Tuesday, March 15, 2016

MAISHA:- JAMBO LA KUKUMBATIANA NA FAIDA ZAKO.........

Kukumbatiana husaidia uzalishaji wa homoni ya "oxytocin" ambayo husaidia sana mwili kuondoa tatizo la kuhisi upweke, hasira na kutengwa.
Unapomkumbatia mtu, unaupa mwili hali ya kujihisi salama na huru pia. Kukumbatiana hufanya misuli isinyae hivyo kuondoa/kupunguza baadhi ya maumivu ya mwili na kuufanya uwe huru. Kukumbatiana huboresha mahusiano ya watu wanaopendana, kwani unapomkumbatia mtu unaonyesha hali ya kupenda, usalama na mapenzi ya dhati. Pia kukumbatiana huondoa wasiwasi. Kama ulikuwa unajiona si wa thamnai, basi ukikumbatiwa unajiona wa thamni. Kumbuka tulipokuwa wadogo, wazazi wetu walitukumbatia na tukajiona tunapendwa na tuko mahali salama. Upendo ule tulioonyeshwa na wazazi wetu unakuwepo ndani yetu kadiri tunavyokuwa watu wazima. Pia unapomkumbatia mtu inakufanya uhisi kupendwa na kuwa wa thamani. Kukumbatia/wa huleta usawa kwenye mfumo wa fahamu kwani wengi wetu tunaishi mazingira yanayoufanya mwili kuwa katika hali ya kujihami muda wote. Hivyo unapomkumbatia/wa mtu mwili husinyaa na kurudi katika hali yake ya kawaida. Kukumbatiana hutufundisha kutoa na kupokea. Kukumbatiana hushusha shinikizo la damu mwilini, mguso wa mwili husababisha neva za kwenye ngozi zinazoitwa "pacinian corpuscles" kupeleka habari kwenye sehemu ya ubongo inayo husika kushusha shinikizo la damu.
Ndio maana watoto wanaokumbatiwa kwa kiasi kikubwa wakiwa wadogo huwa katika hatari ndogo zaidi ya kupata msongo wa mawazo kuliko wasio kumbatiwa vya kutosha.

No comments: