Tuesday, September 4, 2012

ELIMU :- KISOMO CHA WATU WAZIMA!!!

Elimu haina mwisho hapa akina mama wapo darasani kwa ajili ya kupata ELIMU..angalao kuweza kuandika tu..Inafurahisha kuona walezi wetu wana moyo wa kutaka kupata elimu. Ila nimejiuliza hivi hili darasa ni kwa ajili ya akina mama tu? Maana sioni akina baba hapa.

5 comments:

ray njau said...

Mke mwenye uwezo ni taji kwa mume wake, lakini yule anayetenda kwa aibu ni kama ubovu kwenye mifupa ya mume wake._Methali 12:4

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Ray! Ahsante kwa neno..

Rachel Siwa said...

Asanteni Wapendwaaa kaka Ray kwa Neno.

Kadala kwa mada hii!!!MUNGU awenanyi daima.............

Yasinta Ngonyani said...

Kachiki! tupo pamoja ndugu wangu..na pia MUNGU awe nanyi pia hapo katika kaya.

Penina Simon said...

imenikumbusha enzi za mwalimu, bibi yangu alikuwa anajificha akija mjumbe kuwataka waende shule (ngumbaru).
nadhani hiyo sasa hvi haipo, ila ilikuwa safi sana.