Thursday, September 6, 2012

NILIPOFIKA KWENYE KIWANDA/MASHINE YA KUKOBOA MPUNGA NA KUPATA MCHELE AMBAO NI BORA TANZANIA/KYELA!!!

 Mpunga umeanikwa ili ukobolewa na baadaye kuwa mchele. Nilifika hapa "kiwandani na nikapata mfuko mzima wa mchele. Ambao inasemekana ni mchele bora kwa Tanzania yaani hapa Kyela.....

...Hilo jengo ndimo kazi ya kukoboa inamofanyika.Nilisahau kweli kuwauliza haya madawati ni kwa ajili ya nini?..Nilifurahi sana kufika Kyela kwa mara ya kwanza na kuupata mchele bora wa Kyela. Nadhani wengi mnajua hili kuwa mchele wao ni mzuri, unanukia na mtamu sana. Au je kuna mchele unaweza kuushinda huu?

5 comments:

ray njau said...

Je, Sikuzote Dunia Itazaa Chakula cha Kutosha ili Kuendeleza Uhai?
================================
▪ Sayari yetu maridadi, Dunia, ina uwezo mkubwa sana wa kuendeleza uhai. Hata hivyo, kwa sababu ya idadi inayoongezeka ya watu duniani na kwa sababu mali za asili zinapungua haraka sana, huenda ukajiuliza hivi: ‘Je, jambo ambalo tunaogopa sana linaweza kutukia? Je, sikuzote kutakuwa na chakula cha kutosha na mali za asili za dunia?’

Tukifikiria swali hilo, tunaweza kupata uhakikisho kutokana na ahadi hii ambayo Mungu aliwapa wanadamu miaka zaidi ya 4,000 iliyopita: “Siku zote ambazo dunia inaendelea kuwapo, kupanda mbegu na kuvuna, baridi na joto, majira ya kiangazi na majira ya baridi kali, mchana na usiku, havitakoma kamwe.” (Mwanzo 8:22) Hivyo, kama vile tu tulivyo na hakika kwamba jua litaangaza kila siku, tunaweza kuwa na hakika kwamba dunia haitaacha kamwe kuzaa chakula kinachohitajiwa ili kuendeleza uhai.

Katika ripoti iliyotolewa mwaka wa 2004 yenye kichwa “Je, Sayari Hii Inaweza Kutulisha?” Alex Kirby, mwandishi wa habari za mazingira, alisema hivi: “Dunia inazaa chakula cha kumtosha kila mtu. Lakini mara nyingi chakula hicho kiko mahali pasipofaa, au kinauzwa kwa bei ya juu, au hakiwezi kuhifadhiwa kwa muda mrefu. Hivyo, ni daraka la wanasiasa kuhakikisha kwamba kila mtu ana chakula cha kutosha, bali si sayansi.” Dunia ikisimamiwa vizuri na mali zake za asili kutumiwa ifaavyo, hatutakuwa na sababu ya kuogopa kwamba kutakuwa na upungufu wa chakula. Kwa mfano, wakati wa Waisraeli wa kale, Mungu alitoa mwongozo ulio wazi kuhusu matumizi mazuri ya ardhi. Kama ilivyorekodiwa katika Mambo ya Walawi 25:4, Mungu aliwaambia hivi Waisraeli: “Katika mwaka wa saba kutakuwa na sabato ya pumziko kamili kwa ajili ya nchi . . . Shamba lako hutalipanda mbegu.” Ingawa hawakupaswa kulima mashamba yao kila mwaka wa saba, Mungu aliahidi kwamba angehakikisha watu wangefurahia kuwa na vitu vingi na hawangekuwa na wasiwasi wa kukosa chakula.—Mambo ya Walawi 26:3-5.

Hata ingawa jitihada zinazofaa zinafanywa leo ili kuzuia uharibifu wa dunia na mali zake za asili, watu wengi wanahisi kwamba jitihada hizo hazitoshi, au zimechelewa sana. Suluhisho pekee la kudumu linapatikana katika Ufunuo 11:18. Katika andiko hilo, Biblia inasema kwamba Yehova ‘atawaharibu wale wanaoiharibu dunia.’ Yehova hatawakomesha tu wale wanaoiharibu dunia na mali zake za asili, bali pia atahakikisha kwamba dunia inazaa chakula kingi kwa ajili ya wakaaji wake wote. Watu wote wanaokaidi kusudi la Mungu na wote wanaoharibu dunia ili kupata faida watakomeshwa kabisa. Hata hivyo, wote wanaounga mkono utawala wa Yehova kwa kupenda, wataona maneno haya ya Zaburi 72:16 yakitimizwa: “Kutakuwa na wingi wa nafaka duniani; juu ya milima kutakuwa na mafuriko.”

Akichochewa na upendo na hekima yake nyingi, Yehova anakusudia wanadamu waishi na kutunza makao yao, dunia iliyo paradiso. (Mwanzo 1:28) Chini ya utawala wake, wanadamu watiifu watajifunza kutumia kwa hekima mali za asili, bila kuharibu hazina hizo kubwa. Tunashukuru kama nini kwa sababu ya Mwandalizi huyo mwenye upendo ambaye atatosheleza tamaa ya kila kitu kilicho hai!—Zaburi 145:16.

Yasinta Ngonyani said...

Chakula kinaweza kutosha kama wanadamu watazalisha. Ila tusipojishughulisha kuzalisha chakula na kuendelea kuzaa tu hakika chakula hakitatosha...

ray njau said...

@Yasinta;
Hongera sana kwa madokezo maridhawa yaliyohanikizwa na ujasiri.
===============================

"Ila tusipojishughulisha kuzalisha chakula na kuendelea kuzaa tu hakika chakula hakitatosha..."

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Ray! Ahsante kwa kwa yote. na zaidi kwa ushirikiano wako..

ray njau said...

@Yasinta;
Maisha na mafanikio ni kibaraza chema sana na mwenye kiu ya kuchangia mada bila kuchafua hali ya hewa ni ruksa!!