Friday, October 8, 2010

Labda KUNA ambao HAWANA furaha mpaka wapate MTU MWINGINE au KITU KINGINE kisicho chao cha kukichukia au tu kukiona ni USHUZI!

Mt. Simon Mkodo Heriel Kitururu anasema...

Ukichunguza ,....
.... unaweza kupata MAFILINGI kuwa kuna wengi YAO huleta maana tu kama kwao YAWENGINE ni ushuzi.:-(

Ze mfano:

Labda MWENYE tabia nzuri furaha yake katika UPATAJI WAKE maana katika furaha zake ni kwa kuwa wengine anafikiri wana TABIA mbaya kwa hiyo yeye katika jamii anathamani zaidi .:-(

Labda Mkristo katika kufurahia UKRISTO wake- kunaleta maana tu pale astukiapo kuna WAISLAMU na WENGINE wenye dini za KIGAGAGIGIKOKO ambao afikiriao hawataenda mbinguni kwa kuwa si WAKRISTO kitu kimleteacho faraja katika UKRISTO wake ambao anaamini ni YESU tu ndio njia ya kwenda kwenye utamu.:-(

Kwenye Ukristo wa KISABATO labda faraja ni kustukia kuna WAKATOLIKI , Walutheri na hata wale WALOKOLE wa KIKAKOBE ambao kwa kisabato kuna kitu wanakosea katika mwendo wa maringo wa kulenga mbinguni kitu kifanyacho USABATO mtamu.:-(

Wenye akili kwa kuwa wanapasi MITIANI labda furaha ni kwakuwa kuna wajinga waliofeli naa ambao hata kushusha hoja kisomi hawawezi.:-(

Kwa KIMWANA mzuri SURA KAMA CHUNUSI -labda faraja huletwa na uwepo wa VIMWANA wenye sura kama JIPU kitu kisababishacho Kimwana mwenye sura kama chunusi kujisikia ahueni kwa kuwa anasifiwa zaidi ya mwenye sura kama jipu na katika kuchuna buzi akaunti yake hujaa kirahisi zaidi.:-(

Wayahudi labda huhitaji walimwengu wengine ili wajisikie kuwa wao ndio Taifa lililochaguliwa na Mungu kwa hiyo wao spesho.:-(

Ndio ,....
.... labda hakuna mwenye FURAHA kamili kivyake kama hakuna WENGINE na vya wengine vya kunyoshea vidole,.....

.... ili kuhalalisha kuwa vyangu vinaunafuu kitu ambacho husaidia baadhi ya watu ndani ya kibano KUSAIDIA ombaomba mtaani ikiwa ni MOJA YA NJIA ya kujisaidia kupata Uahueni kuwa angalau pamoja na kuwa MAISHA ni magumu lakini angalau mimi bado sijafikia kuwa ombaomba mtaani ingawa ni malaya kidooooogo.:-(

Swali:

SI kuna waonao mgonjwa nakupata unafuu kuwa angalau WAO ni wazima kama tu vile WEWE ukiona MZEE aliyefikia kujinyea ujisikiavyo vizuri kuwa angalau wewe bado kijana na BADO wewe unaweza kwenda mwenyewe chooni kushusha kilo kadhaa za kilichowahi kuwa chakula kwa MAMA N'TILIE?
SI kuna MKE WA MTU akiona MME wa mwenziye ni MZURI zaidi hupunguzwa faraja ya kuvumilia angalau vijambo a.k.a MASHUZI ya MME WAKE YA KILEVI aliyelala naye kitanda kimoja baada ya huyo MME kutoka BAA na kudai kwa nguvu chakula cha usiku cha ushindi wa haraka haraka kimagoli?
Ndio,....
....labda faraja zako hutegemea sana ufikiriavyo mapungufu ya wengine hata wasiokuhusu.:-(
Habari hii imeandikwa na Mzee wa mawazo Mt. Simon Kitururu . Nimeona si mbaya kama nikiibandika hapa kibaraza cha Maidha na Mafanikio.

6 comments: