Wednesday, March 23, 2016

SABABU 4 AMBAZO KAMWE HUPASWI KUACHA KWENDA HAJA NDOGO PALE MAUMBILE YANAPOTAKA UFANYE HIVYO…


ANAHITAJI KWENDA HAJA NDOGO
Wote tunajua kwamba pale tunapokuwa tumebanwa  kweli kweli na haja ndogo(mkojo).
Wakati mwingine huwa tunalazimika kwa muda mrefu kukaa bila kwenda haja ndogo na
hata mwishowe kuhisi kana kwamba kibofu kinataka kupasuka.
Wakati mwingine tunakuwa katika sehemu ambazo hakuna maliwato yaliyoko karibu na
wakati mwingine huwa tunakuwa na marafiki tukipiga soga kiasi kwamba hutuwia
vigumu kuacha kukatisha mazungumzo ili kukidhi hitaji hilo la kimaumbile, lakini pia
wakati mwingine huweza kuwa na foleni ndefu kwenda maliwato hasa katika maeneo ya
Mighahawa au maeneo ya jumuia.
Zipo sababu nyingi kwa nini wakati mwingine yatupasa kuvumilia/kutunza  mkojo kwa
muda mrefu iwezekanavyo kutokana na maeneo tuliyopo kutokuwa rafiki katika kukidhi
hitaji hilo la kimaumbile lakini ni vyema tukijua kwamba jambo hilo lina athari kubwa
kiafya kwetu.
Kwa nini inasisitizwa kwamba tunapokuwa na hitaji hilo la kimaumbile tutafute mahali pa
kujisitiri haraka iwezavyo. Ni kwamba kibofu cha mkojo ni chombo ambacho kinaweza
kubeba/kutunza hadi lita 0.5 za mkojo. Wakati kibofu kikiwa kimejaa kama theluthi mbili
ubongo huwa unapata hisia kwamba ni lazima ukojoe. Lakini kwa sababu mawasiliano
kati ya kibofu cha mkojo na ubongo ni sehemu ya mfumo wa neva involuntary, unaweza
kuamua ni muda gani unaweza kukojoa - hivyo kuna wengi ambao wanaweza kukaa na
mkoja kwa muda mrefu, lakini hata hivyo ni vyema tukijua kwamba jambo hilo ni hatari
kwa afya zetu.
Hizi hapa ni sababu nne(4) kwa nini hupaswi kukaa na mkojo kwa muda mrefu.
1. Unaweza kupata maambukizi kwenye njia ya mkojo
Kama hukojoi kuna hatari bakteria kuwa wengi/kuzidi katika mkusanyiko wa mkojo huo 
watafiti wa (illusterad vetenskap) wanasema wakati unapokojoa bakteria wanatoka nje
ya vimelea(bomba la mkojo). Bakteria, mara nyingi koli bakteria kutoka kwenye utumbo
inaweza kusababisha magonjwa ya maambukizi kwenye njia ya mkojo ambayo inaweza
kukua na kuwa hatari kwa figo. Hii kwa upande mwingine inaweza kusababisha sumu
kwenye damu utafiti umegundua hivyo.
2. Kibofu cha mkojo chaweza kuvuja mara kwa mara.
Kama unatunza mkojo mara nyingi kibofu cha mkojo wako kitatanuka na kuwa kilegevu.
Hii inaweza kusababisha tatizo la udhaifu wa kibofu kuwa mtepetevu ambapo mkojo
unaweza kuwa unatoka wenyewe matone  matone  kila wakati na matone huishia
kwenye nguo ya ndani na hapo ndipo mtu hujikuta unanuka mkojo mara kwa mara.
3. Unaweza kusababsha uharibifu wa figo:-
Mkojo unaozalishwa katika figo wakati unapoutunza mkojo huo kwa muda  mrefu kiasi 
cha kibofu cha mkojo kukaza kwa kuzidiwa basi figo hufanya kazi ya kupeleka mkojo
katika njia ya bomba la mkojo kwa shinikizo (presha) na unapoendelea kuzuia ndipo
unaposababisha athari kiafya. Utafiti wa Illustrared Vetenskap umebainisha kwamba hali
hiyo inaweza kusababisha uharibifu wa figo.
4. Kibofu cha mkojo kinaweza kupasuka na tumbo lako kujaa mkojo.
Kibofu cha mkojo kinaweza kupasuka. Lakini ni nadra, kwa kawaida watu ambao
wamepata tatizo la kibofu cha mkojo au ulevi ambapo mwili waweza "kusahau" kukojoa.
Wakati kibofu cha mkojo kikipasuka mkojo hutawanyika katika tumbo na unaweza
kueneza maambukizi na pia huwa na maumivu makali sana na athari nyingine kiafya.
NIMEONA NIWASHIRIKISHE HABARI HII ILI TUWE MAKINI KWENDA DAIMA HAJA
NDOGO PALE TUNAPOHITAJI, ILI KUEPUKA HIZI HATARI.
CHANZO: NEWSNER VATENSKAP.

No comments: