Monday, March 17, 2008

machi 17,2008 pasaka

Haya wasomaji naona sasa pasaka inakaribia.Nimekaa na nimeamua niwaeleze kidogo mila na desturi wakati/kipindi hiki cha pasaka huku ninakoishi ni tofauti sana na huko nyumbani.ngoja nianze kuwaeleza kuliko kuanza kuwachosha. Ni hivi alhamisi kuu ni kama kawaida au nimesahau sijui yaani watu wanakwenda kazini kama kawaida. Ijumaa kuu baadhi ya watu hawafanyi kazi na JUMAMOSI KUU hapa ndio sikuuu kubwa sio kama huko nyumbani sikukuu ni jumapili. Haya sikiliza sasa siku ile ya jumamosi watu wote ni lazima kula mayai kadiri unavyopenda bila mayai basi si pasaka tena. Halafu kitu kingine siku hii ya JUMAMOSI KUU watoto wadogo wanavaa kama wazee wa zamani. Na pia wanakuwa na barua kwenye vikapu na wanapita kila nyumba na kubadilishana na pipi. Ni mila yaani ni kama jambo la kutakiana pasaka njema. Kwa hiyo kipindi kama hiki kila mwananchi inabidi awe na pipi au matunda kama huna huna hivyo viwili basi uwe na hela. mwanzoni nilishangaa lakini sasa nimezoea.

Na; yasinta Ngonyani

2 comments:

Anonymous said...

Kula mayai mengi pasaka

Anonymous said...

Endelea kutupatia mambo ya ughaibuni ili tufaidi sana