Thursday, December 16, 2010

AFRIKA NA UZURI WAKE !!!!


Mara nyingi huwa najiuliza hivi watu wana picha gani kuhusu Afrika yetu??

8 comments:

malkiory said...

Ni maarafu zaidi kama bara la umasikini na maradhi! Uzuri wa bara letu ni dhahiri. Tatizo ni ubinafsi wa watawala wetu wa bara la Afrika. Ona kinachotokea kule Ivory Coast!

MARKUS MPANGALA said...

Dada Yasinta kwa hakika yako mengi mazuri, lakini ukiangalia historia yetu jinsi maprofesa wazima na ndevu zao na matiti yao wakaandika mengi ya kulikebehi bara hili.

lakini uzuri wetu asilani haujifichi

Mbele said...

Ndugu Mpangala, naafiki malalamiko yako. Mimi nimejitafakari, nikaona niwajibike kwa kuandika kuhusu uzuri wa bara letu, hasa nikizingatia kuwa mimi ni mmoja wa hao maprofesa wenye ndevu zao :-).

Nimeanzia na nyumbani, kama vile Mbamba Bay, Longido, Lushoto, na Litembo.

Halafu, nimetambua kuwa watu sehemu mbali mbali duniani wanasoma hizi taarifa, kila siku. Inanitia moyo na kunipa ari ya kuendelea kuandika.

Kwa maana hiyo, utakaposikia nimetua Lundu, kaa mkao wa kula :-)

Mzee wa Changamoto said...

Labda kuuliza ni UZURI NI NINI?
Wapo wanaoona nyumba za TEMBE kama za kimaskini ila ukiwaelewesha namna ambavyo watu waishio katika mazingira hayo walivyofikia kujua kukabiliana na mazingira yao kwa kutumia nyumba hizo, sio tu wanaona ni nzuri, lakini ni za "akili"
Nilipokuwa nawasilisha mada moja darasani nilijaribu kuweka uwiano wa maisha ya mafunzo ya kikomandoo na maisha ya kila siku ya mMASAI ama mHADZAbe na tuliishia kukubaliana kuwa mMasai wa kawaida angestahili heshima kama Nacy Seal wa kiwano cha chini
Labda tatizo ni sisi tunaojua ukweli na umuhimu wa kuwa tulivyo na kisha tukapuuzia na kutojenga hoja m'badala juu ya sisi.
Na wale wasiojua (na kutokuwa na fikra za kutaka kujua) hawajali kuhusu kuchimba tujuavyo
Tatizo ni kuwa "tumebinafsisha kila kitu hata fikra zetu kuhusu sisi".
Si umesikia RAISI ANAWAOMBA WASOMI KUANDIKA VITABU KUHUSU MAISHA YA VIONGOZI WA NCHI?
Yaani hata maisha yake binafsi ya kimaamuzi anataka aandikiwe na Profesa fulani
Anyway....nahisi naanza kwenda "nje ya ndani"
Labda niache kwa sasa na TUONANE "NEXT IJAYO"

Salehe Msanda said...

Watu hasa wa mataifa ya wenzetu na hasa mataifa yaliyoendelea wanaipenda na kuitukuza afrika na kutamani ingekuwa ni bara lao tatizo liko kwetu sisis waafrika hatuna mapenzi mema na bara leta na tunatafuta visingizio vya kuwalaumu wazungu kuwa wamecahngia hali ilivyo katika bara letu.
Ni kweli AFRIKA ni bara zuri na mlenye kuvutia. Tuanze kulipenda na kuliendeleza kwa nguvu zetu zote.
Na la muhimu Waafrika tunatakiwa kujipenda wenyewe na kulipenda bara letu. Asante kwa burudani !!!

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

kwani wewe unapicha gani mwafrika uliyekimbia afrika????

mimi siwezi kuikimbia na ninaishi vijijini afrika, najua uzuri wake

Yasinta Ngonyani said...

Kamala kutoishi Afrika sio sababu kwani kuna uwezekano mkubwa aishiye Afrika akaishi tu bila kufanya lolote na nchi yake na asiyeisha Afrika akaipenda na kufa kitu kizuri kuhusu nchi yake.

Robert Vumu said...

kuishi Afrika au Ulaya sio kitu, bali nidalili ya kwamba sisi sote ni watoto wa baba mmoja na hii ni matokeo ya globalization, nategemea kabisa kusingekuwa na mwingiliano huo hata uzuri tunaouona ktk picha tusingeuona tatizo ni lile la ubinafsi la watawala wetu.