Saturday, June 8, 2013

KILIMANJARO IONEKANAVYO TOKA ANGANI PICHA KAKA ERIK 2013 JANUARI

 mlima wetu Kilimanjaro
Hakika unapendeza na tuna haki ya kuutangaza mlima wetu Kilimanjaro...
nawatakieni wote JUMAMOSI NJEMA. UJUMBE WA LEO:- Vitu muhimu katika maisha sio vitu.

2 comments:

ray njau said...



UNAPOTAJA JINA KILIMANJARO KWA HAKIKA UNATAJA TANZANIA KUTOKANA NA UMAARUFU WA MLIMA KILIMANJARO AMBAO NI MAARUFU KULIKO YOTE AFRIKA.NGOMA KUBWA YA ASILI YA WACHAGGA NI IRINGI. IRINGI HUCHEZWA KATIKA MDUARA HUKU WATU WAKIWA WAMESHIKANA MIKONO IKIWA NI ALAMA YA UPENDO NA MSHIKAMANO WA KIFAMILIA .ZAO KUU LA BIASHARA NA UCHUMI KWA WACHAGGA NI KAHAWA CHINI YA CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA [KNCU].WACHAGGA WANAISHI KWENYE WILAYA NNE ZA MKOA WA KILIMANJARO AMBAZO NI SIHA;HAI;MOSHI NA ROMBO KWA MPANGILIO UFUATAO:

---------------------------------------------------------------------------------------------------------

1.WASIHA

2.WAMACHAME [ WILAYA YA SIHA NA HAI]

3.WAMASAMA

--------------------------------------------------------------------------------------------------------

4.WAKINDI

5.WAKIBOSHO

6.WAURU

7.WAOLDMOSHI

8.WAMBOKOMU [ WILAYA YA MOSHI ]

9.WAKIRUA

10.WAKILEMA

11.WAMARANGU

12.WAMAMBA

13.WAMWIKA

---------------------------------------------------------------------------------------------------------

14.WAKENI

15.WAMKUU

16.WAMASHATI [ WILAYA YA ROMBO ]

17.WASSERI

18.WANGASA

---------------------------------------------------------------------------------------------------------



WAKAMBA WALIUITA MLIMA HUU "KIMA JA JEU[MLIMA MWEUPE];WAMASAI WALIUITA"OL DONYO EIBOR"[MLIMA MWEUPE];WATAITA WALIUITA NJARO[KILIMA CHA MUNGU];WACHAGGA WALIUITA KIPOO[KIBO] AU KILIMA CHA NJARO [KILIMA CHA MUNGU]

Justin Kasyome said...

kweli vitu muhimu sio vitu!haaaa!haaa!haya nawe pia jumamosi njema ila tunastahili kunivunia mlima Kilimanjaro maana haupo kwingine duniani,japo wewe unasema vitu muhimu maisha sio vitu,ila mlima Kilimanjaro ni kitu buana!