Tuesday, July 24, 2012

KUADIMIKA KWA MUDA!!! LIKIZO....

 Mmmmmhh! Ngoja kwanza nikune kichwa naona kama nimeishiwa cha kusema vile..ni hivi ni raha sana kuwa na ndugu marafiki na jamaa...lakini sasa umefika muda wa kuwa pamoja na familia...niwanongóneza ni kwamba nipo Likizo...
Ila nitajitahidi kuwa nanyi pia kinamna ili tusisauliana..ila mmmhhh kuwasahau ndugu si rahisi...hapa naona kama kapulya hana furaha:-( WOTE MNAPENDWA NA TUPO PAMOJA.  MMEONA ZAWADI YANGU YA HUO UTAMADUNI/KIMASAI:-)

13 comments:

Interestedtips said...

likizo njema dada..naamini utakuwa unakuja kutuchungulia huku mara kwa mara...salimia familia

Yasinta Ngonyani said...

Ester wala usikonde ...nipatapo kamuda nitafanya hivyo..AHSANTE:-)

ray njau said...

@Yasinta;
Hii ni hoja binafsi na kuipinga na kukiuka protokali.
Yaliyosema yamesikika,yaliyosikika yameeleweka na yaliyoeleweka yamehifadhiwa hadi wakati ufaao siku zijazo.
Hadi wakati ufaao siku zijazo asante sana na pumzika kwa raha na furaha.

Rachel Siwa said...

Uwe na wakati mwema kadala, MUNGU awenanyi daima!!!

nakuonea wivu mwayego!!!!!

sam mbogo said...

Yaani bonge la mapumziko safi sana kupumzika na familia muhimu. mimi pia kama sitaki vile ijumaa mungu akitujaalia mimi na kijana wangu tuko Bongo Dar naenda kupumzika dar,Tabora ,mpanda. wana blog wa dar nitawatafuta nikifika ila sijuwi kivipi ila nitajuwa tu nitawapata baadhi yenu. haya Da Yasinta faudu likizo!! kaka s

ISSACK CHE JIAH said...

Tunakutakia likizo njema usisahau kutuletea masuku ya kizungu kama huendi ntyangimbole au litumba ndyosi
kaka yako Che Jiah

EDWIN NDAKI (EDO) said...

endelea na mapumziko mazuri maana naonamajira ya kiangazi ndio yaanza kwi kwi maana huku finland unaweza kufikiri summer imeisha maana mvua jua mtindo mmoja jirani..siku njema
tutafika tu

nyahbingi worrior. said...

Huku nyumbani hatupumziki wala kulala.

Amani.

chib said...

Likizo njema!!

batamwa said...

haya mapumziko mema mimi nami nilikuwa likizo bukoba nimerudi dar lakini nikashikwa bonge la homa,ila hilo pambo la kimasai limekutoa kweli safi sana

emuthree said...

Likizo njema ndugu wangu,tupo pamoja

Simon Kitururu said...

Nadeku Picha. Mtoto Mzuri weye!

Shaziry Nambombe said...

HI! DADA ANGU POLE KWA KILA KITU AMBACHO UNAONA KINAKUPA SHIDA NA PONGEZI KWA KILA JAMBO JEMA UNALOLIFANYA NA KULIPATA . NAOMBA UNISAIDIE MAWASILIANO YAKO .