Tuesday, December 28, 2010

SALAMU/BARUA KUTOKA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO:- SHUKRANI KWA WOTE!!!

Habari zenu jamani!!
Zimebakia siku chache tu kuumaliza mwaka huu 2010 na kuingia katika mwaka mpya 2011. Hakika miaka inayoyoma na watu tunazidi kuzeeka. Ninachotaka kusema ni kwamba, blog ya MAISHA NA MAFANIKIO inapenda kuwashukuru wanablog wenzake wote, wasomaji wote na watembeleaji wote kwa ushirikiano mzuri tulioonyeshana.

Najua katika maisha watu wote hawawezi kuwa sawa yaani kimawazo. Lakini katika hizi blog zetu kwa asilimia kubwa imekuwa ni changamoto kwetu. Tumekuwa hatupendi kupoteana, mara mmoja wetu anapokuwa kimya kwa muda basi wengine tunakuwa hatuna raha tunachukua hatua ya kumtafuta. Hii yote inaonyesha ni jinsi gani ukaribu wa wanaBLOG sisi tu/ulivyo, hakika najivuna sana kwa uwepo wenu na kwa hili napenda kusema SISI SOTE NI NDUGU. NA PIA NAPENDA KUWATAKIENI WOTE KILA DOGO NA PIA KILA KUBWA MTENDALO LIWE JEMA. NA MWAKA 2011 UWE WENYE MAFANIKIO. KAMA KUNA KITU ULIAHIDI KUFANYA MWAKA HUU BASI JITAHIDI UFANYA KABLA HAUJAISHA. KWANI KUMBUKA HAKUNA KISICHOWEZEKANA. PAMOJA DAIMA. KAPULYA WENU!!!!

19 comments:

Unknown said...

Dada Yasinta, sitochoka kukupa kono la pongezi tena nyenyekevu toka kona hii ya Waungwana. Kona hii yatambua kuwa bila mchango wako basi mwendo ungekuwa ni wa kobe mzee... Nakushukuru sana na nakutakia kila la kheri kwa niaba ya Mama wa Uungwana (Mama Naima) na Naima. Kila la kheri dada na Mungu akulinde wewe na familia.

Simon Kitururu said...

Amen!

Wait a minute,...

...Unauhakika kweli hakuna kisichowezekana au tunapeana tu moyo?:-(

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Mrope! Kwanza nachukua nafasi hii na kusema ahsante sana na pia pongezi kwako kwa kutochoka kupita katika kona hii na pia ahssante nyingine kwa wifi yangu mama Uungwana(mama Naima) Nanyi Mwenyezi Mungu awalinde, furaha na amani atawala nyumbani mwenu. Mbarikiwe sana!!

Simon! ni kweli kabisa hakuna kichowezekana kama kweli umedhamiria kulifanya jambo nakuambia utalifanya tu.

Simon Kitururu said...

Kwa mfano mie nimedhamiria kuonja chakula cha usiku cha Yasinta,...
na labda hilo NI MOJA ya yasiyowezekana!:-(

Sasa huoni dhamira zangu zitakapo kwamia wakati YASINTA Ngonyani ,...


(Samahani jina la aliyekabidhiwa vionjo SHEMEJI silijui)


.... ni MKE wa mtu?

Na hudhani DHAMIRA za KUKU kupaa kama NJIWA wakati anafukuzwa na BATA zaweza kuwa ni dhamira tu na hakuna liwezekanalo.


Ndio ,...
... nakubaliana na yote ya kutiana MOYO,...



... lakini kuna mengine awezayo ni KIKWETE na sio Prof LIPUMBA na labda ndio maana aliye RAIS sio hata Profesa ambaye ni KIKWETE ,....

ingawa wote ya PROFESSOR LIPUMBA katika kutaka URAHISI kama RAIS KIKWETE Tanzania twayajua.:-(


Samaani kwa ku-EDIT comment ya kwanza!:-(

Mwanasosholojia said...

Shukrani sana Da' Yasinta! Lazima nikiri kuwa kibaraza chako ni moja ya vibaraza maridhawa vinavyonifanya niuone wajibu wa kushirikiana katika kubadilishana mawazo na kujenga urafiki na udugu.Mtakatifu Kitururu komenti yako ya pili imenivunja mbavu...teh!teh!

Simon Kitururu said...

@Mwanasosholojia: :-)

Lakini sitanii!
Ingawa labda kila kitu chadaiwa chawezekana kinadharia,...
... ila wote twajua hata ya YESU mpaka leo kuna wengi wanaoweza kusema hayawezekani kwa kuwa mpaka leo hayajawezekana.:-(

Yasinta Ngonyani said...

Simon:-) hapo nawaachie wengine wajibu.

Kaka Mathew! ahsante sana kwa hilo nimefurahi kusikia kuwa Maisha na Mafanikio ni maridhawa.

Na simon tena! IMANi, kuamua kwa dhati ndio msimamo!

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

simon mimi naamini wewe na yasinta mnaweza piusiniulize kwa nini

Simon Kitururu said...

@Komandoo Kamala:DUH! Mke wa mtu huyo kwa hiyo nasikia kidude HATA KIDHAMBI kina kifuniko na kuingia kingi!


AU?

mumyhery said...

shukran Yasinta tupo psmoja!!!

John Mwaipopo said...

yasinta ngonyani ndaga fijo ni nongwa syako isya kusumusya inyinogono isya abandu. kama hujaelewa mie simo

yeah nnachotaka kusema ni kuwa tumekuwa pamoja na tuombe nguvu kuu iendelee kutufanya tuwepo pamoja.

John Mwaipopo said...

yasinta ngonyani ndaga fijo ni nongwa syako isya kusumusya inyinogono isya abandu. kama hujaelewa mie simo

yeah nnachotaka kusema ni kuwa tumekuwa pamoja na tuombe nguvu kuu iendelee kutufanya tuwepo pamoja.

EDNA said...

Kwako pia Dada Yasinta,

Mija Shija Sayi said...

Asante Yasinta, huyu Kitururu ana yake lakini yote yanawezekana...

Ubarikiwe.

Masangu Matondo Nzuzullima (MMN) said...

Kublogu raha jamani. Nyote barikiweni!!!!

Salehe Msanda said...

Asante
Kila la kheri na tunashukuru kwa kuonyesha unajali michango na mawazo yanablog.

Nadhani umefanya majo ya habari moja uliyowahi kuiweka katika blog ya kushukuru na kuwapenda wengine.
Daima tuonyeshe moyo wa kujipenda na siyo kuwa na tamaa au njaa ya kutaka kupendwa na kuacha kuwapenda wengine. Upendo uliouonyesha unadhirika pale uliposema kuwa hatuwezi kuwa na mawazo sawa na kutafutana pale mmoja anapopotea.
Hii ndiyo maana ya upendo sahiohi kumkubali mtu bila ya kutaka kumbadilisha na kuwa kama wewe unavyotaka.

Tuumalize mwaka mpya na kuanza mwaka mpya kwa kuwa na malengo,maana sisi binaadamu hasa watanzania wengi tunaishi bila ya malengo wakati wadudu mfano nyuki wanamalengo na shughuli maalum ya kufanya kila siku.

Badala ya kukata tamaa katika maisha tuiige au tujifunze katika suala la chanzo cha mto na kule unakoelekea hata siku moja hautaona mto unarudikule ulikotoka bali kukiwa na kikwanza unamianda upande mwingine na kuelekea na safari ya kufika mwisha wa mto husika.
Mfano hiki ninachoongelea cha chanzo cha mto mimi nimejifunza katika chanzo cha mto zambezi kipo katika Wilaya ya Njombe,sasa fikiria kutoka Njombe hadi zimbabwe huo mto umepita katika maeneo mengi na ya aina mbalimbali TUJIFUNZE katika hilo

Kila la kheri.

Rachel Siwa said...

mimi nikuite dada mkubwa si kwa umri tuu kwa busara, upendo,na umoja!
ubarikiwe pamoja na shemeji na watoto wetu pia!.

yanmaneee said...

curry 6
yeezy shoes
nike sneakers for women
jordan shoes
yeezy shoes
valentino shoes
lebron 10
nike air max 97
golden gooses
goyard

Unknown said...

check here bags replica gucci Bonuses important link you can find out more you can try these out