Thursday, March 29, 2012

POROJO YA LEO !!!

Bwana mmoja karudi nyumbani toka kazini amechoka ile mbaya, akaingia ndani na kujitupa kochini ili aangalie TV. Akamwambia mkewe:-
- Niletee bia, karibu inaanza .
-Mkewe akapumua na akampa bia.
- Baada ya dakika kumi na tano akasema :-
-Nipe bia nyingie maana karibu inaanza.
Mke wake akamwangalia kwa kuchoka choka lakini akampa bia nyingine:
Alipokuwa amemaliza ile bia baada ya dakika kadha akasema:-
- Nipe bia nyingie, kwani itaanza dakika yoyote ile.
-Mkewe akachukia na kumpigia kelele, akasema.
- Yaani huna kazi nyingine ya kufanya jioni hii, zaidi ya kukaa na kuangalia TV na kunywa bia?
Wewe huna lolote isipokuwa ni mvivu, mwanaharamu mkubwa.......
Yule bwana akapumua na kusema:-
-Sasa imeanza.......
Je wewe pia unajiuliza kama mimi ni nini kilichoanza?

5 comments:

ray njau said...

Hata mimi najiuliza ni nini hiyo?

Rachel Siwa said...

Kasheshe/Ugomvi!!!!Tehtehtehte nimejaribu.

o'Wambura Ng'wanambiti! said...

kelele!!!!

Yasinta Ngonyani said...

Mimi nahisi mpira!!

Seleman Awadh said...

Niseme labda ilikuwa inaanza move au mechi ya mpira wa miguu kwa kuwa alikuwa anaangalia TV.