Monday, September 24, 2012

HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA JUMAPILI YANGU YA 24/92012:- ILIKUWA JUMAPILI NJEMA SANA ....

Jumapili ya jana ilikuwa sio kama jumapili nyingine. Jumapili hii kulikuwa na ugeni kutoka Tanzania Huyo  baba mwenye suti nyeusi ni baba askofu na anatokea njombe ila anafanya kazi Dodoma na mwenye nguo za kijiani kijana ni mke wake halafu walikuwa wakaka watatu ambao ni wamasai...Kama kawaida Kapulya hakukosa kuuliza maswali hapa nilijikuta nipo nyumbani kabisa kuonana na waTanzania wenzangu na kuongea kiswahili kwa raha zote pia kibene. Majina yao nimesahau kidogo...

Hapa hadithi zimekolea na wote tupo ndani ya kicheko  kama muonavyo....

 Ndani ya kanisa

10 comments:

sam mbogo said...

inapendeza na kuvutia unapokutana na watu kutoka bongo. kaka s

MARKUS MPANGALA said...

Aaaah mambo yalikuwa matamu kweli maana kuna pozi moja la kushika mkono kiunoni mie hoiiiiiii kwa kichekoooo. Lol

simbadeo said...

Safi sana. Nimependa jinsi Watanzania hao walivyofurahi na kupata bahati ya pekee kukutana na wewe. Naamini hapo Kapulya alikuwa Kapulya kwelikweli ... maana Mjukuu huyu wa Shaka Zulu ni hodari wa masimulizi ... Hongereni sana.

Mija Shija Sayi said...

Kwa muda mfupi mtu unajiona uko kwenu..

Safi sana yaani..

Penina Simon said...

duh hadi raha, bigup mdada,

Interestedtips said...

duh, raha sana, nahisi ulifurahi kupita maelezo, safi sana

Yasinta Ngonyani said...

Nachukua nafasi hii na kuwashukuruni wote kwa kuwa nami. Hakika jumapili hii itakuwa ambayo kati ya zile ambazo sitazisahau MISA YA KISWAHILI hakuna raha kama hiyo. Nilifurahi sana na wao walifurahi sana kama muonavyo katika picha.

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

safi hiyo aisee

roberto vumo said...

Nimefurahi kuiona hiyo picha ya pili! Mhhhhhh!



Roberto VUMO said...

Nimefurahi kuiona hiyo picha ya pili! Mhhhhhh! Hiyo picha umeshika kiuno, natamani nami ningekishika!