Friday, February 19, 2010

Hongera Kwa Siku Ya Kuzaliwa Kaka SAVIO!!!!

2007 Ruhuwiko!!

Wote tunakutakia kheri sana kwa siku hii maalum kwako kwa kutimiza miaka. Twakutakia mafanikio mema katika maisha na kila jambo ufanyalo pia familia yako . Kumbuka kwamba sisi ndugu, marafiki, wajombo, watoto, shemeji twakupenda sana. HONGERA KWA SIKU YA KUZALIWA KAKA SAVIO.!!!!

Kwa vile leo pia ni Ijumaa basi ngoja tusherehekee siku yako kwa kipande hiki cha muziki:-)

19 comments:

Mija Shija Sayi said...

Hongera kaka Sovio. Mungu akulinde na kukuongezea miaka zaidi.

Jamani yasinta mbona mwenzenu mmempa jina la kiitaliano...lol!

Yasinta Ngonyani said...

Da Mija sio mimi ila baba yetu alisoma na waitaliano na alinusurika kuwa Padre. Ndio maana tuna majina ya ajabuajabu:-)

Fadhy Mtanga said...

Hongera sana braza Savio. Uwe na maisha marefu.

Da Yasinta sikufahamu umeongeza utamu jina la blog. We mkali. Limependeza.

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

Da Mija: hilo si la kiitaliano bali la KILATINI....lol

Da Yasinta: Alinusurikaje? nani alimnusuru?...lol

Mija Shija Sayi said...

Swali zuri Chacha.

Yasinta Ngonyani said...

Ok, Samahani kwa kupindisha kiswahili kaka Chacha na Da mija ni kwamba alitaka kuwa padre lakini kwa bahati mbaya kulitokea kitu fulani ntamuuliza na nitawajibu ni kitu gani. Upendo Daima. Hongera kwa siku ya kuzaliwa Savio

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

Hongera kaka Savio....ujaaaliwe nguvu na miaka ya kuwaona wajukuu na vitukuu!

John Mwaipopo said...

'ongela' ndugu savio. mungu akunyooshee mapito, upate miaka tele hata uone watoto wa wajukuu wako.

watila said...

hongera kaka sovio hongera kwa siku yako ya kuzaliwa mungu aibariki familia yenu ma head phone ya nini dada Yasinta

watila said...

umefana na kaka deo kweli dayasinta
kumbe ni style ya nyele mimi nilifikiri ni headphone lol

chib said...

Usisahau kunywa ulanzi kidogo ukiwa umechanganya na pingu, ndo sherehe za kijadi. Hongera sana

John Mwaipopo said...

du pingu!

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

YES! Lakini sherti afunge sarawili kwa chini ili spring na skrubu zitakapolegea awe ngangariii....lol

Koero Mkundi said...

Hongera kaka Savio kwa kusherehekea siku yako ya kuzaliwa,
nakutakia maisha marefu

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

nje ya mada,:

eti mafanikio ninini?

EDNA said...

Happy birthday Savio,Mungu akuongezee miaka mingi zaidi.

mumyhery said...

Happy Birthday Kaka Savio

watila said...

kamala kufanikiwa ni wishes
wanting something to happen
I wish she will say yes

Christian Bwaya said...

Mwaipopo: 'ongela' sio? napenda sana kiswahili chako.

Kwenu wadau: kwa kuzingatia maana hasa ya neno hongera, je tunapompa hongera mtu fulani kwa kufikisha miaka kadhaa, huwa tunamaanisha nini? Kuna alichofanya kuchangia idadi hiyo ya miaka au?