Thursday, December 31, 2015

SALAMU/BARUA KUTOKA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO:- SHUKRANI KWA WOTE!!!

Mmmhh! huyu Twiga kanipita urefu nitafika huko kweli...

Habari zenu jamani!!
Yamebakia masaa machache tu kuumaliza mwaka huu 2015 na kuingia katika mwaka mpya 2016. Hakika miaka inayoyoma na watu tunazidi kuzeeka. Ninachotaka kusema ni kwamba, blog ya MAISHA NA MAFANIKIO inapenda kuwashukuru wanablog wenzake wote, wasomaji wote na watembeleaji wote kwa ushirikiano mzuri tulioonyeshana.

Najua katika maisha watu wote hawawezi kuwa sawa yaani kimawazo. Lakini katika hizi blog zetu kwa asilimia kubwa imekuwa ni changamoto kwetu. Tumekuwa hatupendi kupoteana, mara mmoja wetu anapokuwa kimya kwa muda basi wengine tunakuwa hatuna raha tunachukua hatua ya kumtafuta. Hii yote inaonyesha ni jinsi gani ukaribu wa wanaBLOG sisi tu/ulivyo, hakika najivuna sana kwa uwepo wenu na kwa hili napenda kusema SISI SOTE NI NDUGU. NA PIA NAPENDA KUWATAKIENI WOTE KILA DOGO NA PIA KILA KUBWA MTENDALO LIWE JEMA. NA MWAKA 2016 UWE WENYE MAFANIKIO. KAMA KUNA KITU ULIAHIDI KUFANYA MWAKA HUU BASI JITAHIDI UFANYA KABLA HAUJAISHA. KWANI KUMBUKA HAKUNA KISICHOWEZEKANA. NA PIA KAMA KUNA KITU AU MTU NILIMKWANZA BASI NAOMBA TUSAMEHEANE KWANI HAKUNA BINADAMU ALIYEKAMILIKA. PAMOJA DAIMA. KAPULYA WENU!!!!

Tuesday, December 29, 2015

KARIBUNI TULE EMBE.....

Wandugu mpo  ule msimu wa kula embe sasa umefika. Karibu  tujumuike...duh! Ama kweli  watu tumetoka mbali. ..maisha haya. ...

Monday, December 28, 2015

PALE HALI YA HEWA INAPOBADILIKA...LEO ASUBUHI ILIVYOKUWA/DET SNÖAR!

Mila na desturi au nisema ni mazoea ya nchi nyingi za Ughaibuni/ulaya siku ya Krismas kuwa na thaluji yaani kweupe huko nje lakini krismas hii haikuwa hivi hasa Swedan badala yake theluji imeanguka jana 27/12 mpaka leo 28/12 na kamera ya maisha na mafanikio imebahatika kupata picha hizi kama uonavyo...
Wakati mwingine ni safi kuacha gari na baiskeli na hapo ndipo utakapofaidi mambo angalia hii picha  hapa nilikuwa nikitoka mazoezi ya asubuhi:-) pia ni vizuri kutembea/kimbia na kamera......

 Basi nikalipokaona hako kajua nikaanza kuimba kala kawimbo ka mchakamchaka ....Jua lile...nikabadili nikaanza kuimba Idiamini akifa mimi siwezi kulia......Kama nilivypsema Ujenzi unabana ila leo nimepata kamuda...na pia sasa nitapumzika kidogo na ujenzi mpaka huu mwaka uishe ndo tutaendelea...Bado siku 4-3½ hivi kuufikia mwaka  mpya...TUOMBEANA  ILI TUWEZE KUUONA ...NI MIMI KAPULYA WENU!!


Friday, December 25, 2015

NAWATAKIENI WOTE KRISMASI YENYE UPENDO, AMANI, FURAHA NA BARAKA TELE!!

Kamera ya Maisha ya Mafanikio ilikuwa mitaani lao na imepata picha hii ya mtoto Yesu..Hapa Papa Franciskus akimkabidhi mtoto Yesu  ili aende akalale holini ....Mwokozi amezaliwa. Na sasa hebu tusikilize mwimbo huu ambao ni zilipendwa wale wote wenye umri kama mimi na zaidi nadhani watakuwa wanaukumbuka..KARIBUNI.

YESU NDIYO SABABU YA KUWA NA HII SHEREHE YA KRISMASI...KWA HIYO BASI TUWE NA KRISMASI YENYE UPENDO, AMANI, FURAHA NA BARAKA....KRISMASI/NOEL NJEMA.

Tuesday, December 22, 2015

KUFANIKIWA SI LELEMAMA YATAKA MOYO NA UVUMILIVU NA KUJITUMA....!

Mara nyingi nimesikia watu wakisema, aise fulani yule  ana maendeleo sijui inakuwaje. Ni kwamba amevumilia, badala ya kula nyama kala mchicha kila siku, kanywa maji kila siku, kalala kwenye mkeka na hata mwanzo wa maendeleo yake ni biashara ndogondogo/ genge. Lakini utakuta wengine wengine wakikaa na kusubiri wakidhani watashushiwa na Mungu. ...TUJITUME NA MAFANIKIO TUTAYAONA.....KILA LA KHERI TUPO PAMOJA!!!

Sunday, December 20, 2015

HII NI ZAWADI YANGU YA LEO NILIYOTUMIWA NA RAFIKI AJUAYE YA KWAMBA NAPENDA VITUMBUA

Napenda kusema AHSANTE kwa zawadi. Pia nawatakieni wote JUMAPILI HII YA MWISHO KABLA KRISMASI.....KAPULYA

Friday, December 18, 2015

Tuesday, December 15, 2015

UJENZI WA NYUMBA ....MKIONA NASUASUA BASI MJUE NIPO KATIKA ZOEZI LA UJENZI WA NYUMBA.....MBINGA

 HAPA NI MSINGI WA NYUMBA INAANZA ...NI SEHAMU YA MABANDA NIMEANZA
 BAADA YA SIKU KADHAA ILIFIKIA HAPA NI  KAMA MUONAVYO NI MATOFALI YA KUCHOMA
 HAPA NYUMBA IPO TAYARI NA SASA KENCHI ZINAPANDISHWA....NA NI MWONEKANO KWA NYUMA,,
 HAPA WAWEZA KUONA KENCHI ZIMEKWISHA PANDISHWA NA NI MWONEKANO KWA MBELE......
HAPA TAYARI TUMEEZEKA ...KAMA NILIVYOSEMA NIMEANZA NA MABADA  NA NI NUSU TU YA SAFARI........PICHA ZAIDI ZITAKUJA:-) KILA LA KHERI  PAMOJA DAIMA. KAPULYA WENU.

Thursday, December 10, 2015

IWE PICHA YA WIKI HIII....

Sasa hapo sijui atakulaje  huo ugali? Niwatakieni kila la kheri ..pamoja daima... Kapulya

Wednesday, December 9, 2015

LEO NI TAREHE 9/12 AMBAYO N I MIAKA 54 YA UHURU TANZANIA ...LAKINI MWAKA HUU RAIS KASEMA WANANCHI WOTE KATIKA SIKU HII WACHUKUE MUDA NA KUFANYA USAFI...

Na kama unavyoona katika picha wananchi wapo bega kwa bega katika zoezi hili la usafi katika hii siku.  Halafu naona hata Mh. Rais mstaafu Jakaya Kikwete naye  hayupo nyuma....

Tuesday, December 8, 2015

TUNDA LA PERA SIO TUNDA TU ISIPOKUWA :- MAJANI YA MPERA KWA NYWELE ZINAZOKATIKA NA KUPUNGUA

Wanawake wengi wanaopenda urembo wa nywele wamekuwa wakihangaika hata  kama bei mbaya kisa tu kujaza nywele kichwani na kuzifanya zisikatike.
Wasiokuwa na muda wa saluni na wasiokuwa na hela hizi ni habari njema kwao kwamba majani ya mpera ni mazuri kwa kukuza nywele na kuzitibu zile zinazokatika.
Jinsi ya kuyatengeneza kama dawa
Chukua majani yanayotosha kwenye kiganja chako kisha weka kwenye sufuria yenye lita moja ya maji, chemsha kwa muda wa dakika 15 mpaka 20.
Baada ya hapo, yaache yapoe kisha paka kwenye nywele zako kuanzia kwenye mzizi wa nywele mpaka mwisho.
Ukimaliza fanyia masaji nywele zako kama mtu anayepaka mafuta nywele zote.
Baada ya hapo unaweza kuacha kwa muda  kisha ukaosha.
Fanya hivi mara kwa mara, naamini utaona mabadiliko.

Monday, December 7, 2015

MRADI WA MAJI KUCHIMBA MTARO NA KUWEKA MABOMBA: HAPA NI KUSINI MWA TANZANIA KATIKA KIJIJI CHA MUHUKURU WANANCHI WAPO KATIKA KAZI YA KUPATA MAJI SAFI ONA WANAVYOSHIRIKIANA....

 Maji ni uhai wananchi wakiwa bega kwa bega kivhimba mtaro.
 Mtoto naye hayupo nyuma kushiriki zoezi hili muhimu.
Haikuishia hapo..Vijana nao wanashiriki kwa makini zoezi hili la mitaro.

Sunday, December 6, 2015

HII NI JUMAPILI YA PILI YA MAJILIO:- NA LEO TUANGALIE MAANA YA MAJILIO KATIKA MAISHA YA BINADAMU

JUMAPILI YA PILI(2) YA MAJILIO
Sisi binadamu hatuwezi kuishi daima katika hali ileile bila ya matazamio. Hasa kijana anatarajia mambo mapya tena mema. Hivyo tunajitahidi kuyapata. Asiyetazamia chochote amevunjika moyo, hana hamu ya kuishi. Lakini matazamio ya kibinadamu yakimfikia mtu hayamridhishi moja kwa moja. Kristo tu anatimiza hamu zote kwa kumkomboa kutoka unyonge. Majilio yanatukumbusha kila mwaka matarajio ya kweli na hivyo yanaamsha hamu ya kuishi kwa bidii ya kiroho.
BASI WOTE MUWE NA AMANI PIA UPENDO KATIKA JUMAPILI HII YA PILI YA MAJILIO NA SIKU ZOTE....AMINA!

Friday, December 4, 2015

AKAMWAMBIA MKEWE AMKATE KICHWA!

Leo nimemkumbuka sana mdogo wangu KOERO MKUNDI kumsoma zaidi gonga hapa...  http://koeromkundi.blogspot.se/

Karibu mgeni Sungura
Hapo zamani za kale Sungura alijenga urafiki na Jogoo, sasa siku moja Jogoo akamualika Sungura amtembelee nyumbani kwake. Basi sungura akajikusanyia zawadi zake na kumuaga mkewe kisha akaondoka kwenda kumtembelea rafiki yake Jogoo.

Alipofika alikaribishwa kwa bashasha na jogoo, na aliandaliwa chakula kitamu na wenyeji wake, baada ya kula Jogoo alimtoa mgeni wake huyo na kumtembeza sehemu mbali mbali ili kumuonesha fahari ya mji wao, Sungura alipendezwa sana na ziara hiyo.

Ilipofika jioni walirudi nyumbani wakamkuta mke wa Jogoo kawaandalia chakula cha jioni, baada ya kula Sungura alioneshwa mahali pa kulala, kisha jogoo na mkewe nao wakaingia chumbani kwao kulala. Lakini kabla sungura hajapitiwa na usingizi akasikia mazungumzo ya jogoo na mkewe huko chumbani kwao, na mazungumzo yenyewe yalikuwa ni haya.
Jogoo: Mke wangu nikate kichwa nataka kulala mie.
Mke wa Jogoo: Sawa mume wangu,
Sungura kusikia hivyo akataharuki, “He kumbe Jogoo kulala ni mpaka akatwe kichwa? Ilipofika alfajiri akamsikia Jogoo akimuamsha mkewe tena.
Jogoo: Mke wangu, eh, hebu nirudishie kichwa changu nataka wika mie kuwaamsha watu.
Mke wa Jogoo: Haya mume wangu ngoja nikurudishia kichwa chako. watu.

Baada ya kurudishiwa kichwa chake, jogoo akaanza kuwika kama kawaida yake,ili kuwaamsha watu…Koko rikooooo ………Kucha kucheleeeeeeee………

Basi kulipopambazuka sungura akaamka na kupata staftahi iliyoandaliwa na wenyeji zake na baada ya stafutahi akapewa zawadi za kwenda nazo nyumbani kwake, lakini kabla ya kuondoka aliamualika Jogoo naye amtembelee ili kulipa fadhila kwani alipanga kumfanyia jogoo mapokezi makubwa kushinda yale aliyoyapata.

Sunguara alipofika nyumbani kwake alimsimulia mkewe juu ya safari yake na mapokezi aliyoyapata, pia hakusahau kumweleza mkewe mshangao alioupata kuhusiana na ule utaratibu wa Jogoo kukatwa kichwa na mkewe kabla ya kulala na kurudishiwa kichwa chake alfajiri ili awike.

Sungura alimtaka taka mkewe na yeye afanye hivyo siku wakitembelewa na Jogoo, kwa kuwa amemwalika aje kuwatembelea, alimtaka mkewe amkate kichwa akitaka kulala, na kukirudishia alfajiri ili amwonyeshe jogoo kuwa na yeye anaweza kukatwa kichwa na kurejeshewa asubuhi.

Ni kweli baada ya juma moja kupita Jogoo akamtembelea Sungura, na yeye alibeba zawadi kemkem kwa ajili ya wenyeji wake.

Alipofika alipokelewa na wenyeji wake ka bashasha, na kuonyeshwa ukarimu wa hali ya juu.

Kama alivyofanyiwa kule na Jogoo, na yeye Sungura alimtembeza mwenyeji wake kumuonesha mji na maeneo ya vivutio vya mji wao.

Walirejea jioni na kupata mlo wa usiku, huku wakipiga soga. Ulipofika muda wa kulala, sungura alimuonesha jogoo mahali pa kulala, na yeye na mkewe wakaingia chumbani kwao kulala.

Mara Sungura akamwambia mkewe.

Sungura: Mke wangu eh, hebu nikate kichwa mie nilale..
Mke wa Sungura: Sawa mume wangu.
Mke wa Sungura akachukua kisu na kumkata mumewe kichwa, na kukitenganisha na kiwiliwili.

Asubuhi kulipopambazuka akaanza kumuamsha mumewe,a lakini hakuamka alijitahidi kukiunganisha kichwa ili mumewe aamke lakini hakikuunga na wala Sungura hakuamka, alikuwa amekufa tayari.

Mke wa Sungura ikabidi aombe msaada kwa Jogoo, lakini Jogoo alipofika chumbani aliona damu zimetapakaa kila mahali na kichwa cha Sungura kilikuwa kimetenganishwa na kiwiliwili.
Jogoo kuona hivyo, akataharuki, lahaulaaaa…kulikoni huyu hana kichwa, aliauliza Jogoo.
Mke wa Sungura akamsimulia Jogoo kuwa utaratibu wa kukatwa kichwa kabla ya kulala aliupata kutoka kwake alipowatembelea.

Ndipo Jogoo akamwelewesha kuwa yeye huwa hakatwi kichwa na mkewe kama vle alivyofanya Sungura bali mkewe humsaidia kuficha kichwa cheke kwenye mbawa zake kila akitaka kulala na alfajiri mkewe humsaidia kutoa kichwa chake kutoka kwenye mbawa ili aweze kuwika kuwaamsha watu.

Mke wa Sungura liaposikia hivyo akaanza kulia kwa uchungu kwa kuondokewa na mumewe.

Jogoo aliporudi kwa mkewe alimsimulia masaibu yaliyomkuta Sungura.

Hadithi hii nilisimuliwa na bibi yangu Koero, siku nyingi kidogo, wakati nilipokwenda kijijini likizo. Nimeikumbuka leo nikaona si vibaya nikiiweka hapa ili tutafakari pamoja.

Je hadithi hii inatufundisha nini? Tafakari………………………

Koero Mdogo wangu huko uliko ujue unakumbukwa sana na wote hasa mimi dada yako kwa hiyo usomapo ujumbe huu nitafuta TAFADHALI...Dadayo Yasinta /kapulya....Ahsante kwa hadithi hii.

Sunday, November 29, 2015

MIMI "KAPULYA" NA DADA YANGU ANNA TWAPENDA KUWATAKIENI MWANZI MWEMA WA MAJILIO

Ndani ya migolole ntu na dada yako. Tumependeza eeehh-:) Wote kama tunavyojua majilio:- ni majuma manne ambayo ni kama kifananisho cha miaka elfu nne ambayo Wakristo hujiandaa kukumbuka siku aliyozaliwa Yesu  Kristo. Amina.

Friday, November 27, 2015

Monday, November 23, 2015

TUANZE JUMATATU YA LEO NA PICHA HII NA IWE PICHA YA MWEZI.....

Ni wasomi ambao ni Taifa la kesho, wakiwa wamevalia "kisomi zaidi" Najaribu kuwaza kama hapo mchakamchaka utaenda salama kweli? Au wenzangu unasemaje? Tuliangalie hili jambo kwa pamoja!!

Saturday, November 21, 2015

UJUMBE WA LEO TOKA KWA KAPULYA WENU......

Napenda kwatakieni wote Jumamosi njema. Panapo majaliwa tutaonana katika pitapia zetu au sivyo wandugu-:).

Wednesday, November 18, 2015

KATIKA DUNIA MAJI NI MUHIMU SANA KWA UHAI WA BINADAMU KAMA TUONEVYO KATIKA PICHA HII...

Akina baba hawa:- WanataFuta maji kwenye chanzo- Ni mradi wa maji ya mtiririko Kijiji cha Liganga. Picha nimeipata katika KALENDA 2015

Monday, November 16, 2015

POMBE SI MAJI....NA WALA SI RAFIKI ILA POMBE NI HATARI KATIKA MAISHA YETU.....


Karibu wiki  mbili  zilizopita nilishuhudia kisa hiki cha kusikitisha ambacho sitakisahau katika maisha yangu. Na kimekuwa fundisho katika maisha yangu. Ilikuwa siku ya  jumatano ya tarehe 5/11/2015, majira ya saa mbili asubuhi. Kulikuwa na mkusanyiko wa wafanyakazi ambao walitakiwa kuwa kwenye mafunzo (kozi). Sasa kwa bahati naweza nikasema bahati  mbaya dada mmoja jina nalihifadhi ila tumwite Maria. Alitoweka ghafla pamoja na bosi bila "wengine" kujua nini kimemkumba  dada Maria.

Lakini baada ya muda habari zikaja ya kwamba kuna wafanyakazi wenzake walipokuwa wakiongea na  Maria , wao waligundua harufu ya kinywa cha Maria ilikuwa inanuka pombe. Nao hawakuishia hapo, wakapeleka ripoti kwa bosi. Na hicho ndicho kilikuwa kisa cha Maria kutoweka ghafla. Kilichoendelea, Maria alipelekwa sehemu ili kuhakikisha kama kweli alikuwa na pombe katika mwili/damu yake. Majibu yalionyesha ni kweli Maria alikuwa na pombe mwilini. Siku ya Maria ilikuwa ni kitendawili alirudishwa nyumbani hakuweza/hakuruhusiwa kuhudhuria ile kozi  siku ile. Na mbaya zaidi ile siku ilipotea bila kulipwa alikatwa mshahara wake.

Niliwaza sana na kumfikiria dada Maria na nikaishia kusema ama kweli sheria kama hizi zingekuwepo dunia nzima :- Basi maendeleo yangekuwepo. Nikawaza  nchi nyingi zingekuwa na maendeleo sana kama zingefuata sheria zilizowekwa. Nikaanza kukumbuka nilipokuwa msichana mdogo nilivyokuwa nikiwaona baadhi ya walimu walikuwa wakienda kupata kupata "chai ulanzi" badala ya chai ile saa nne.  Je? hao vinywa vyao vilikuwa vikitoa harufu kiasi gani? Lakini hakuna sheria yoyote ilichukuliwa  na kama ingekuwa ikichukuliwa sheria je? Wangapi wangepoteza kazi zao?

NENO LA LEO:- NDUGU ZANGUNI POMBE SI MAJI NA WALA HAZITATUI MATATIZO. ISIPOKUWA ZINAHARIBU AFYA NA MWISHO ZINAUA.

Friday, November 13, 2015

MAJINA YA WANAUME NA SIFA ZAO KATIKA MAPENZI......JE? ULIJUA HILI? KARIBU......

1. Andrew-mapenzi ya tamthiliya
2. Nicolas-muongo
3. Albert-domo zege ila mjanja mjanja
4. Mathias-anapenda mwanamke kwa muda mrefu
5. Joseph/Josephat/yusuph-kicheche
6. Jeryson-anapenda mademu ila wanawake wanamkataa
7. Shadrack-anapenda sifa kwa mademu
8. Richard-ana wapenzi wengi ila msiri
9. Mathew-anapendwa na wanawake ila domo zege
10. Thomas-anapendwa na mademu ila hajatulia
11. Prosper-hajui habari za mapenzi
12. Fidelis-mtaalam wa kutongozea mademu wenzie (kuwadi)
13. Aaron-maneno mengi ila vitendo sifuri
14. Costantine-wanapenda kutongoza hovyo ingawaje wana mpenzi mwaminifu
15. Elvis-handsome ila hapendwi na mademu
16. Edward-serious sana kwenye mapenzi
17. Moses/Mussa-mwepesi kutongoza na mwepesi kuwacha
18. Ally/Elly-wasiri sana kwenye mapenzi
19. Mohammedy-anapenda watu waliomzidi umri
20. Nickson-wakiingia kwenye mapenzi wanatendwa vibaya
21. Alpha-wanapenda sifa kwa wanawake ili wapendwe
22. Jimmy-wana mapenzi ya kejeli
23. Elias-wanapenda mademu ila wanaogopa kuwaambia
24. Frank-huyu mpole wanawake wanajitongozesha wenyewe
25. Joachim-hana habari na mademu,anaamini ipo ataoa tu
26. Omary-anapenda achape tu atembee
27. Steven-hana habari kabisa na wanawake ila ana bahati ya kupendwa
28. Gerald-mpole na antulia na mpenzi mmoja kwa mda mrefu
29. Elisha-anapenda wanawake wanaochukiwa katika jamii
30. Benard-akipenda kapenda
31. Juma-hawa kazi yao ni kuchafua wanawake wa mtaani na jamii inayozungukwa

32. Kassimu- anapend utukufu na kusifiwa hata na mkewe
33. Khalid -msumbufu na anapenda kupedwa kuliko kupenda wanawake
34. Daniel-anawivu sana mjanja na anapenda kujua mambo yaliyojuu ya uwezo wake.
35. Said-hajui kupenda na huwa anatamaa hasa kwa bint weupe.
36. Rajabu-mgumu kumuamin mwenza wake.
37. David-Kupenda kujionesha mbele ya wanawake kwamba anauwezo mkubwa hata kama hana.
38. Farid-Mpenda wanawake warefu wenye mwanya na shepu.
39. Rama-hupenda kusikilizwa yeye tuu na anapenda wanawake wenye makalio makubwa hasa wanene.
40. Seleman-anapenda ngono.
41. Issa -huwa na msimamo hasa katika maamuzi yake hat kwa mwenza wake
42. Fadhili- vitu vyake ni vya siri saana na hata mwenza wake ni ngumu kujua
43. Charles -Hapend kudumu katika mahusiano na hupenda kuwa pek yake
44. Karimu- hupenda kuwa na wanawake weupe
45. Laurence-hunyanyasika kwenye mahusiano hata huweza kulia hovyo
46. Masoud- anajua kujali na kuheshimu ndoa yake ila mkali sana.
47.Hamad-mpole pia hapend kutoa siri zake kwa mwenza wake pia hupend kunyenyekew na mpenz wake
48. Hasani -hupenda kupewa kuliko kutoa hata kwa wenza Wap
49. Alen-hupenda kulaumu hata kwa jambo dogo na hupend wanawak weupe
50. Luka- wanapenda kwa mda ukijichanganya utaumia ukiwa nae.
51. Jafari- Hupenda wake za watu

Thursday, November 12, 2015

NDUGU ZANGU ULE MSIMU WA KUANZA KUANDAA MASHAMBA UMEFIKA KWA HIYO JEMBE BEGANI....

Twendeni kuandaa mashamba/ sisi wangoni tunasema (KUSANGILA) yaani maandalizi. Ila nawaombeni hakuna kuchoma moto... kwani ni kuharibu ardhi. Atakaye chelewa anarukiwa matuta:-)

Tuesday, November 10, 2015

TUNAPOISHI MAISHA YA WENGINE NA KUSAHAU YETU!!!

Maisha ya binadamu hapa duniani yanaanzia pale ambapo natoka kwenye tumbo la mama yake, japokuwa inawezekana kabisa binadamu alianza kabla ya hapo lakini kwa hapa duniani tunaanza kumhesabu kuwepo pale ambapo anatoka kwenye tumbo la mama yake na ndio maana umri wake unaanza kuhesabika kuanzia siku hiyo.

Binadamu huyu anapokuja hapa duniani kwa njia ya kuzaliwa wenyeji wake wa kwanza kabisa ni wazazi wake na ndugu zake wa familia hiyo kwa maana ya kaka na dada zake kama watakuwepo, hawa wenyeji wake wa kwanza ndio ambao wanaanza kumuelekeza na kumuonesha namna ya kuishi hapa duniani, kwa bahati mbaya sana ni kwamba hawa wenyeji kama wana mitazamo mibaya kuhusu maisha na dunia kwa ujumla ndivyo ambavyo mgeni huyu nae atayachukulia maisha ya hapa duniani kwa namna hiyo hiyo kwasababu wenyeji wake wamemuelekeza hivyo na kwasababu yeye ni mgeni basi hatakuwa na namna ya kupingana nao kwakuwa hajui lolote kuhusu maisha haya na dunia kwa ujumla.

Kimsingi makala yangu hii itaegemea sana hapo ili kuweza kuelezea kile ambacho ninataka kukielezea leo, wenyeji wetu hawa mara nyingi kama sio zote wametuaminisha na kutufundiosha mambo mengi sana ambayo yanakuja au yamekuja kutuumiza kwenye maisha yetu, kwanza kabisa kuna mambo ya aina mbili katika maisha yetu hapa duniani, nitajitahidi kuelezea kwa lugha rahisi kabisa ili niweze kueleweka zaidi.
1: Mabaya
2: Mema
Japokuwa kimsingi mambo yote haya yanategemea namna mtu mwenyewe anavyoyachukulia au kutafsiri baya na jema lakini bado haiondoi ukweli kuwa yote hayo yapo, kwa bahati mbaya au nzuri karibia binadamu wote tunayafasiri mambo haya kwa namna inayofanana hivyo tunajikuta kama ni matatizo basi tunakuwa na yale ya kufanana.

Wataalam wa masuala ya malezi wanasema kuwa binadamu anapokuwa na umri wa kuanzia mwaka 0 hadi 6 pale ndipo anapokuwa anaanza kujifunza na kuelewa mambo kwa kiwango cha juu sana kwenye mawazo yake ya kina, binadamu tuna mawazo ya aina mbili, kuna yale ya kawaida na yale ya kina ambapo ndipo "uhalisia" wa maisha yetu unajengwa, hili nitalielezea siku nyingine kwa kina, sasa basi wakati mtoto huyu anaandika mambo haya kwenye ubongo wake ambao unakuwa ni "mweupe" au kwa lugha nyingine tunasema uko mtupu kabisa mtoto huyu au binadamu huyu mpya anakuwa anaanza kujenga kitu kinachoitwa tabia.

Wataalam wanasema kuwa atakaeweza kuja kufuta kile ambacho mtoto amejifunza kwenye umri huo ni yeye mwenyewe tena kwa juhudu hasa maana sio kazi ndogo, katika kipindi hiki ndipo wengi wetu tunaharibikiwa au kuharibiwa na ndio kiini cha karibu kila tatizo katika maisha yetu, hata namna unavyoiona dunia na kuichukulia na namna unavyoyachukulia mambo chanzo chake ni huku, lakini pia kuna kipindi kingine ambacho binadamu huyu anaweza kujifunza ambacho ni cha miaka 7-18, inadaiwa kipindi hiki hakina nguvu sana kama kile cha utotoni japokuwa hata hiki nachoi kinaweza kumfanya mtu kuwa na tabia fulani lakini mara nyingi wanasema wataalam hawa kuwa msingi wa haya yote ni kipindi kile cha umri wa mwaka 0 hadi 6.

Tunapokuwa tunalelewa katika kipindi hicho tunafundishwa kuyapenda zaidi mambo hasi au mabaya kuliko yale chanya au mazuri, unaweza kushangaa au kuanza kukataa, lakini usijali maana nitakueleza kwa mifano pia.
Mfano:-
Hebu chukulia umerudi nyumbani jioni halafu ukafika nyumbani kwako ukakuta taarifa kwamba jirani yako, yaani mliepanga nae nyumba amepita kwenye uchochoro huko njiani alipokuwa anakwenda kwenye shughuli zake na kuokota fuko la hela limejaa kweli kweli....

Baada ya kupata taarifa hii, kwanza utauliza ni kiasi gani na baada ya kupewa jumla ya fedha utapata wivu na baada ya kuona tu huna la kufanya utaishia kumpongeza alieokota na kusema "una bahati sana wewe", hautafikiria kama na wewe unaweza kuja kuokota fuko lile la hela na hata mtu akikuambia kuwa na wewe uwe unapita vichochoroni unaweza kukutana na fuko la hela unaweza kumchika sana mana hauamini kama inaweza kukutokea maana unajua na unaamini ni vigumu.

Lakini wewe huyo huyo siku nyingine ukirudi na ukakutana na taarifa kuwa kuna mpangaji mwenzako mwimngine ambae alipita kwenye barabara fulani kisha akakutana na vibaka na kumkaba kisha wakampora kila kitu, utaingiwa na huruma na utampa pole, baada ya hayo utaingiwa na hofu sana...

Hofu hiyo haitasababishwa na kitu kingine chochote isipokuwa utaamini kabisa na wewe kuna uwezekano mkubwa sana wa kuja kukutana na tukio kama alilokutana nalo mpamgaji mwenzako huyo, kama kuna mtu akikuambia usipite barabara ile aliyopita jirani yako maana kuna uwezekano wa kukutana na vibaka na kuporwa utaona ni ushauri wa maana sana na utaamini kabisa hili linawezekana kukutokea wewe.

Ndivyo ilivyo,wakati tunakua tuliaminishwa hivyo kuwa yale mabaya ndio yanaweza kututokea sisi lakini mazuri hayawezi kututokea sisi hao hao, aina hii ya imani au fikra imejengeka kwentu tangu tukiwa watoto wadogo na tumerithishwa kutoka kwa wazazi wentu na jamii yetu hivyoi kuikwepa ni kama haiwezekani mpaka utakapokuja kujifunza utambuzi na kujua matatizo haya.

Tatizo hili la kimalezi linakuja kuzaa tatizo lingine kubwa sana ambalo ndio msingi wa makala hii na tatizo hilo ni la kuja kuishi maisha ya wengine huku sisi tukiyaacha maisha yetu.

Je ni kwa namna gani hili linatokea? Hebu soma kisa hiki cha kweli kabisa halafu utanuelewa tu......

Niliwahi kupanga nyumba moja kipindi fulani huko nyuma na dada mmoja hivi ambae alikuwa na rafiki yake mmoja ambae alikuwa ameolewa, hebu tuchukulie kuwa huyu dada niliekuwa nimepanga nae nyumba moja alikuwa anaitwa Anna na huyu aliekuwa ameolewa alikuwa anaitwa Rebeca....

Anna alikuwa ni rafiki mkubwa sana wa Rebeca na walikuwa wanashaurina mengi sana, Anna alikuwa hajaolewa kama rafiki yake, huyu rafiki wa Anna alikuwa anaishi kwenye ndoa ya mateso sana maana mumewe alikuwa ni mfujaji wa hela na mlevi lakini pia alikuwa ni mtu wa kubadilisha wanawake sana,Rebeca alikuwa akipata kipigo karibu kila siku kutoka kwa mumewe na kila kitu alikuwa anamsimulia rafiki yake Anna

Anna alikuwa ni kama mfariji wa Rebeca kwenye mateso ya ndoa yake ile,baada ya muda Rebeca alianza kuugua maradhi ya moyo na pia alianza kupata matatizo ya miguu na baadae alianza kulazwa mara kwa mara,rafiki yake alijitahidi sana kwenda kumsalimia kila alipopata muda na baada ya mwaka mmoja wa kuugua Rebeca alifariki dunia akimuacha mumewe na mtoto mmoja wa miaka 6

Baada ya msiba Anna aliendelea na maisha yake kama kawaida lakini alikuwa akisema hana hamu ya kuolewa kwasababu ya mateso aliyokuwa anayasikia na machache kuyashuhudia aliyokuwa anayapata rafiki yake ambae kwa wakati huo ni marehemu, lakini haikupita muda mrefu rafiki yake ya kiume Anna ambae pale nyumbani alikuwa mwenyeji na nilifahamiana nae pia maana alikuwa akija pale mara kwa mara aliamua kumuoa Anna. Anna alionesha kusita sana lakini baadae aliamua kukubali na ndoa ilifungwa na baadae Anna alihamia kwa mumewe.....

Maisha yalianza lakini baada ya miezi minne mumewe Anna aliachishwa kazi baada ya kampuni aliyokuwa anafanyia kazi kufilisika, alirudi nyumbani na kuanza harakati za kutafuta kazi nyingine, lakini huyu jamaa alianza kulalamika tabia ya mkewe kutomuamini haswa pale anapokuwa amechelewa kwenye harakati zake za kutafuta kazi maana kuna wakati alikuwa analazimika kwenda mbali kidogo na pale walipokuwa wanaishi kutafuta kazi.

Mumewe Anna alikuwa anasema mkewe alikuwa hampi hata hela ya nauli alipokuwa anataka kwenda kuhangaika kutafuta kazi na alikuwa anasema kuwa mkewe huyu alikuwa anasema kuwa akimpa hela atakwenda kuzinywea pombe na kuwahinga wanawake, huyu jamaa alishangaa sana maana hajawahi kunywa pombe na alikuwa anajiuliza sana kitu gani kinachomfabnya mkewe kufikiria hivyo,pia anasema hakuwa mtu wa wanawake pia na alikuwa akishangaa sana sababu ya mkewe kuhisi hivyo.

Aliendelea kumpuuza na kuhangaikia kutafuta kazi na wakati akiwa hajapata alikuwa akifanya vibarua vya hapa na pale ili kupata hela ya matumizi madogo madogo ambayo hakuwa akiipata kutoka kwa mkewe japokuwa alikuwa akifanya kazi iliyokuwa inamuingizia kipato kikubwa sana tu.

Kuna wakati ulikuwa unaibuka ugomvi miubwa sana kati ya Anna na mumewe kwasababu Anna alikuwa kimtuhumu jumewe kuchelew maksudi kwasababu alikuwa akitumia muda na vijihela vya vibarua kuhonga wanawake ma kunywa pombe.jamaa alikuwa anakasirika na ulikuwa ukiibuka ugimvi mkubwa sana mara kwa mara, taratibu ndoa yao ikaanza kupata ufa mkubwa sana na ikafikia wakati kukawa na mikwaruzano kila siku huku Anna akimlaumu mumewe kwa kuwa na wanawake wengi.

Mumewe huyu alikuwa anafahamiana na kijana mmoja ambae alikuwa mara nyinbgi wakienda wote kutafuta kazi maana kijana yule alikuwa amemaliza masomo yake ya elimu ya juu, kijana huyu alikuwa anashangaa sana sababu ya mkewe huyu jamaa kumtuhumu mumewe kuwa na wanawake kwasababu hajawahi kusikia huyu jamaa [mumewe Anna] kuzungumzia wanawake wengine achilia mbali kuwa nao.

Ndoa ya Anna ilifikia tamati baada ya miaka miwili tu ya ndoa hiyo na waligawana kila kitu huku Anna akiwa anaondoka kwenye ndoa hiyo akiwa na mtoto mdogo........


Ukitazama kwa juu juu huwezi kuona kiini cha tatizo la ndoa ya Anna, lakini hapo utaona kuwa Anna alikuja kuyaishi maisha ya marehemu rafiki yake, hapa badala ya kuyachukulia maisha ya rafiki yake kama shule yeye aliyachukulia kuwa yake.

Kuna tofauti kubwa sana kati ya kuyachukulia matukio yanayotokea maishani mwetu kama shule na kuyachukulia yetu, mtu anaevuka barabara kwa mfano, huku akijiona kama mtu ambae atagongwa na gari, huyo ana uwezekano mkubwa sana kugongwa na gari kwasababu atababaika kila akivuka barabara na kupoteza umakini kitu kitakachomfanya agongwe kirahisi sana.

Lakini mtu anaevuka barabara hukua akijua kuna kugongwa na kulichukulia hilo kama suala la kumfanya ajue kuwa akiwa makini hawezi kugongwa na kuchukulia matukio ya watu kugongwa na magari kama shule kwake huyu atakuwa na utulivu wa hali ya juu na utulivu huo utamsababishia umakini mkubwa na kumfanya asibabaike na kufanya uwezekano wa kugongwa na gari kuwa mdogo sana au kutokuwepo kabisa.

Anna aliona maisha ya Rebeca ni maisha yake pia na akayachukua kama yalivyo kwenda kuyaishi kwa mumewe ambae masikini ya Mungu wala hakuwa na tabia kama za shemeji yake Anna [mume wa Rebeca] Anna alimuona mumewe kama ni mume wa Rebeca na akawa na hamaki na kuhisi mabaya kila wakati kumhusu.

Matatizo haya leo na sisi tunayo,chochote ambacho kinaweza kumtokea mtu fulani na kikawa ni kibaya basi tunakibeba na kukifanya chetu na matokeo yake tunaishi maisha ya wengine huku yetu tukiyaacha kabisa.

Tunapokuwa tunatafuta kazi tunakuwa tunatafuta huku tayari tukiwa tumekosa kazi hizo kwasababu fulani alishatafuta akakosa.

Tunapokuwa tunatafuta wachumba tunatafuta wachumba wa aina fulani au wenye sifa fulani kwasababu kuna hiki na kile kilishawatokea akina fulani, hatutafuti wachumba ambao sisi tunawataka isipokuwa tunatafuta wachumba wanaotofautiana na wachumba wa akina fulani maana tumeyabeba maisha yao na kuyafanya yetu.

Tunapokuwa tunasoma ni hivyo hivyo, yaani sisi hatupo kabisa, tumefundishwa kuyapenda mambo hasi na yakiwatokea mambo hasi wenzetu basi tunaamua kuyabeba na kuyafanya yetu, lakini yale mazuri hatuyachukui na tunaamini sio yetu kabisa.....

Malezi yetu yanatuumiza sana, tunaishi kwa matukio, hatumuamini Mungu tena na tunaona fulani kafilisika tunaona na sisi tuko njiani kufilisika, tunaona fulani kaachika kwenye ndoa kwasababu za mateso na sisi tunaona tuko njiani kuachwa na tunaanza kujilinbda na kuwa na tabia za ajabu ajabu.....

Ifikie wakati tujifiunze kuwa sisi ili tufanye maisha yetu kuwa mazuri na yenye furaha....

Habari hii nimetumiwa na Peter Shirima [King] 0786256380. Baada ya kuisoma kwa makini nikaona si vibaya  nikiiweka hapa Maisha na Mafanikio  ili wote tupate elimu hii. AHSANTE PETER!!.

Saturday, November 7, 2015

NAWATAKIENI KILA LA KHERI KWA KILA MTAKACHOKIFANYA....KWA UJUMBE/USEMIHUU!!!

Changamoto  kubwa katika maisha  ni kujigundua wewe ni nani/nini........
Na kikubwa zaidi pia cha pili ni kuwa na furaha kwa ulichokipata/gundua........

Wednesday, November 4, 2015

HAPA NI VITABU VYANGU NILIVYONUNUA HIVI KARIBUNI. ..BOOKSHOP YA PERAMIHO

Hakuna kitu kizuri kama kununua vitabu. Hivi ni vitabu vyangu kilivyonunua hivi karibuni....

Sunday, November 1, 2015

JUMAPILI NJEMA KWA WOTE JUMAPILI HII YA KWANZA YA MWEZI WA KUMI NA MOJA....NA WIMBO HUU:- AMANI YA TANZANIA NI NGUZO IMARA......


Namshukuru Mungu tangu uchaguzi umeanza mpaka leo kumekuwa na AMANI na nazidi kumwomba Mwenyezi Mungu amani na utulivu vizidi kuendelea. Pia namshukuru Mungu kwa kutulinda na kutuepusha na magonjwa makubwa. Sisi sote ni ndugu na watoto wa baba mmoja kwa hiyo tupendane na tukumbukane.....Kapulya!

Friday, October 30, 2015

KWA VILE LEO NI IJUMAA NA PIA NI MWISHO WA JUMA PIA IJIMAA YA MWISHO YA MWEZI HUU WA KUMI BASI SI VIBAYA TUKIMALIZA KWA MTINDO HUU.....

 Akina mama wanachunja pombe ya kienyeji kama sio komoni basi ni myakaya tayari kwa kunywewa
Na hapa mzee kesha pata nusu yake .Nusu ni hicho kikombe anachonywea. Amewahi  maana yupo peke yake hapo ila muda si mwingi wengi watajitokeza. Ila tukumbuke pombe si maji kwa hiyo tuwe makini.....MWISHO WA JUMA UWE MWEMA KWENNU NDUGU ZANGU:-)

Thursday, October 29, 2015

TUNAKARIBIA KUUMALIZA MWEZIHUU WA KUMI...BASI TUUMALIZE KWA USEMI HUU....KARIBU

Mlinde kama binti yako, mpende kama mke wako na muheshimu kama mama yako........Kapulya wenu!

Monday, October 26, 2015

Friday, October 23, 2015

Wednesday, October 21, 2015

CHAKULA AKIPENDACHO KAPULYA....MAKANDE

Ni chakula am,bacho ukila unashiba na muda mrefu huhitaji kula chakula kwa muda mrefu..leo nimekitamani mno ......nawatakieni wote siku njema...tulage kwa macho haya makande.

Sunday, October 18, 2015

NAPENDA KUWATAKIENI WOTE JUMAPILI NJEMA NA JIONI NJEMA!!!!

Amani upendo na furaha itawala katika nyumba zetu. JUMAPILI NJEMA SANA PIA JIONI NJEMA...KAPULYA!!!!

Thursday, October 15, 2015

HASIRA HASARA PIA NI MBAYA KWA AFYA ZETU!!!

Sisi sote hukasirika mara kwa mara. Hasira ni sehemu ya hisia zetu kama vile ilivyo upendo, tumaini, wasiwasi, huzuni na woga. Hasira ilivyodhibitiwa inaweza kuonyeshwa kwa njia inayofaa na inaweza kuwa na faida. Kwa mfano, hasira inaweza kuwa na faida ikiwa itamfanya mtu aazimie kushinda vizuizi au matatizo fulani.

Kwa kawaida, mtu huudhika anapotendewa isivyo haki. Kutukanwa, au kukosewa heshima kunaweza pia kumuudhi mtu. Pia, mtu anaweza kuwa na hasira anapoona jambo fulani kuwa tishio kwa mamlaka au sifa yake.

Bila shaka, watu hukasirika na mambo tofauti ikitegemea umri, jinsia, na hata utamaduni wao. Isitoshe, watu hutenda kwa njia tofauti tofauti wanapopandwa na hasira. Watu fulani hawakasiriki upesi, nao husahau haraka wanapokosewa, lakini wengine hukasirika kwa haraka na huenda wakaendelea kuwa na hasira kwa siku nyingi, majuma , miezi au hata miaka.

Binadamu tumezungukwa na mambo yanayoweza kuchochea hasira. Zaidi ya hilo, siku hizi watu wanachokozeka kwa urahisi zaidi, Kwa nini imekuwa hivi? Sababu moja ni kwamba kuna mtazamo wa ubinafsi  yaani umimi ambao umeenea mno.

Kwa kweli, watu wenye ubinafsi wasipopata kile wakitakacho, mara nyingi wao hukasirika. Kuna sababu nyingi kwa nini mwelekeo wa watu kulipuka kwa hasira unaongezeka, ambazo wewe msomaji na mimi twaweza kusaidiana kuzifikiria...

Na kama tunavyoelewa hasira imekuwa ni adui kwa watu wengi sana kwasababu imekwisha leta madhara makubwa sana kwa wengi
Binadamu anadaiwa kuwa ni kiumbe ambaye anakabiliwa na tishio la kuangamia kwa hasira kwasababu ya maendeleo anayoyafikia
Hivi ni kweli  kwamba kadiri maendeleo yanavyoongezeka ndivyo uwezekano wa binadamu kuwa na hasira unaongezeka pia?.Kama ni kweli ipo hivi,  kwa binadamu  ni kitisho kwa usalama wake mwenyewe
Kuna haja ya kuwa na elimu na semina kwa wingi ili kuweza kumuokoa binadamu na kitisho cha hasira

Saturday, October 10, 2015

Wednesday, October 7, 2015

SHUJAA WETU HAKUSALITI JAMAA ZAKE NA UTAWALA WAKE.....!!!!!


Nduna Songea Mbano, muda mfupi kabla ya kuuawa
Nduna Songea: Shujaa wa Wangoni aliyewapeleka puta wajerumani..SHUJAA WETU HAKUSALITI JAMAA ZAKE NA UTAWALAWAKE..!!. HUWEZI kuielezea na kuikamilisha historia ya vita ya Majimaji na ukombozi wa nchi yetu
bila kumtaja shujaa wa kabila la Wangoni, Nduna Songea Mbano ambaye jina lake lilipewa hadhi ya kuuita mji wa Songea kutoka kwenye jina la Ndonde mwaka 1906.
Kiongozi huyo alikuwa ni miongoni mwa wasaidizi ( Nduna) 12 wa Chifu wa kabila la wangoni (Nkosi) chifu Mputa bin Gwezerapasi Gama. Wasaidizi wake wengine walikuwa ni Mgendera Mawaso Gama, Kohongo Magagura, Mputa Mkuzo Gama, Magodi Mbamba Mbano, Mtekateka Muyamuya Tawete, Fratela Fusi Gama. Manduna wengine ni Maji ya Kuhanga Komba, Zimanimoto Gama, Mpambalyoto Soko Msalawani, Mtepa Hawaya Gama na Nduna Mkomanile ambaye alikuwa ni mwanamke pekee kuwa nduna.
Nduna Songea Mbano alikuwa maarufu kuliko manduna wenzake na hata chifu Mputa Gama alikuwa anamtegemea sana katika kuwaongoza manduna na wapiganaji
wa vita ya Majimaji kiujumla.  Mhifadhi kiongozi wa Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Songea, Philipo Maligissu
akizungumzia maisha ya Nduna Songea Mbano katika viwanja vya Makumbusho hayo, anasema kuwa Nduna Songea Mbano weledi ndio uliompa umaarufu sana.
Kutokana na weledi na ushadi wake, aliwazidi wenzake 11 katika mbinu za kuandaa mikakati ya kivita, kutoa uamuzi mzito pasi na kutetereka na kusimamia utekelezaji wake kikamilifu.
Kwa umakini mkubwa, Nduna Songea Mbano aliweza kufanya kile alichokuwa akikiamini na uthibitisho wa jambo hilo ulianza kujitokeza Julai 12, 1897 katika viwanja vya Bomani kwa mkuu wa Wilaya wa Wajerumani, Luteni Engelhardt.
Maligissu anasema rekodi zilizopo zinaonesha kuwa tarehe hiyo Nduna Songea Mbano, alionekana kuwa ni mtu wa kipekee katika idadi ya manduna 11 ambao walikuwa wasaidizi
wa Chifu Mputa Gama kwa kitendo chake cha kubisha wazi wazi tamko la utawala mpya wa Wajerumani la kutaka Wangoni wakomeshe biashara ya utumwa.
Siku hiyo ilikuwa ni rasmi ambayo utawala wa kikoloni ulikuwa unaanzishwa katika mji wa Songea, wakati huo ukiitwa Ndonde na Mkoa wa Ruvuma kiujumla ukiwa chini ya Luteni
Engelhardt aliyekuwa Mkuu wa Jeshi Kanda ya Kusini.
Wajerumani walipofika kuanzisha makoloni yao katika maeneo ya ukanda wa kusini walikutana na msuguano mkubwa kutoka kwa tawala za Kiafrika, hasa tawala za Wangoni.
Maligissu anasema kuwa Wangoni walikuwa na tabia ya kwenda mikoa ya Lindi na Mtwara
kuvamia, kuchukua mateka na kuwapeleka Songea kuwafanyisha shughuli mbalimbali katika maeneo yao ya utawala wao.
Tabia hiyo ya Wangoni iliwachukiza sana Wajerumani, kwani walikuwa wanaheshimu sana makubaliano yaliyofikiwa kutoka kwenye mkutano wa Berlin wa 1884 /85.
Katika mkutano huo moja ya makubaliano ni na kila nchi yenye koloni barani Afrika ikomeshe biashara ya utumwa, hasa ikizingatiwa kwamba Wajerumani walikuwa wamejiimarisha sana.
Hivyo walipofika Ruvuma wakatoa tamko kwa Wangoni kuwa hairuhusiwi na haitaruhusiwa tena kwenda Lindi, Mtwara au kokote kuchukua mateka na kwamba mateka wote waliochukuliwa na Wangoni waachiwe huru.
Baada ya Wajerumani kutoa tamko hilo, ndipo Nduna Songea Mbano alipojitokeza waziwazi
na kusimama kujibu hoja iliyotolewa na Wajerumani kuhusu tamko hilo.
Nduna Songea Mbano alisema kuwa utawala wa kabila la Wangoni hauwezi kutekeleza tamko hilo na kwamba msimamo wao ni kutoutambua utawala mpya wa Kijerumani na tamko lao.
Kwamba ujio wa Wajerumani na tamko lao kwa Wangoni vililenga kudhoofisha utawala wa machifu na manduna katika maeneo yao kwa kufuata kanuni zao za kimila na kitamaduni.
Kuanzia hapo Wajerumani walimwona Nduna Songea Mbano kuwa ni mtu hatari sana katika utawala wao mpya, hivyo kumweka alama maalumu na kuanza kumfuatilia nyendo zake.
Alionekana kuwa kiongozi shupavu mwenye misimamo mikali na anayezingatia heshima na utu wa kabila lake bila kuyumbishwa. Alionekana kuwa pekee mwenye uwezo mkubwa wa kufanya kazi katika mazingira yoyote kwa kushirikiana na wananchi wake ambao walikuwa
wanamheshimu sana na kumsikiliza.
Maligissu anaeleza kuwa Nduna Songea Mbano alikuwa na uwezo mkubwa wa kuwaunganisha
wananchi wake na kuwa na umoja, upendo na mshikamano na kwamba alikuwa akiwaelekeza jambo wanalifanya kwa umakini na kwa ukamilifu.
Nduna Songea Mbano aliendelea kujizolea umaarufu mkubwa na baada ya kutamka kuwa yupo tayari kwa lolote lile na hawezi kukubali kuona tawala za Kiafrika zinadharauliwa na wakoloni kwa namna yeyote ile.
Wajerumani wakaamua kuwaalika machifu na manduna wote Julai 13, 1897 Bomani kwa mkuu wa wilaya na kuwaambia kuwa mtu yeyote katika eneo lake atakayekaidi amri yoyote kutoka kwa uongozi mpya wa Wajerumani atapigwa risasi, kunyongwa hadi kufa au kufungwa maisha. Siku hiyo hiyo machifu na manduna walichukuliwa hadi juu ya mlima wa shabaha wa Chandamari, katikati ya mji wa Songea na kuoneshwa nguvu ya risasi inavyoweza kufanya kazi katika mwili wa binadamu na kwamba silaha za kijadi na kimila za Wangoni hazingeweza kufua dafu mbele ya silaha hizo.
Licha ya Wajerumani kutoa vitisho vingi, Nduna Songea aliendelea na msimamo wake wa awali wa kuchukia na kuupinga utawala wa Wajerumani na kuutetea utawala wa Kiafrika mpaka ilipokuja kutokea Vita ya Majimaji. Nduna Songea alitoa ushindani mkubwa sana katika vita hivyo na kuonesha ustadi mkubwa kwenye mapigano na katika sehemu zote ambazo Wajerumani walipigana, wameandika kuwa hawakupata ushindi mkubwa kama waliopata katika mkoa wa Ruvuma, zamani nchi ya Ungoni.
Viongozi wao hawakuwa wanafiki, kwani walijitoa kikwelikweli kusaka ukombozi na hadhi ya tamaduni zao mpaka dakika ya mwisho. Ndio maana idadi kubwa ya watu walionyongwa katika historia ya Tanzania walitoka katika himaya ya Nduna Songea Mbano na ushahidi upo wazi kuwa watu 67 walihukumiwa kunyongwa hadi kufa, akiwamo Nduna Songea Mbano.
Katika kuonesha kuwa Nduna Songea alikuwa na uwezo wa kufanya mambo kwa weledi mkubwa bila kusaliti dhamira yake kuanzia mwaka 1897 aliandaa jeshi lake la kupambana na utawala wa Wajerumani.
Akaanza kuchukua watu wake na kuwapeleka juu ya mlima wa Chandamari kufanya nao mkutano, kutoa mafunzo ya kivita na kuwaelekeza kwa nini Wajerumani wachukiwe.
Katika mlima huo ndipo alipoeleza kwa kina madhara ya kuukubali utawala wa Wajerumani
na kutoa ahadi kwa wananchi wake ya kuwaondoa Wajerumani kwa lazima na kuwa eneo hilo ni la Wangoni, wamekuwa wakiishi siku zote chini ya utawala wao, hivyo haiwezekani wapelekewe utawala mpya wakati hawauhitaji.
Chokochoko hizo zilizaa vita vya Majimaji na wakati mapigano yakiendelea Wajerumani walianza kumtafuta Nduna Songea ili wamkamate na kufanya naye mazungumzo ya maridhiano.  Kumbe Songea Mbano alikuwa amejificha kwenye pango kubwa lililopo kwenye mlima wa Chandamari na usiku alikuwa akikutana na askari wake nje ya pango hilo na kuwapa mafunzo zaidi ya kivita.  Maligissu anaeleza kuwa Nduna Songea alikuwa anaishi na ndugu zake katika eneo la Mateka, leo hii manispaa ya Songea na wakati wa vita ndipo Songea Mbano alikuwa anajificha katika pango hilo ili wasimkamate mpaka atakapotimiza malengo yake.  Wajerumani walipoona wanaendelea kupata madhara makubwa kutokana na vita hivyo, waliamua kuwakamata ndugu na familia yake, Chifu Mputa Gama na manduna wengine na kuwafunga gerezani kwa lengo la kumdhoofisha Nduna Songea.
Baada ya Wajerumani kumdhoofisha Nduna Songea alipata taarifa zote na akaamua kutoka
kwenye pango hilo na kwenda kwa Wajerumani na kutaka watu wake waachiwe ili mapigano yaendelee.  Ndipo naye alipokamatwa na kuswekwa gerezani na Wajerumani wakawahukumu wafungwa hao kunyogwa hadi kufa.  Wafungwa hao waliamriwa kuchimba shimo kubwa bila kujua ndilo lingekuwa kaburi lao na ilipofika siku ya kifo chao, walinyongwa kwa zamu kwa muda wa siku mbili na maiti zao kuwekwa kwenye kaburi hilo hadi walipofikia 66 ndipo walizikwa kwa pamoja.  Walimwacha Nduna Songea Mbano ili awasaidia kutimiza malengo yao kwa wananchi, kwani waliamini akiwa kiongozi jasiri na anayependwa na watu wake angesikilizwa vizuri. Tangu siku hiyo walipomwacha bila kumnyonga, Nduna Songea aliwasumbua Wajerumani na kutaka naye anyongwe kama ndugu zake, kwani hakuona sababu ya yeye kuishi wakati ndugu zake alishauawa; akasema wasipomnyonga angegoma kula na kunywa chochote mpaka afariki dunia. Ndipo Wajerumani walipoamua kumnyonga na kumzika katika kaburi la peke yake, wakiamini kuwa ni mtu wa pekee mwenye ushujaa, uamuzi mzito na msimamo usioyumba. Walimuenzi kwa kubadilisha jina la mji wa Ndonde na kuubatiza jina la Songea, ambapo mpaka sasa linatumika kuuita mji huo wenye hazina kubwa ya historia na utalii wa kitamaduni.
KATIKA PITAPITA MTANDAONI NIMEKUTANA NA HII MADA YA KIHISTORIA YA WANGONI  NIKAONA SI MBAYA KAMA NIKIWEKA HAPA MAISHA NA MAFANIKIO UKIZINGATIA ASILI YANGU NI MNGONI....PANAPO MAJALIWA TUTAONANA TENA......NA CHILAWU MEWAWA/NA KESHO HIVYOHIVYO
 

Tuesday, October 6, 2015

UNAPOLIMA MASHAMBA NI LAZIMA KUYATYNZA/KUANGALIA

Hapa mdada anakagua baadhi ya mashamba na hapa ni shamba/bustani ya matunda hasa ni ndizi ndizo zinaonekana lakini kuna mananasi, mapera, maparachichi, machungwa, malimao nk.

Thursday, October 1, 2015

TUANZA MWEZI HUU WA KUMI NA PICHA HII....IWE PICHA YA MWEZI.....

Nimeipenda hii picha...inaonyesha upendo wa wazazi kwa watoto wao na pia pia jinsi ya kusaidiana kazi. Inapendeza kwa kweli....Au wewe msomaji unasemaje?...KILA LA KHERI!!

Tuesday, September 29, 2015

SALAMU ZA MAKABILA YETU TANZANIA

 


Wasomaji wapendwa wa blog ya MAISHA NA MAFANIKIO, nimejaribu kufanya utafiti wa lugha za makabila yetu hapa nchini Tanzania. Kama tujuavyo ni kwamba kuna makabila zaidi ya 120 hapa nchini. Nami nimeamua kuangalia zaidi salaam, hasa za asubuhi, kutokana na utafiti wangu pia kwa msaada wa marafiki nimepitia makabila kadhaa na kukutana na maneno yanayotumika katika salaam za asubuhi ambayo yanafanana kidogo, hebu tuone maneno hayo ni yapi:

KINGONI: Uyimwiki = Habari za asubuhi
KIZIGUA: Kugona vihi = Habari za asubuhi
KINYAKYUSA: Ughonile = Habari za asubuhi
KIYAO: kwimukaga = Habari za asubuhi
KIPARE: Murevuka = Habari za asubuhi
KIUNGUJA: wambaje = Habari za asubuhi
KISAMBAA: Onga makeo = Habari za asubuhi
KIANGAZA: Mwalamtse = Habari za asubuhi
KINYAMWEZI: Mwangaluka = Habari za asubuhi
KICHAGA: Shimbonyi = Habari za asubuhi
KIMERU: Konumbware = Habari za asubuhi
KIMASAI: Sopai = Habari za asubuhi
KISUKUMA: Mwadila = Habari za asubuhi
KIHEHE: Kamwene = Habari za asubuhi
KIBENA: Kamwene = Habari za asubuhi
KIKINGA: Ulamwihe = Habari za asubuhi
KINYIRAMBA: Ulalaliani = Habari za asubuhi
KIHAYA: Wabonaki = Habari za asubuhi
KIMATENGO: Ja kujumuka = Habari za asubuhi
KIKURYA:  Agha nyinkyo = Habari za asubuhi
KIPOGORO: Za mandawila = Habari za asubuhi
Hayo ni baadhi tu ya makabila machache katika mengi yaliyomo nchini kwetu, unaweza ongezea salaam za makabila unayofaham wewe ndugu yangu

Friday, September 25, 2015

TUMALIZE JUMA HILI KWA USEMI HUU.....!!!

Kila kitu/mtu kina/ana uzuri wake, lakini sio wote wanaouona usuri huo!
BASI NGOJA MIMI /KAPULYA WENU NIWATAKIENI IJUMAA NJEMA NA MWISHO MWEMA WA JUMA HILI.

Wednesday, September 23, 2015

HEBU LEO TUANGALIE KICHEKESHO HIKI CHA MZARAMO V/S MCHAGA...KARIBU

Mzaramo alitangaza anatibu magonjwa yooooooote kwa tsh. 100,000/=
Na kama akishindwa kukutibu anakurudishia laki
yako nakukuongeza laki nyingine.
MCHAGA akaona hii fursa yakujipatia hela aiwezi mpita akaenda kutibiwa.
MZARAMO: "unaumwa nini?"
MCHAGA: "Sisikii ladha ya aina yoyote mdomoni kabisaaaa.."
MZARAMO: "sawa, toa laki kabisa.."
Mchaga akatoa.
MZARAMO akamuagiza msaidizi wake; "Naomba kikopo no.27 mpe anywe huyu.."
MCHAGA akanywa akatema faster; "Puh puu puu, Aisee huu si mkojo huu..?"
MZARAMO: "Umepona karibu tena.."
Mchaga aka-mind sana Kesho yake akarudi tena hakuamini ameliwa pesa yake.
MCHAGA: aisee nina tatizo la kumbukumbu nasahau
sanaaaaa.."
MZARAMO akamwambia "hakuna tabu, toa laki tukupe tiba..'
MCHAGA akatoa pesa akijua leo lazima afanikiwe..'
MZARAMO: "nesi naomba kikopo no.27.."
MCHAGA: "ASA CHALII ANGU HICHO SI CHA JANA CHA MKOJO HICHO AISEE..?"
MZARAMO: "UMEPONA KUMBUKUMBU UNAYO.
PANAPO MAJARIWA TUTAONANA TENA!

Monday, September 21, 2015

NIMEONA KUWA NA KIPENGELE KIPYA NACHO NI UTAMADUNI WA MTANZANIA/AFRIKA NA NIMEONA IWE JUMATATU NA KWA KUANZA NIMEONA TUANZA NA KUSIKILIZA NGOMA HII YA KUNYAKYUSA....KUTOKA MBEYA


Kama tunavyotambua Tanzania ni nchi yenye makabila mengi ni 121 kama sijakosea. Kwa hiyo kila kabila lina utamaduni na mila zake kuanzia kwenye chakula  hadi ngoma. Kwa hiyo leo nimeona tuwatembelee ndugu zetu Wanyakyusa na ngoma hii ya kuvutia.
TUONANE TENA JUMATATU IJAYO NA KABILA JINGINE!

Friday, September 18, 2015

KARIBUNI TUJUMUIKE CHAKULA CHA MCHANA HUU. .....

Ni wali, kebichi su wengine wanasema kabichi  na maharage tena ya kutoka Mbinga. Karibuni sana ndugu  zanguni. Na pia nichukue nafasi kuwatakieni mwisho mwema wa juma.

Monday, September 14, 2015

VYAKULA VYETU VYA ASILI-----

Ulijua ya kwamba chakula kinachopikwa kwenye chungu ni kitamu sana kuliko kupika kwenye sufuria? Basi ngoja niwatakieni JUMATATU NJEMA NA PANAPO MAJALIWA TUTAONANA TENA!

Friday, September 11, 2015

TUMALIZE WIKI KWA USEMI HUU...

Kuna njia moja tu ya kuwa na furaha, nayo ni kuwaacha kuwa na wasiwasi juu ya jambo ambalo halipo juu ya uwezo wetu.
Panapo majaliwa tutaonana tena...wenu Kapulya

Wednesday, September 9, 2015

TASWIRA YA MLIMA KILIMANJARO

Mlima wetu Kilimanjaro

Labda tu tusikilize hapa ni vipi kupanda mlima Kilimanjaro

Tutaonana tena tupo pamoja!

Tuesday, September 8, 2015

PICHA YA WIKI:- KUWA MAKINI UNAPOFUNGUA GARI YAKO !!

Hapa kazi ipo fikiria huyo nyoka yupo pia ndani ya gari, au kwenye kiatu na pia hata chooni, Ndugu zangu tuwe makini  tusikurupuke tu tuchunguze kwanza....Hata kitandani uendapo kulala chunguza kwanza......Niwatakie kila la khri na panapo majaliwa tutaonana tena...Kapulya:-(

Sunday, September 6, 2015

NNAPENDA KUWATAKIENI WOTE JUMAPILI HII YA KWANZA YA MWEZI HUU WA TISA (9) KWA USEMI HUU

Ukisha muamini Mungu basi yatosha, ya walimwengu waachie wenyewe!!
BARAKA NA UPENDO WA BABA MUNGU MWENYEZI VWEE MIOYONI MWETU KILA WAKATI.

Friday, September 4, 2015

MATUNDA NI MUHIMU KWA AFYA ZETU!!

Nimeyatamani kweli machungwa...Niwaambie kitu nilipokuwa mwanafunzi wa darasa la kwanza na pili. Shuleni kwetu Lundo kulikuwa na miti mingi sana ya matunda mbalimbali mojawapo machungwa...Basi nakuambieni baada ya shule unaaga nyumbani kwenda kuchota maji au kuokota kuni kumbe kula machungwa ya shule...shhhh.:-(.....Ila mmhhh ilikuwa ukikamatwa na mlinzi basi ni viboko tu ...Kaaazi kwelikweli:-) PAMOJA DAIIMA NA MWANZO MWEMA WA MWISHO WA JUMA. PANAPO MAJALIWA TUTAONANA TENA. Kapulya.

Thursday, September 3, 2015

SWALI NILILOULIZWA NA MSOMAJI /MFUATILIAJI WA MAISHA NA MAFANIKIO:-

Swali lenyewe lipo hivi:- Hivi ni  kitu gani akina mama/wanawake kinawafanya wampende mtoto fulani zaidi kati ya watoto wao wa kawazaa?
Akaendelea:- Utamkuta mama ana watoto wanne, lakini anampenda mmoja zaidi ya wengine? Hii inakuwaje kwa upande wako? akanipa hili swali mimi......akaendelea nakuuliza kwa kuwa nadhani una watoto.....halafu akaendelea kusema ....Pia nadhani utakuwa umeshawahi kuisikia hii au inatokea.
Jibu langu lilikuwa kama ifuatavyo:- Binafsi kama mama nawapenda wanangu sawasawa na sijawahi kufikiria  KUWAPENDA  TOFAUTI.
Baadaye nikakumbuka kwanini niwashirikishe ninyi wasomaji/ ndugu zangu. Maana naamini palipo na wengi pana mengi
Hata hivo nami nikajiwa na swali:- Je?  Hiki kitu kipo? na kama kipo kwa akina mama/wanawake tu?  na sio akina baba/wanaume? Maana nao pia ni wazazi. NAOMBA TUJADILI KWA PAMOJA......Kapulya wenu!

Wednesday, September 2, 2015

UJUMBE WA WIKI HII KUTOKA KWA KAPULYA!

Msione nipo kimya nipo sema tu mambo ya afya hayapo sawa sanma na majukumu ni mengi basi kila kitu kimejichanganya...Ila tupo Pamoja.....Kapulya.

Monday, August 31, 2015

NIMEKUMBUKA NILIPOKUWA DARASA LA KWANZA NA PILI TULIKUWA TUKIIMBA SANA NYIMBO MOJAWAPO NI HII:- KWAHERI BABA NA MAMA!!!

1. Kwaheri baba na mama twaenda shuleni x2
Kusoma huko shuleni pamoja na mwalimu.
Kuandika huko shuleni pamoja na mwalimu.
 
2. Kwaheri baba na mama twaenda shuleni x2
Kuhesabu huko shuleni pamoja na mwalimu.
Kuchora huko shuleni pamoja na mwalimu.
 
3. Kwaheri baba na mama twaenda shuleni x2
Kuimba huko shuleni pamoja na mwalimu.
Twaimba sote pamoja pamoja na mwalimu.
JE? NA WEWE NDUGU YANGU KUNA WIMBO UNAUKUMBUKA AMBAO ULÖIKUWA UKIIMBA KILA SIKU?....Kapulya:-) Panapo majaliwa tuonane mwezi ujao!!
 

Sunday, August 30, 2015

BLOGG TA MAISHA NA MAFANIKIO IMEONA IMALIZE JUMAPILI HII YA MWISHO WA MWEZI KWA WIMBO HUU AHSANTE MUNGU!!


Nawatakieni wote jumapili njema sana na upendo pia baraka za Mungu zitawale ndani ya nyumba zetu pia mioyo yetu....Kapulya wenu!!

Thursday, August 27, 2015

JINSI MALEZI YETU YA UTOTONI YANAVYOWEZA KUATHIRI NDOA ZETU

Habari za leo ndugu zanguni leo nimeamka nikiwa na fikra nyingi sana juu ya jambo hili la malezi yetu ya utotoni yanvyoweza kuathiri ndoa...Naanza na mfano huu:-  Patrick na Maria  ni mke na mume, kila mmoja amelelewa malezi tofauti.
Patrick alisema  tangu nakua au napata akili, nilizoea kumuona baba akirudi nyumbani muda wowote anaotaka na sijawahi kusikia ugomvi wowote toka kwa mama kuhusu kuchelewa huko.
Kwenye akili yangu, nikaamini kwamba, kumbe mwanamme anaweza kurudi muda wowote nyumbani hata kama ni usiku wa manane. Pia niliwahi kumsikia mzee mmoja akimwambia mzee mwenzake ambaye alikuwa anaomba amruhusu aondoke ili awahi nyumbani.... alimwambia hivi.... wewe ni mwanamme bwana, unawahi nyumbani kufanya nini? Au unaenda kupika? Maneno haya yalimuumiza sana mzee yule na mwisho aliamua kubaki wakaendelea kunywa pombe yao taratibu huku akimshukuru kwa ushauri wake mzuri.
Maneno haya yakazidi kumfanya Patrick aamini kwamba kumbe mwanamme hapaswi kurudi mapema nyumbani, alianza kuwaza na kujisemea kimoyomoyo,  na mimi  nikioa nitakuwa nafanya hivyohivyo kwani huo ndio uanaume.
Kwa upande wa pili, Maria  mke wangu kakulia kwenye familia ya mzee Mapunda ambayo baba alikuwa anarudi mapema sana nyumbani, na binti Maria  akaamini kwamba kumbe mwanamme anapaswa awahi kurudi nyumbani. Hajawahi kusikia ugomvi wowote kutoka kwa baba na mama yake.
Watu hawa wawili ambao wamekulia malezi tofauti wakaoana, wakawa mke na mume.
Siku za mwanzo bwana Patrick  alikuwa anawahi kurudi nyumbani kama ilivyo ada ya mapenzi mapya. Ndoa ilikuwa na furaha kubwa sana
Baada ya miezi miwili kupita, mume akaanza kuchelewa kurudi nyumbani kitendohiki  kilimuumiza sana bi Maria , akahisi mume wake kapata mchepuko ( mwanamke wa nje), ugomvi ukachukua mkondo wake, bi Maria akaanza kumnyima unyumba mume wake, akatumia tendo kama silaha ya kumwathibu mumewe, furaha iliyokuwepo kwenye ndoa hii ikayeyuka ghafla, paradiso iliyokuwepo ndani ya ndoa hii ikageuka na kuwa jehanamu, ikabaki historia, ikawa asubuhi ikawa jioni, maisha yakaendelea.
Mume akazidisha kuchelewa, hamu ya mapenzi ikampanda, akaamua kutafuta mwanamke wa pembeni ili apozee hamu zake.
Siku moja wanandoa hawa wakaamua kwenda kupata ushauri kwa mtaalamu wa masuala ya ndoa. Baada ya kuwasikiliza akawaeleza kwa kina namna jinsi malezi yao utotoni yalivyopelekea kuharibu ndoa yao. Akawapa mtihani wachague, wafuate malezi ya mke au mume? Kwa kuwa mume alikuwa akimpenda sana mkewe akashauri wafuate malezi ya mke ya yeye kuwahi nyumbani mapema.
Huwezi amini sasa hivi ndoa ya bi Maria na bwana Patrick ina amani na furaha maradufu ukilinganisha na wakati wanaoana.
Hebu na wewe jiulize kwenye ndoa yako, kwa nini huelewani na mwenzi wako?