Tuesday, October 19, 2010

Swali:- Ni heshima/Adabu au ni Utamaduni/mila:- Yaani jinsi ya kuitika twiitwapo?

Nimekuwa nikijiuliza muda sasa umepita. Na sijapata jibu. Tangu nilipokuwa mtoto mdogo nimekuwa nikisikia watoto,vijana na wazee wakiitika kwa mtindo tofauti nikiwa na maana Wanaume/wavulana wakiitwa wanaitika NAAM. Na wanawake/wasichana wakiitwa wanaitka ABEE/BEE!.
Nimefanya utafiti hasa hapa Sweden kwa kweli MmmmH. hiyo haipo kabisa utakuta unamwita mtoto anatitika NINI? au EEEHH! Hapo ndio niliposema ama kweli TEMBEA UONE. Sijui wenzangu mnasemaje naomba tujadili kwa pamoja . UMOJA NI NGUVU NA UTENGANO NI UDHAIFU. Karibuni!!!!

No comments: