Thursday, August 9, 2012

Raymond Mkandawile na Bibie Janeth Manongi tulifunga pingu za maisha!!!


Hello ndugu,mimi ni mdau na mmiliki wa mtandao wa mkandawilejr.blogspot.com
tafadhali naomba niwekee taswira hizi za siku ya harusi yangu.
Hapo juu ni taswira mbalimbali za siku hiyo ya kihistoria ya tarehe 4/08/2012ambapo mimi Raymond Mkandawile na Bibie Janeth Manongi tulifunga pingu za maisha  huko jijini mbeya katika kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania usharika wa Sinai na kufuatiwa na sherehe iliyofanyika katika ukumbi wa chuo cha Teku uliyopo maeneo ya Block T.
Natanguliza shukrani zangu kwa ushirikiano wenu.
Mr. Raymond Mkandawile
BA (HON) in Business Studies
University of Wales Institute of Cardiff(UK)
Mob; +255656-561-314
Email; raymonds19@yahoo.com
Website;http://www.mkandawilejr.com




Maharusi wakiteta jambo baada ya kunganishwa na kuwa mwili mmoja

Bwana na bibi Harusi wakiwa nanyuso za furaha...
Blog ya Maisha na Mafanikio inapenda kuwatakieni maisha mema ya NDOA na pia kuwakaribisheni katika maisha haya ya Ndoa. Ambayo yanahitaji UVIMILIVU NA USIKIVU PIA MAWASILIANO. MAISHA MEMA/HONGERENI SANA.



1 comment:

ray njau said...

UNAWEZA KUFANYA NINI ILI NDOA IDUMU?
==============================
Ikiwa wenzi wanataka ndoa yao idumu, wanapaswa kuwa na maoni yanayofaa kuhusu uwajibikaji. Mara nyingi sinema na vitabu vya hadithi huisha watu wawili wanaopendana wakifunga ndoa na kuishi raha mustarehe, maisha ambayo wengi hutamani sana. Lakini, katika maisha halisi, ndoa si mwisho bali ni mwanzo—mwanzo wa kitu ambacho Yehova alitaka kidumu. (Mwanzo 2:24)) Kwa kusikitisha, watu wengi ulimwenguni leo hawana maoni hayo. Watu fulani hulinganisha kufunga ndoa na “kufunga pingu za.” Huenda wasitambue jinsi hilo linavyofafanua vizuri maoni ya wengi leo kuhusu ndoa. Namna gani? Ingawa pingu zinaweza kufunga kitu kwa nguvu kwa muda unaohitajika, zinaweza pia kufunguliwa kwa urahisi.
Wengi leo huona ndoa kuwa ya muda tu. Wanaingia katika ndoa haraka-haraka kwa kuwa wanafikiri itatosheleza mahitaji yao, lakini wanatazamia kwamba watatoka kwa urahisi mambo yakichacha. Hata hivyo, kumbuka kwamba Biblia inapozungumzia kifungo, kama vile kifungo cha ndoa, inatumia mfano wa kamba. Kamba za meli hukusudiwa kudumu, zisikatike-katike wala kufumuka hata kunapokuwa na dhoruba kali sana. Vivyo hivyo, ndoa imekusudiwa kudumu. Kumbuka kwamba Yesu alisema: “Kile ambacho Mungu ameunganisha mtu yeyote asikitenganishe.” (Mathayo 19:6) Ukifunga ndoa, unapaswa kuwa na maoni hayohayo kuhusu ndoa. Je, uwajibikaji wa aina hiyo huifanya ndoa iwe mzigo? Hapana.
Kila mmoja anapaswa kuendelea kuwa na maoni yanayofaa kuhusu mwenzi wake wa ndoa. Kila mmoja wao akifanya yote awezayo kukazia fikira sifa nzuri na bidii ya mwenzake, ndoa hiyo itakuwa yenye furaha na yenye kuburudisha. Je, kuwa na maoni yanayofaa kuhusu mwenzi asiye mkamilifu ni kujifanya kipofu? Yehova hawezi kamwe kuwa kipofu, hata hivyo, sisi hutazamia awe na maoni yanayofaa kutuelekea. Mtunga-zaburi alisema: “Kama ungekuwa unaangalia makosa, Ee Yah, Ee Yehova, ni nani angesimama?” (Zaburi 130:3) Waume na wake pia wanapaswa kuwa na maoni yanayofaa na kuwa tayari kuwasamehe wenzi wao wa ndoa.—Wakolosai 3:13
Kadiri miaka inavyopita, ndoa inaweza kuwa baraka hata zaidi. Biblia inazungumzia ndoa ya Abrahamu na Sara walipokuwa wazee. Bila shaka maisha yao yalikuwa na mabonde na milima. Wazia hali ya Sara. Huenda alikuwa na umri wa miaka 60 na kitu alipoondoka makao yake yenye starehe katika jiji lenye ufanisi la Uru na kwenda kuishi katika mahema maisha yake yote. Hata hivyo, alijitiisha chini ya ukichwa wa mume wake. Alikuwa kikamilisho na msaidizi kwelikweli kwa Abrahamu, na kwa heshima alimsaidia kufanikisha maamuzi yake. Ujitiisho wake haukuwa wa kijuujuu. Hata “ndani yake mwenyewe,” alimwita mume wake bwana. (Mwanzo 18:12; 1 Petro 3:6) Alimheshimu Abrahamu kutoka moyoni.
Bila shaka, hilo halimaanishi kwamba Abrahamu na Sara walikubaliana katika kila jambo. Siku moja alitoa pendekezo ambalo “halikumpendeza Abrahamu hata kidogo.” Lakini Abrahamu alitii maagizo ya Yehova, na kwa unyenyekevu akaisikiliza sauti ya mke wake, nayo familia yao ikabarikiwa. (Mwanzo 21:9-13) Waume na wake leo, hata wale ambao wamekuwa katika kifungo cha ndoa kwa miaka mingi, wanaweza kujifunza mengi kutokana na wenzi hao wenye kumwogopa Mungu.