Sunday, December 6, 2015

HII NI JUMAPILI YA PILI YA MAJILIO:- NA LEO TUANGALIE MAANA YA MAJILIO KATIKA MAISHA YA BINADAMU

JUMAPILI YA PILI(2) YA MAJILIO
Sisi binadamu hatuwezi kuishi daima katika hali ileile bila ya matazamio. Hasa kijana anatarajia mambo mapya tena mema. Hivyo tunajitahidi kuyapata. Asiyetazamia chochote amevunjika moyo, hana hamu ya kuishi. Lakini matazamio ya kibinadamu yakimfikia mtu hayamridhishi moja kwa moja. Kristo tu anatimiza hamu zote kwa kumkomboa kutoka unyonge. Majilio yanatukumbusha kila mwaka matarajio ya kweli na hivyo yanaamsha hamu ya kuishi kwa bidii ya kiroho.
BASI WOTE MUWE NA AMANI PIA UPENDO KATIKA JUMAPILI HII YA PILI YA MAJILIO NA SIKU ZOTE....AMINA!

No comments: