Nimekaa hapa nikajikuta naimba huu wimbo je wewe unaukumbuka? Ungana nami katika kumbukumbu hii haya moja,mbili, tatu..............
1. Bendera ta Tanzania, ndiyo ya kujivunia,
Ilianza kupepea, mwaka sitini na moja,
Hapo inashuhudia, tunavyojitegemea,
Muumba wetu Rabuka, ijaze yako fanaka.
2. Siku ya tarehe tisa, saa sita kamili,
Mwezi wa kumi na mbili, yalikuwa mambo sasa,
Mlima Kilimanjaro, bendera yetu hutwekwa,
Muumba wetu Rabuka, ijaze yako fanaka.
3. Rangi kijanikiwiti, yaonyesha mbuga zetu,
Manjano ndiyo madini, yaliyo uchumi wetu,
Buluu huonyrsha maji, yaliyo nchini mwetu,
Nyeusi ni yetu sisi, Waafrika asilia
Muumba wetu Rabuka, ijaze yako fanaka.
4. Bendera yetu mwanana, yajulikana bayana,
Duniani twatukuka, katu hatuwi mateka,
Bendera yapeperuka, Uchina na Amerika,
Wala haitatatuka, na juani kuchujuka,
Muumba wetu Rabuka, ijaze yako fanaka.
.......................................................................................................................
Kama sikosei ilikuwa darasa la sita au la saba