Friday, September 16, 2011

KARIBUNI KIKOMBE CHA CHAI...NINYIME VITU VYOTE LAKINI SIO CHAI!!!


You´re Just my Cup of Tea,

Our Love Warms my Heart.

Najua wote mnajua mie ni mpenzi sana wa chai tena ile isiyo na sukari(Chingambu) :-).

Kichwa cha habari hapo juu kinasema kuwa "NINYIME VITU VYOTE LAKINI SI CHAI" Duh ! naungama ni kwamba nimesema uongo kwani mimi ni mdhaifu/mpenzi sana wa smaki pia kama ilivyo kwenye chai......



Ngoja tusikilize wimbo huu wa Nuru ft Mr Chocolate Flavour - Muhogo Andazi!!!




NAPENDA KUWATAKIENI WOTE MWANZO MWEMA WA MWISHO WA JUMA ....MUWE NA AFYA NJEMA , AMANI NA FURAHA ZITAWALE NYUMBANI MWENU/WAKO.......IJUMAA NJEMA!!!!

6 comments:

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

Aksante sana ...na wewe pia uwe na weekend njema!

issack che jiah said...

asante ila chai huwa sinywi kwvile sisi ni wakulima na wasafirishaji kwani muda wote tunanukia chai labda ubuni supu inayotengenezwa kwa chai nawe wiki mwisho jema

sam mbogo said...

Da Yasinta heri mie sijasema,ukinyimwa kublog chai itanyweka? wiki njema.kaka S

Simon Kitururu said...

Ijumaa njema kwako pia!

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Da Yacinta, karibu tena ugani tulikosa vimbwanga vyako. Bila shaka ulifaidi sana kule home.

Yasinta Ngonyani said...

Chacha! Ahsante kwa kushukuru.. wikiend yangu iliishia kazini...

Issack che jiah!
usiwe na wasiwasi hukuona kulikuwa na samaki pia hapo ungepata ugali kwani najua kwa wakulima ugali ndio poa:-)

Kaka S! Ha ha ha ha..hakika nakuambia kunyimwa kublog si kitu ila si CHAI we hapa nitapelekwa kulazwa mwenzio..na samaki ndo usijaribu:-(

Simon kakang! Ahsante:-9

Kaka NN Mhango..Ahsante kwa kunikaribisha katika ulimwengu huu..ila nadhani ni wewe sasa ulipotea sijui ulikuwa wapi? mie nimerudi kipendi tu rudi nyuma na uangalia....Kwa hiyo nasema karibu sana nawe. Pia nimefurahi kusikia kuwa mlikosa "vimbwanga" vyangu