Tuesday, February 2, 2010

WAREMBO WA LEO:- NAJIVUNIA MAVAZI YETU YA HESHIMA NA UTAMADUNI WETU

Hili vazi nimelimeze mate kweli

Hapa ndo natamani kama nimvua na nilivae mimi.

13 comments:

Lulu said...

Kwa kweli hata mimi mavazi haya yamenivutia sana. Natamani sana tungekuwa na vazi letu la taifa kama ilivyokuwa kwa Uganda, Burundi na Nigeria. yaani mtu akivaa vazi fulani unajua tu huyu ni mnigeria au mganda. Jamani tufanyeje ili tuweze kupata vazi letu la taifa

Chacha o'Wambura a.k.a Ng'wanambiti! said...

Ntakutafutia hizo nguo Da Yasinta wala usikonde :-) kwani hakuna haja ya kumvua huyo nguo zake....lol

wakati weye unalitamani wenzako wanawaona hao kama wanaojikomba ama kujipendekeza kwa nchi yao kwa kuvaa maguo yenye rangi za bendera taifa :-(

ila inapokuja kwa maswala ya kitaifa unadhani kuwa nguo na maana ama fasheni? kwani hujaona sherehe ya UHURU 90% ya wahudhuriaji wanavaa nguo za kijani na kofia za njano wakati walobaki wanavaa suti?

Je hii inaweza kutafsiri kuwa uzalendo ushatoweka?

waweza kushangaa pia kuona majamaa wanashabikia kununua bidhaa ikiwamo mbogamboga za nje katika maduka makubwa a.k.a supermarket wakati akina mama wanasota gulioni na mboga zao zinadoda!

mh!

EDNA said...

Inapendeza kwa kweli

Lulu said...

Ng'wanambiti una changamoto weye!!!

Faith S Hilary said...

yup yup yup dada! Bendera yetu ina rangi nzuri na zina-"blend" in together...nguo nzuri kweli

chib said...

Big up Chacha, wewe mzalendo asilia.
Suti kali na joto la Dar, yaani .. labda kama zina ka kiyoyozi ndani kanakoendeshwa na harufu ya jasho :-(

@Yasinta, hiyo tamaa yako.... yaani mpaka unafikiria kumvua mtu hadharani kabisa, thatha thi utamuaibisha!

Mija Shija Sayi said...

Yasinta niandalie vipimo vyako nikushonee moja utulie roho.

Wamependeza kwa kweli.

mumyhery said...

wamependeza mno, kwa mama wa kwanza kupendeza ni kawaida yake!!!

Chacha o'Wambura a.k.a Ng'wanambiti! said...

Da Mija: ulijifunzia wapi kushona? usije ukamshonea nguo akaonekana kituko badala ya kurembuka :-)

Mija Shija Sayi said...

Chacha, mimi ni moto wa kuotea mbali katika Cherehani...

Chacha o'Wambura a.k.a Ng'wanambiti! said...

Da Mija: hongera kwa hilo...

lakini...kwa kukosa uzalendo si waweza kujikuta umeshona tenge katika mtindo wa kumfaa zaidi Madonna kuliko Yasinta? :-(

halafu tukimwona tutaanza kusalimia 'Hi ms Yasinta' (ataonekana nzungu na kituko zaidi a.k.a mashing'weng'we) badala ya 'mlongo vangu, unyumwike? :-(

Mija Shija Sayi said...

Sio siri Ng'wanambiti...

Yasinta Ngonyani said...

Da Mija nitakupaje vipimo hata e-mail yako sina tuma ujembe kwangu ntakupa vipimo au ndo yale mambo ya utani utani tu?