Showing posts with label bendera ya taifa. Show all posts
Showing posts with label bendera ya taifa. Show all posts

Tuesday, December 9, 2014

LEO WATANZANIA TUNASHEREHEKEA MIAKA 53 YA UHURU!!

AHSANTE MUNGU
BENDERA TAIFA LA TANZANIA

Mungu ibariki Tanzania
Dumisha uhuru na Umoja
Wake kwa Waume na Watoto
Mungu Ibariki Tanzania na watu wake.
Ibariki Tanzania
Ibariki Tanzania
Tubariki watoto wa Tanzania.

Tuesday, April 23, 2013

KUNA NJIA NYINGI YA KUITANGAZA BENDERA YETU YA TANZANIA...

Nimependa magauni haya nafikiri safati ijayo nami nitashona maana duh nimepeata hamu kweli--kama tusemavyo ni rangi nzuri na kila moja ina maana yake..tukianzia na..
1. Nyeusi- Huonyesha watu wa Jamuhuri ya Tanzania.
2. Kijani - Huonyesha mimea na ardhi ya Tanzania
3. Njano - Huonyesha utajiri wa mali ya asili.
4. Bluu - Huonyesha bahari inayoziunganisha sehemu za Jamuhuri ya Muungano
Haya ni maelezo  ya Bendera yetu ya Jamuhuri ya Tanzania....Si mnakumbuka tulijifunza darasa la tatu-nne vile au?......Nawatakieni wote JUMANNE NJEMA!!!!

Thursday, August 30, 2012

KUHESHIMU BENDERA YA TAIFA!!!!!!

Nimekaa hapa nikajikuta naimba huu wimbo je wewe unaukumbuka? Ungana nami katika kumbukumbu hii haya moja,mbili, tatu..............

1. Bendera ta Tanzania, ndiyo ya kujivunia,
Ilianza kupepea, mwaka sitini na moja,
Hapo inashuhudia, tunavyojitegemea,
       Muumba wetu Rabuka, ijaze yako fanaka.

2. Siku ya tarehe tisa, saa sita kamili,
                         Mwezi wa kumi na mbili, yalikuwa mambo sasa,
                    Mlima Kilimanjaro, bendera yetu hutwekwa,
                Muumba wetu Rabuka, ijaze yako fanaka.

3. Rangi kijanikiwiti, yaonyesha mbuga zetu,
     Manjano ndiyo madini, yaliyo uchumi wetu,
    Buluu huonyrsha maji, yaliyo nchini mwetu,
Nyeusi ni yetu sisi, Waafrika asilia
Muumba wetu Rabuka, ijaze yako fanaka.

4. Bendera yetu mwanana, yajulikana bayana,
Duniani twatukuka, katu hatuwi mateka,
   Bendera yapeperuka, Uchina na Amerika,
Wala haitatatuka, na juani kuchujuka,
  Muumba wetu Rabuka, ijaze yako fanaka.
.......................................................................................................................
Kama sikosei ilikuwa darasa la sita au la saba