Wednesday, October 5, 2011

Muhimbili, Prof. Masangu Matondo, Mubelwa Bandio, Yasinta Ngonyani, Simon Kitururu...

Kama kawaida KIPENGELE CHETU CHA MARUDIO YA MATUKIO, MADA/MAKALA PICHA NK KITUJIACHO SIKU HII YA JUMATANO. NA LEO KINATUKUMBUSHA MAKALA HII AMBAYO INATOKA KWA DA`YETU SUBI.

Juzi kaka mdogo Mubelwa Bandio aliandika habari ya kumshukuru Dk. A. Kinasha na wengine wote katika hospitali ya Muhimbili na kwingineko ambao walishughulikia suala la afya yake iliyokuwa halijojo hadi kupata ahueni.

Ni mara ya tatu sasa ninasoma mrejesho wa waliopatiwa huduma katika sekta ya afya kwa njia ya blogu. Kwanza nilisoma kutoka kwa Prof. Matondo na pili ikawa ile ya dada Yasinta akisimulia na kushukuru kuhusu mdogowe Asifiwe. Napenda kuamini kuwa wapo watu wengine wengi tu waliofanya hivi kwa njia mbalimbali ikiwemo ya barua, maneno ya mdomo, kupiga simu, kwenye redio, televisheni na hata kuandika magazetini na kwenye vijarida kadha wa kadha.

--------------------------------------------------------------------------------
Yasinta Ngonyani Ninaafiki kuwa si watu wote wanaweza kuwa wamezisoma (kama ilivyo habari za kwenye blogu na tovuti, si wote wanaozipata). Lakini faida ya kuandika mrejesho kwa huduma alizopewa mtu zina umuhimu wa hali ya juu kwa wale wote wanaojali na kuzingatia maana na dhana ya neno 'huduma' na katika hilo nikimulikia sekta ya Afya ambayo imekuwa mojawapo ya sekta zinazolalamikwa sana, niliziandika katika posti iliyopita (unaweza kubofya hapa kuirejea).

Kilichonigusa katika posti ya Mubelwa, si tu maandishi yake ambayo niliyapeleka kunako jiko, bali pia maoni yaliyotolewa na wadau, mosi kutoka kwa Kaka Simon Kitururu na pili toka kwa Kaka Prof. Matondo.


--------------------------------------------------------------------------------
Kwa mfano, katika sehemu ya maoni yake, Simon anaandika, "...Huwa unanifanya nifikirie ni WANGAPI maishani mwangu ambao sijawashukuru na WASTAILIO shukurani za DHATI ."
Maneno haya ni kama vile Simon aliyasema kwa niaba yangu (na pengine wengi) kwamba katika kusoma habari za watu wengine, je, tunapata kujifunza kutokana na maneno yao? Kama kuna jambo la pekee sana kutoka kwa Mubelwa ambalo mtu aweza kujifunza, basi ni utamaduni wa KUSHUKURU na kusema ASANTE. Kwa hili Mubelwa ameendelea kunikumbusha tena na tena. Nami kwa sina budi kusema Asante Mubelwa kwa kunikumbusha kushukuru.


--------------------------------------------------------------------------------
Mfano mwingine ni maoni ya kaka Matondo, ambapo sehemu katika maoni yake kwenye posti hii anauliza, 'Hivi madaktari bingwa kama hawa wakistaafu wanakwenda wapi?..." na kisha anamalizia, '...Ningekuwa "serikali", ningewapa kila kitu wanachohitaji na kuwaomba wabakie kazini mpaka umri utakapowaamuru kuacha." na hapa ndipo aliponikumbusha juu ya maisha ya wasomi na wastaafu wetu. Ananikumbusha habari niliyowahi kuisoma katika jarida pepe la IRINnews.org (TANZANIA: Pensioners step in to plug medical gaps) kuhusu baadhi ya wastaafu hawa katika sekta ya Afya nchini Tanzania.
Kisha, upo mjadala uliowahi kujadiliwa na redio ya BBC katika kipindi chake cha Africa Have Your Say (bofya hapa kusikiliza) ambako nako walisikika wastaafu na wasio wastaafu wakizungumza kuhusu faida ama/na hasara ya kuendelea kuwa na watu wa umri ambao unadhaniwa kuwa ni wa kustaafu, wakiendelea kushika nafasi zao za kazi kadiri ya uhitaji si wao binafsi tu, bali kwa taifa lao pia.



Kuna jambo ambalo umewahi kufanyiwa na kuridhika hata ukatamani urejeshe shukrani? Fanya hivyo.

Je, lipo jambo ambalo umewahi kufanyiwa likakuudhi na ukakereka sana hata ukatamani utoe dukuduku ambayo itaonya na kusababisha wahusika wajirekebishe? Liseme.

Hii ni karne ya TEKNOHAMA, wakati muafaka kutumia teknolojia ya habari na mawasiliano kusema ili usikike.

Elimu, Maarifa, Wajibu, Shukrani... katika maisha ya Mwanadamu.

Tuambizane. Tusemezane.

3 comments:

Simon Kitururu said...

Mmmmh!

obat vimax said...

vimax thanks gan infonya vimax asli di tunggu info selanjutnya gan obat klg

cytotec said...

obat telat bulan i think your blog very informative obat penggugur thanks for sharing obat cytotec