Monday, July 30, 2012

SIO LAZIMA UAMBIWE KWA MDOMO....

....hata kwenye kanga ni tosha kabisa...

4 comments:

Interestedtips said...

HUO UJUMBE WA KANGA NIMEUPENDA MNOOO

Rachel Siwa said...

Hahahahhaa da'Kadala hii kiboko!!

Yasinta Ngonyani said...

Ester nami nimeupenda kiasi kwamba nikaona nisiwe muchoyo...

Kachiki! Yaani haswaaa kiboko!!

ray njau said...

KIELELEZO KWA WAUME

5 Biblia inasema kwamba waume wanapaswa kuwatendea wake zao jinsi Yesu alivyowatendea wanafunzi wake. Fikiria mwongozo huu wa Biblia: “Waume, endeleeni kuwapenda wake zenu, kama vile Kristo pia alivyolipenda kutaniko na kujitoa mwenyewe kwa ajili yake . . . Vivyo hivyo, waume wanapaswa kuwa wakiwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Yeye anayempenda mke wake anajipenda mwenyewe, kwa maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake kwa vyovyote; bali huulisha na kuutunza kwa upendo, kama vile Kristo pia anavyolitendea kutaniko.”—Waefeso 5:23, 25-29.

6 Upendo wa Yesu kwa wanafunzi wake ni kielelezo bora kwa waume. Yesu ‘aliwapenda mpaka mwisho,’ akadhabihu uhai wake kwa ajili yao, hata ingawa hawakuwa wakamilifu. (Yohana 13:1; 15:13) Vivyo hivyo, waume wanahimizwa hivi: “Endeleeni kuwapenda wake zenu nanyi msiwakasirikie kwa uchungu.” (Wakolosai 3:19) Ni nini kitakachomsaidia mume kufuata shauri hilo, hasa ikiwa nyakati nyingine mke wake hatendi kwa busara? Anapaswa kukumbuka makosa yake na anachopaswa kufanya ili kupata msamaha wa Mungu. Anapaswa kufanya nini? Anapaswa kumsamehe kila mtu anayemkosea, kutia ndani mke wake. Bila shaka, mke anapaswa kufanya vivyo hivyo. (Mathayo 6:12, 14, 15) Je, unaona ni kwa nini watu fulani husema kwamba ili ndoa zifanikiwe lazima wenzi wote wawili wawe tayari kusameheana?

7 Waume wanapaswa kukumbuka pia kwamba sikuzote Yesu aliwajali wanafunzi wake. Alizingatia udhaifu wao na mahitaji yao ya kimwili. Kwa mfano, alisema hivi walipokuwa wamechoka: “Njooni, ninyi wenyewe, faraghani katika mahali pasipo na watu mpumzike kidogo.” (Marko 6:30-32) Wake pia wanastahili kuhangaikiwa kwa upendo. Biblia husema kwamba wao ni “chombo dhaifu zaidi” na waume wanaamriwa wawape “heshima.” Kwa nini? Kwa kuwa waume na wake pia wanashiriki “pendeleo lisilostahiliwa la uzima.” (1 Petro 3:7) Waume wanapaswa kukumbuka kwamba Mungu hupendezwa na uaminifu wa mtu wala si jinsia yake.—Zaburi 101:6.

8 Biblia inasema kwamba mume “anayempenda mke wake anajipenda mwenyewe.” Hiyo ni kwa sababu mume na mke “si wawili tena, bali mwili mmoja,” kama Yesu alivyosema. (Mathayo 19:6) Hivyo basi, hawapaswi kufanya ngono na mtu mwingine yeyote. (Methali 5:15-21; Waebrania 13:4) Wataepuka kufanya hivyo ikiwa kila mmoja anajali mahitaji ya yule mwingine bila ubinafsi. (1 Wakorintho 7:3-5) Kikumbusho hiki pia kinafaa: “Hakuna mtu anayeuchukia mwili wake kwa vyovyote; bali huulisha na kuutunza kwa upendo.” Waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama wanavyojipenda wenyewe, wakikumbuka kwamba watatoa hesabu kwa Yesu Kristo, aliye kichwa chao.—Waefeso 5:29; 1 Wakorintho 11:3.

9 Mtume Paulo alizungumzia ‘upendo mwororo alio nao Kristo Yesu.’ (Wafilipi 1:8) Wororo wa Yesu ulikuwa sifa yenye kuburudisha, iliyowavutia wanawake ambao walikuwa wanafunzi wake. (Yohana 20:1, 11-13, 16) Nao wake hutamani sana waume zao wawapende kwa wororo.