Monday, September 12, 2011

NI JUMATATU NYINGINE TENA NA JUMATATU HII KUNA UJUMBE WAKE

Jumatatu yangu meanza safi sijui wewe mwenzangu ebu tumsikiliza Juma nature na wimbo huu wa kila siku za wiki ni mikikimikiki

Jumatatu njema

7 comments:

sam mbgo said...

Da Yasinta,jumatatu ya leo huku kwetu, UK hali yahewa siyo nzuri,tuna kimbunga sasa sijuwi kinaitwa Hadija au Jene!!? (mjina yakike hayo).upepo ni mkali kwelikweli usipo kuwa makini mtoto anaweza chukuliwa nao. mambo mengine safi tu. kaka S.

sam mbogo said...

Yasinta mbona umtoa,mada yako ya mjina,na nilikuwa nisha kutembelea halafu ikapotea' chigafula'kaka s

Yasinta Ngonyani said...

kaka S. Kwanza pole na chimbunga Hadija au labda tusema Juma. jumatatu ya leo kwangu imeanzia kazini na baadae hospitali na pia hapa hali ya hewa si nzuri upepo ila si shimbunga, pia mvua za manyunyumanyunyu. Nadhani wiki yangu imeanza kweli na mikikimikiki na itaendelea hivyo...Nimetoa ile mada baada ya kuona wiki yangu imeanza na mikikimikiki na jana niliusikiliza huo wimbo nikaona nianza hivyo na hiyo mada ya majina nitaweka wala usikonde kaka S...

Mija Shija Sayi said...

Asante kwa wimbo Da Yasinta.. na pia pole na mikiki ya Jumatatu..

@Kaka S, kumbe nanyie mmekiona kimbunga Hadija...yaani wee acha tu, sema huku kwetu kiliambatana na jua na joto pia..

Haya j'tatu njema.

Unknown said...

Dada kwanza habari za siku nyingi?
huku kwetu wazima kabisa
karibuni kwenye my blog
www.gshayo.blogspot.com

raynjau njau said...

NI JUMATATU NYEUSI KATIKA UKANDA WA AFRIKA MASHARIKI ANGA LIKIHANIKIZWA VILIO KUTOKA ZANZIBAR NA NAIROBI.

-----------------------------------
KIFO NI ADUI MKUBWA KATIKA MAISHA YA MWANADAMU
-----------------------------------
Mhubiri 7:1-29
1 Jina ni bora kuliko mafuta mazuri, na siku ya kufa kuliko siku ya kuzaliwa kwa mtu. 2 Ni afadhali kwenda katika nyumba ya maombolezo kuliko kwenda katika nyumba ya karamu, kwa sababu huo ndio mwisho wa wanadamu wote; naye aliye hai anapaswa kuliweka jambo hilo moyoni mwake. 3 Afadhali sikitiko kuliko kicheko, maana kwa kukunjamana uso moyo huwa afadhali. 4 Moyo wa watu wenye hekima umo katika nyumba ya maombolezo, lakini moyo wa wajinga umo katika nyumba ya kushangilia.

5 Ni afadhali kusikia kemeo la mtu mwenye hekima kuliko kuwa mtu anayesikia wimbo wa wajinga. 6 Kwa maana kicheko cha mjinga ni kama sauti ya miiba chini ya chungu; na hilo pia ni ubatili. 7 Kwa kuwa uonevu mtupu unaweza kumfanya mtu mwenye hekima atende kiwazimu, na zawadi inaweza kuharibu moyo.

8 Mwisho wa jambo ni bora kuliko mwanzo wake. Mtu mwenye subira ni bora kuliko mwenye roho ya majivuno. 9 Usiwe na haraka kuudhika katika roho yako, kwa maana kuudhika hukaa katika kifua cha wajinga.

10 Usiseme: “Kwa nini siku za zamani zilikuwa bora kuliko hizi?” kwa maana hukuuliza hilo kwa hekima.

11 Hekima pamoja na urithi ni nzuri na ni yenye faida kwa wale wanaoliona jua. 12 Kwa maana hekima ni ulinzi, kama vile pesa ni ulinzi; lakini faida ya ujuzi ni kwamba hekima huwahifadhi hai waliyo nayo.

13 Ona kazi ya Mungu wa kweli, kwa maana ni nani anayeweza kunyoosha kitu alichokipotosha? 14 Katika siku njema uwe mwema, na katika siku yenye msiba ona kwamba Mungu wa kweli ameifanya hata hii sawasawa na ile, ili wanadamu wasipate kuvumbua chochote baada yao.

15 Nimeona kila jambo katika siku zangu za ubatili. Yuko mwadilifu anayeangamia katika uadilifu wake, na yuko mwovu anayeendelea kuishi kwa muda mrefu katika ubaya wake.

16 Usiwe mwadilifu kupita kiasi, wala kujionyesha kuwa na hekima kupita kiasi. Kwa nini ujiletee ukiwa? 17 Usiwe mwovu kupita kiasi, wala kuwa mpumbavu. Kwa nini ufe kabla ya wakati wako? 18 Ni afadhali ushikilie upande mmoja, lakini usiachilie ule mwingine; kwa maana yeye anayemwogopa Mungu atatoka akiwa na zote hizo.

19 Hekima ina nguvu zaidi kwa mwenye hekima kuliko watu kumi wenye mamlaka waliokuwa katika jiji. 20 Kwa maana hakuna mwanadamu aliye mwadilifu duniani ambaye huendelea kufanya mema na asifanye dhambi.

21 Pia, usiweke moyoni mwako maneno yote ambayo huenda watu wakasema, ili kwamba usipate kumsikia mtumishi wako akikulaani. 22 Kwa maana moyo wako mwenyewe unajua vema kwamba hata mara nyingi wewe, naam hata wewe, umewalaani wengine.

23 Mambo yote haya nimeyajaribu kwa hekima. Nilisema: “Nitakuwa na hekima.” Lakini ilikuwa mbali nami. 24 Lile ambalo limekuja kuwako liko mbali sana na ni lenye kina kirefu sana. Ni nani anayeweza kulitambua? 25 Mimi mwenyewe niligeuka, hata moyo wangu ukageuka, nipate kujua na kuchunguza na kutafuta hekima na sababu ya mambo, na kujua juu ya uovu wa ujinga na upumbavu wa wazimu; 26 nami nilikuwa nikivumbua: Jambo lenye maumivu zaidi ya kifo, nikampata mwanamke ambaye yeye mwenyewe ni nyavu za kuwinda na moyo wake ni nyavu za kukokota na ambaye mikono yake ni pingu. Mtu ni mwema mbele za macho ya Mungu wa kweli ikiwa anaponyoka kutoka kwake, lakini mtu anafanya dhambi ikiwa ananaswa naye.

27 “Tazama! nimevumbua hili,” akasema mkutanishaji, “kitu kimoja kikichukuliwa baada ya kingine ili kujua jumla yake, 28 ambayo nafsi yangu imetafuta kwa kuendelea, wala sijaiona. Nimemwona mwanamume mmoja kati ya elfu moja, lakini sijamwona mwanamke mmoja kati yao wote. 29 Tazama! Nimeona hili peke yake, ya kwamba Mungu wa kweli aliwafanya wanadamu wakiwa wanyoofu, lakini wao wenyewe wametafuta mipango mingi.”

Mangaza Lucie said...

nanyi piyaaaaaaaaaa