa kiswahili ila kiswidi ni (RÖDVIVA/GULLVIVA)
Na haya hapa nilipanda mwaka jana mwezi wa kumi na sasa yapo hivi ni yanaitwa(Tulpaner) mmmhh itabidi nijifunze kwa kiswahili...Bustani ya mboga bado sijaanza kwani bado ni baridi kweny udongo....Mija, Rachel, Edna Simon, Kaka S, aahh! na wengine wote nitawajuza itakapokaribia si mnakumbuka  huwa kuna ushirika wa kulima/chama  na baada ya kulima kupiga UGIMBI au mmesahau?...:-)...
.Halafu mwenzenu nina UDHAIFU SANA WA MAWE kuna mawe mengine ni kutoka TZ na sehemu mbalimbali niendako:-) JIONI NJEMA SANA JAMANI NGOJA MIE NIENDELEE kuongea NA MAUA YANGU......pia MAWE.....

Saturday, May 22, 2010

Swali:- Mmmea huu una sumu au ni uzushi?

Nimeletewa ujumbe huu jana na dada Penina kwa kuwa hili ua ni hatari na nimeona niweke hapa ili kufikisha ujumbe huu na kwa wenzangu.

Upo ujumbe unaozunguka katika barua Pepe ukifahamisha Rangi kuwatahadharisha Watu kuhusiana Rangi mmea ambao wengi wetu tunaufahamu kama Ua ama pambo la nyumbani. Ujumbe umeandikwa Kwa lugha ya Kiingereza lakini mdau Ray Njau ameutafsiri Kwa lugha ya Kiswahili mama ambao unasomeka hivi:

Unaoonekana pichani mmea unapatikana Kwa wingi nchini Cameroon (Hata hapa Tanzania), ofisini, majumbani Rangi kwenye bustani, Ni sumu hasa Kwa Watoto, unaweza kumuua Mtoto ndani ya dakika 15 baada ya kuweka Tu kinywani. Ukigusa huweza kusababisha upofu macho "Wa kudumu.

Swali: Je Habari Hii INA UKWELI WOWOTE AU Ni ya UDANGANYAFU Tu?