Thursday, August 16, 2012

HII KALI NAONA IWE PICHA YA MWAKA:- MWANAUME AFUNGA NDOA KANISANI NA WANAWAKE WATATU KWA SIKU MOJA!!!

Sijawahi kuona wala kusikia tukio kama hili kaaazi kwelikweli..na tena ni mpya. Mwanamke mmoja tu kazi kwelikweli je watatu na tena kwa mpigo. Nimeshindwa kuvumilia kushangaa peke yangu nimeona niwashirikishe na wenzangu.  

10 comments:

ray njau said...

Asante kwa taswira hii da'Yasinta.Ijapokuwa ndoa ni jambo la kibnafsi lakini hapa naona ile maana ya ndoa haipo tena bali ni maisha shaghalabagala.

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Ray! au yeyote yule je hapo yupi ni mke mkubwa na yupi wa ili na yupi wa tatu? au wote wa kwanza? na swali jingine kwa kawaida mke husimama upende wa kulia wa mume wake katika siku hii sasa hapa wawili wamesimama upande wa kukushoto na mmoja kulia je hapa inakuwaje?

ray njau said...

@Yasinta;
Nimesema kuwa ndoa ni jambo la kibnafsi katika maana hii:
Mipango yote ya ndoa ni siri ya wanandoa wenyewe na hakuna mwenye utambuzi katika hilo.Mke mkubwa na mdogo wanajuana wenyewe katika mipango yao na kwa nini wamekaa wamejipanga hivyo wanajua.Na ukiwa na hisia kuwa aliyekaa kulia ndiyo mkubwa na wengine ndiyo wake wenza inawezekana pia.Lakini mpango mzima wa tukio na picha hii ni siri ya wahusika na wasaidizi wao.Kwa ujumla ile maana ya ndoa hapa haipo.

EDNA said...

Duuuh! dunia ina mambo.

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Ray nimekupata ahsante sana kwa ufafanuzi..
Edna! Yaani si utani duniani kuna majimambo..nimejaribu kujiuliza mwenyewe hapa hivi kwa nini wamevaa hiyo kofia/shara tofauti tafauti? Na si ilimgharimu sana hayo magauni? Sijui aliona tu ni bora amalize mkataba kufunga ndoa na wote watatu..ngoje niachie hapa...

Anonymous said...

Haya jamani tusishangae sana kama ni kweli ni ndoa za kanisani tujue kuwa hizi ni dini za watu binafsi vikundi vya watu vinaanzisha dini kwa matakwa yao binafsi sio katik IMANI TULIZOZIZOEA NA KURITHI KUTOKA KATIKA VIZAZI VYETU VILIVYOTUTANGULULIA heee jamani mbona ni kituko cha karne na kila nikiwaza hata sipati jibu kwa kweli haya dada Nanganyani- nabambu mbawala

Penina Simon said...

Mimi binafsi sidhani kama kweli hawa wanawake wana akili timamu + huyo mume wao na huyo anaewafungisha ndoa,
nway Mungu atusaidie tuwe waelewa wa maana halisi ya ndoa na kuiheshimu kama kitu kitakatifu kilichobarikiwa na Mungu.



Anonymous said...

ray wala sio shagabala hii ni safi inatakiwa wanaume wote tuoe hata zaidi ya saba maana sasahivi unawaona akina dada mpaka zinaa barabarani hivyo nibora kuwachukua ukakaa nao wote na kuwasitiri,kwani wengine ukioa mmoja bado unamwacha unawafuata hao wa barabarani kwahiyo ni bora ukawa nao nyumbani maana mwanamme ni mfalume na hao ni malikia wake hicho nikidume cha mbegu yaani dume la mbegu safi nimeipenda hiyo

emuthree said...

Kubana matumizi, maana gharama ya harusi ya kuoana wake watatu, tofauti tofauti sio mchezo!

Anonymous said...

Pesa ndo inaongea