1. Maua mazuri yapendeza x 2
Ukiyatazama utachekelea
Hakuna mmoja asiyeyapenda x 2
Kwa kutaka kuimba bila kukosea basi fuata hii hapa:-)
Au pia tusiwasahau na watoto, si mnakumbuka na huu wimbo haya wazazi waimbieni watoto wenu kwa raha zote ni kama vile umsomeapo/msimuliapo hadithi :-
2.Mtoto msafi apendeza x 2
Ukimtazama utachekelea
Hakuna mmoja asiyependeza x 2
3. Mtoto mtii apendeza x 2
Ukimtazama utachekelea
Hakuna mmoja asiyempenda x 2
JUMAMOSI IWE YENYE UPENDO, FURAHA JUU YA KICHEKO. SI MNAJUA KUCHEKA/KICHEKO NI DAWA ISIYOLETA MADHARA.
KUMBUKENI TUPO PAMOJA!!
