Tuesday, August 21, 2012

CHAKULA CHA ASUBUHI YA LEO..DADA PENINA UPOOOO??? KARIBU PIA NA WENGINE WOTE...!!!

Haya ni maoni ya Dada Penila Simon kutoka katika picha hii hapa."Hongera, jitihada zako nimeziona, nakupenda ulivyo na pia, the way ulivyo busy na pia husahau asili. i real loe u baby.
Napenda na naomba unionjeshe kidogo picha baada ya kulipika lilisindikizwa na nini na lilikaaje mezani plz..." Nami nimeona si vibaya kama nikifanya kama dada P alivyoniomba hivi ndivyo mambo yalivyokuwa dada P, pamoja na wengine wote..fuatana nami.....

 Nimeamka asubuhi. Nimeingia katika shambani/bustani yangu na  kuchuma boga..kama nilivyowaambia hapo juzi na ....hivi ndivyo ilivyokuwa....boga
Nimechemsha na halafu tayari kwa Chakula cha asubuhi. Yaani boga kwa chai ya rangi. Kwa mimi chai yangu kama kawaida bila sukari hapo nimelifaidi na kulamba mikono si mchezo..je wewe unapenda kula boga lako vipi? au unalitemshia na nani?....mmmhhh sijui mchana huu nipike/nile nini? Natamani.. naacha sisemi mtaona baadaye kidogo tu...:-)

4 comments:

Interestedtips said...

Kwakweli hayo mavuno yako na yadumu daima....maboga ni matamu sana, unakunywa na chai na uji linashuka vizuri, hata ukinywa na maji, lol. ume enjoy sanaaaaaa

Unknown said...

Duh hii kitu zamani nilikuwa siipendi bt nw naipenda hii chakula

Rehema said...

Wamdala veve hasa pa chani ukuniholosa mata namiyaku naha? Nene maboga nigagani sana,haya usengula baho.

emuthree said...

Safi sana, tunda hili, hivi hili ni tunda, au ni ...!