Tuesday, August 7, 2012

FILAMU YA WRONG LANE KUWA MTAANI WAKATI WOWOTE KUANZIA SASA! Read more: FILAMU YA WRONG LANE KUWA MTAANI WAKATI WOWOTE KUANZIA SASA!



RASTEMWI PRODUCTIONS yenye makao yake jijini Dar es Salaam itaingiza sokoni filamu yake mpya inayoenda kwa jina la wrong LANE ‘njia POTOFU’ wakati wowote kuanzia sasa.

Akiongea na WAVUTI.COM, mkurugenzi mtendaji wa RASTEMWI PRODUCTIONS, Dr. Rama Mwiru, amesema filamu hiyo imeshirikisha wacheza filamu nyota wa Tanzania kama Miriam Jolwa ‘jini kabula’, Rose Michael ‘zambarau’, Gilbert Sindani ‘mack’, Ibrahim Banane ‘mzee katembo’, na Kulwa Kikumba ‘dude aka dr lugusha’. Ma-star wengine walioshiriki kwenye wrong LANE ni pamoja na Salma Jabu ‘Nisha’, Mariam Mndeme, Kojack Chillo, Michael Philipo ‘kojack’, Alice Bagenzi ‘rayuu’, Mustafa Matambo na mwanamuziki maarufu wa zouk Rehema Tajiri.

Filamu ya wrong LANE pia inaingia sokoni ikiwa imeshirikisha wacheza filamu wapya na wenye vipaji vya hali ya juu kama Salma Tuesday ‘salma chuzi’ ambaye ni mtoto wa ma-supa stars wa bongo movie, Mr. Chuzi na Kabula. Wengine wageni lakini wenye vipaji vya hali ya juu ni Dhahabu Francis, Johnson George ‘john cena’, Salvina Stambuli, Mohamedy Ally, Fadhil, na Dr. Rama mwenyewe.

Dr. Rama amesema wrong LANE imelenga kuwaburudisha na kuwapa mafunzo mbalimbali ya kimaisha watanzania na watu wengine wanaopenda filamu.

No comments: