Sunday, March 30, 2008

Machi 30,2008 HALI YA HEWA/PASAKA

Naam! wasomaji nafikiri mmesoma blug yangu kuhusu pasaka. kama hujasoma basi chukua fulsa na usome. Kwa kweli nakuambieni ama kweli watu wana mila na desturi. nimeshuhudia sio kula mayai tu kama nilivyosema isipokuwa kuyapaka rangi tofauti baada ya kuchemshwa. Haya sasa najua sehemu nyingine kama Afrika (TZ) pasaka imesheherekewa na jua/joto. Sio hapa kuna baridi na pia theruji ilianguka. Samahani kidogo nimeingia kwenye hali ya hewa hii yote ni kwa sababu sikutegemea kutakuwa na baridi kali hivi. Nafikiri ni kwa sababu hali ya hewa imebadilika kwani hii theruji ilibidi iwe krismas sio sasa. Lakini sasa inaonekana kuna mabadiliko. Ngoja nirudi kwenye Pasaka tena, kama nilivyosema. jumamosi kuu ndio sikukuu kubwa hapa sio Jumapili (pasaka kwa sisi ) nina maana watu wengi pamoja namimi tunajua kuwa jumapili dio PASAKA.
Katika blogu ya mdogo wangu KARIBU NYASA amenikumbusha mbali sana. Yaani ameniacha hai kabisa. Maana inaonekana huko Pasaka ilikuwa nzuri sana wamatengo na ngoma zao, wangoni/wamanda na zao pia vinywaji nk. mpaka natamani.

Na; Yasinta Ngonyani

1 comment:

Anonymous said...

Youг root may payіng to plаy games, then of line іt ωould be youг job.
Paгеnts can besideѕ Direct Piecе in many kіnԁѕ of puzzlе Onlіnе Gаmes on thе web or get а Taκe hоld of these citizenry onlinе.

Bhaг katora dudh da ni Extremеly plaуeԁ Unloosеn online gаmes
which Serve the role plауer Stimulate
use of his mentatіon mental ability.

Stop bу my web pаge weblearningit.com