Saturday, May 26, 2012

JUMAMOSI HII TUANGALIA JINSI NDOA NDOANA INAVYOKUWA....!!!!


Mmmmhh hapa kaaaaazi kwelikweli!!! NATUMAINI JUMAMOSI YAKO ITAKUWA NJEMA...

8 comments:

Simon Kitururu said...

Jumamosi njema Kadala!

Yasinta Ngonyani said...

Nawe pia Kadoda Wangu:-)

ray njau said...

Ndoa ni kama ndoana ukiwa nayo na ikivunjika inakuachia doa.

Unknown said...

kwa!

sam mbogo said...

Hapa wala sioni ugumu wa ndoa,ukiangali hii video.kila mtu anamatatizo yake ambayo mwisho wa yote nikuwa hawana mawasiliano mazuri. ndoa ndowano !!? sija ipata zaidi!?.kaka s.

Salehe Msanda said...

Ni kweli jmosi ni njema. Kila la kheri lakini tunafananisha ndoa na ndoani kwa mtazamo upi.
Tuingalieno ndoani kwa ndoa kwa upande chanya. kinyume chake tunpotoshaa ukweli wa maana ya ndoa. Tukiingalia ndoa kwa mtazamo wa kujenga tutakuwa tunafanya maisha kuwa ya furaha na kujenga familia yenye amani na fulaha. Tusitake kuwa na ndoa ya kama malaiki maana haipo na haitaokea kwanza itakuwa booring kind of marriage i think so.

Mija Shija Sayi said...

Kweli kabisa.. @Salehe Msanda na Kaka S.

ray njau said...

KIELELEZO KWA WAUME

5 Biblia inasema kwamba waume wanapaswa kuwatendea wake zao jinsi Yesu alivyowatendea wanafunzi wake. Fikiria mwongozo huu wa Biblia: “Waume, endeleeni kuwapenda wake zenu, kama vile Kristo pia alivyolipenda kutaniko na kujitoa mwenyewe kwa ajili yake . . . Vivyo hivyo, waume wanapaswa kuwa wakiwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Yeye anayempenda mke wake anajipenda mwenyewe, kwa maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake kwa vyovyote; bali huulisha na kuutunza kwa upendo, kama vile Kristo pia anavyolitendea kutaniko.”—Waefeso 5:23, 25-29.



9 Mtume Paulo alizungumzia ‘upendo mwororo alio nao Kristo Yesu.’ (Wafilipi 1:8) Wororo wa Yesu ulikuwa sifa yenye kuburudisha, iliyowavutia wanawake ambao walikuwa wanafunzi wake. (Yohana 20:1, 11-13, 16) Nao wake hutamani sana waume zao wawapende kwa wororo.
KIELELEZO KWA WAKE

10 Familia ni kama shirika, na ili lifanye kazi vizuri, linahitaji kuwa na kichwa. Hata Yesu anajitiisha kwa Yule aliye Kichwa chake. “Kichwa cha Kristo ni Mungu” kama vile “kichwa cha mwanamke ni mwanamume.” (1 Wakorintho 11:3) Kujitiisha kwa Yesu chini ya ukichwa wa Mungu ni mfano mzuri kwa kuwa sote tuna kichwa ambaye tunapaswa kujitiisha kwake.

11 Wanaume wasio wakamilifu hufanya makosa na mara nyingi wao hupungukiwa katika jukumu lao la kuwa vichwa vya familia. Kwa hiyo, mke anapaswa kufanya nini? Hapaswi kudharau mambo ambayo mume wake anafanya au kujaribu kumnyang’anya ukichwa. Mke anapaswa kukumbuka kwamba roho ya utulivu na upole ina thamani kubwa machoni pa Mungu. (1 Petro 3:4) Akiwa na roho hiyo, itakuwa rahisi kwake kuonyesha utii wa kimungu hata katika hali ngumu. Isitoshe, Biblia inasema: “Mke anapaswa kumheshimu sana mume wake.” (Waefeso 5:33) Lakini vipi akikataa kujitiisha chini ya Kristo akiwa Kichwa chake? Biblia inawasihi wake hivi: “Jitiisheni kwa waume zenu wenyewe, ili, ikiwa wowote si watiifu kwa lile neno, wavutwe bila neno kupitia mwenendo wa wake zao, kwa sababu wamekwisha kushuhudia kwa macho mwenendo wenu ulio safi kiadili pamoja na heshima kubwa.”—1 Petro 3:1, 2.


12 Mume awe ni mwamini au la, mke hatakuwa akimvunjia heshima ikiwa ataeleza maoni yake kwa njia ya busara hata kama yanatofautiana na ya mume. Huenda maoni yake yakawa sawa, na yanaweza kufaidi familia nzima ikiwa mume atamsikiliza. Ingawa Abrahamu hakukubaliana na mke wake Sara alipopendekeza jinsi ya kutatua tatizo fulani la familia, Mungu alimwambia: “Sikiliza sauti yake.” (Mwanzo 21:9-12) Bila shaka, mume anapofanya uamuzi ambao haupingani na sheria ya Mungu, mke wake anapaswa kuonyesha anajitiisha kwake kwa kuunga mkono uamuzi huo.—Matendo 5:29; Waefeso 5:24.

13 Mke anaweza kutimiza jukumu lake kwa kutunza familia. Kwa mfano, Biblia inaonyesha kwamba wanawake ambao wameolewa wanapaswa ‘kuwapenda waume zao, kuwapenda watoto wao, kuwa na utimamu wa akili, safi kiadili, wafanyakazi nyumbani, wema, wakijitiisha kwa waume zao wenyewe.’ (Tito 2:4, 5) Mke ambaye pia ni mama anayefanya hivyo, atapendwa na kuheshimiwa daima na familia yake. (Methali 31:10, 28) Lakini kwa kuwa ndoa ni muungano wa watu wasio wakamilifu, huenda hali fulani wasizoweza kuvumilia zikawafanya watengane au kutalikiana. Biblia inaruhusu kutengana hali fulani zinapotokea. Hata hivyo, kutengana hakupaswi kuchukuliwa kivivi hivi tu, kwa kuwa Biblia inashauri: “Mke hapaswi kuondoka kwa mume wake; . . . na mume hapaswi kumwacha mke wake.” (1 Wakorintho 7:10, 11) Msingi pekee wa Kimaandiko wa talaka ni uasherati.—Mathayo 19:9.