Wednesday, October 13, 2010

HONGERA SHANGAZI YANGU PAULINA ARIANNA BANDIO KWA KUTIMIZA MWAKA MMOJA

mtoto Paulina mwaka mmoja leo
Binafsi nitakuita Shangazi/rafiki yangu. Lakini kuna wengine watakuita
binti, mtoto, binamu, mpwa n.k.
Shangazi/rafiki yangu Paulina leo ni siku kubwa sana kwako. Ni mwaka sasa
umepita tangu uyaanze maisha yako. Yaani leo unatimiza mwaka 1(mmoja) kwa
kweli miaka inakimbia sana, ni juzi tu ulikuwa kachanga leo hii umekuwa
binti wa kuweza kukutuma utuchotee maji ya kucnywa na karibuni tu utatupikia
na hata ugali.
Blog ya Maisha na Mafanikio inapenda kutoa pongezi nyingi sana kwa wazazi wa binti Paulina ambao ni Mubelwa na Esther Bandio kwa malezi
mazuri wampayo mtoto Paulina. Mwenyezi Mungu awazidishia nguvu ili muzidi
kumlea mtoto huyu na awe kama ninyi wenyewe.
Unaweza kuwatembela Mubelwa.

6 comments:

Simon Kitururu said...

Hongera Paulina!

John Mwaipopo said...

'ongela' paulina kwa kuchana kalenda moja. vipi ushaanza kujifunza kihaya?

MARKUS MPANGALA said...

Tulizaliwa ili tuwapende, hatukuumbwa tuwe na tabia mbaya bali tumejitungia wenyewe. Hakika uujaliwe mengi mema yenye heri na fanaka daima. Kila kilichopo moyoni mwako kiwe na amani. Ungeweza kujisomea sana FALSAFA za Mtakatifu Kitururu, hakika mie amenijuza na kunibadilisha baadhi ya mitazamo. Kwahiyo tunachokuomba PAULINA a.k.a PAULINHO mungu akupe jema daima. iwe usika ama mchana

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

hongela mweee!

Mija Shija Sayi said...

Paulina unaonekana si mvivu wa kula. Hongera sana, Mungu azidi kukupa afya tele uendelee kupendeza. Wazazi pia hongereni kwa usimamizi mzuri wa Paulina. Mbarikiwe sana. Amina.

Mzee wa Changamoto said...

Sikuwepo kompyutani
NAPENDA KUWASHUKURU NYOOOTE WALEZI WA PAULINA.
Kwa niaba ya nusu yangu njema na "zao" tulilojaaliwa, TWAWAPENDA NA KUWAHESHIMU SAAANA


Da Yasinta.........GRACIAS!!!!