Saturday, April 21, 2012

JUMAMOSI NJEMA JAMANI!!! WANDUGU WANGU:)

Tazama  jinsi ilivyo veme, ndugu wakae pamoja kwa umoja Zab 133:1
Michezo huleta burudani na kujenga miili yetu. Itusaidie pia kuleta umoja na mshikamano kati yetu; badala ya sokomoko, chuki na fitina.

6 comments:

ray njau said...

Zaburi 133:1-3

Wimbo wa Mipando. Wa Daudi.

1 Tazama! Jinsi ilivyo vyema na jinsi inavyopendeza

Ndugu kukaa pamoja kwa umoja!

2 Ni kama mafuta mazuri juu ya kichwa,

Yanayoshuka juu ya ndevu,

Ndevu za Haruni,

Yanayoshuka kwenye ukosi wa mavazi yake.

3 Ni kama umande wa Hermoni

Unaoshuka kwenye milima ya Sayuni.

Kwa maana huko Yehova aliamuru baraka iwepo,

Naam, uzima mpaka wakati usio na kipimo.

Rachel Siwa said...

Ameeeeeen,Dadake iwe njema nanyi pia.

ray njau said...

Asante sana dada Yasinta kwa kunikumbusha maneno mazuri ya Zaburi ya 133:1-3.
Hakika ni zawadi njema sana ya kifamilia kwa wikiendi hii.Hii ni kitia moyo kwetu sote kuwa tusimezwe na mikikimikiki ya maisha na kusahau kabisa kusoma neno la Mungu biblia tukiwa mtu mmoja mmoja au kifamilia.
---------------------------------- SOMA NENO LA MUNGU BIBLIA KILA SIKU
-----------------------------------
IJUE BIBLIA YAKO
Biblia

KUNA vitabu 66 katika Biblia. Kila kitabu kina sura na mistari, ili kurahisisha usomaji. Maandiko yanapotajwa katika kitabu hiki, nambari inayofuata jina ndiyo sura ya kitabu au barua katika Biblia, nayo nambari inayofuata ni mstari. Kwa mfano, “2 Timotheo 3:16” ni barua ya pili kwa Timotheo, sura ya 3, mstari wa 16.

Ukifungua na kusoma maandiko yaliyo katika kitabu hiki, utazoea kuitumia Biblia. Pia, mbona usianze kuisoma Biblia kila siku? Ukisoma sura tatu hadi tano hivi kila siku, unaweza kuisoma Biblia nzima kwa mwaka mmoja.

ray njau said...

Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Je, Hivi Ndivyo Mungu Alivyokusudia?

SURA

Je, Hivi Ndivyo Mungu Alivyokusudia?

Ukweli Kumhusu Mungu
Biblia—Kitabu Kutoka kwa Mungu
Mungu Ana Kusudi Gani kwa Dunia?
Yesu Kristo Ni Nani?
Fidia—Zawadi Bora Zaidi Kutoka kwa Mungu
Wafu Wako Wapi?
Tumaini Hakika kwa Wapendwa Wako Ambao Wamekufa
Ufalme wa Mungu Ni Nini?
Je, Tunaishi Katika “Siku za Mwisho”?
Jinsi Viumbe wa Roho Wanavyohusika Maishani Mwetu
Kwa Nini Mungu Anawaacha Watu Wateseke?
Kuishi Maisha Yanayompendeza Mungu
Maoni ya Mungu Kuhusu Uhai
Jinsi ya Kufanya Maisha ya Familia Yako Yawe Yenye Furaha
Ibada Ambayo Mungu Anakubali
Chukua Msimamo Upande wa Ibada ya Kweli
Mkaribie Mungu Katika Sala
Ubatizo na Uhusiano Wako Pamoja na Mungu
Kaa Katika Upendo wa Mungu

Nyongeza

Chapa ukurasa huu Chapa ukurasa huu

KATIKA magazeti, televisheni, na redio, kuna habari nyingi kuhusu visa vya ugaidi, vita, na uhalifu. Hebu fikiria pia mahangaiko yako mwenyewe. Labda unasumbuliwa na ugonjwa fulani au umefiwa na mtu unayempenda. Huenda ukahisi kama alivyohisi Ayubu, aliyesema kwamba maisha yake yalikuwa ‘yamejaa masumbuko.’—Ayubu 10:15, Verbum Bible.

Hebu jiulize:

Je, hivi ndivyo Mungu alivyokusudia maisha yangu na ya wanadamu wengine yawe?
Ninaweza kupata wapi msaada wa kukabiliana na matatizo yangu?
Je, dunia itapata kuwa na amani?

Biblia inajibu maswali hayo kwa njia ya kuridhisha.
BIBLIA INAFUNDISHA KWAMBA MUNGU ATATIMIZA MAMBO HAYA DUNIANI.
Mtu aliyekuwa mzee awa kijana tena

“Atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.”—Ufunuo 21:4

Msichana aliyekuwa mlemavu aanza kukimbia tena

“Kilema atapanda juu kama vile paa anavyofanya.”—Isaya 35:6

Mtu aliyekuwa kipofu aanza kuona tena

“Macho ya vipofu yatafunguliwa.”—Isaya 35:5

Mwanamke akifurahia kumwona mpendwa wake aliyefufuliwa

‘Wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho watatoka.’ —Yohana 5:28, 29

Mvulana aliyekuwa mgonjwa apona

“Hakuna mkaaji atakayesema: ‘Mimi ni mgonjwa.’”—Isaya 33:24

Mashamba ya nafaka

“Kutakuwa na wingi wa nafaka duniani.”—Zaburi 72:16

FAIDIKA NA MAFUNDISHO YA BIBLIA
Wanaume wawili wakijifunza Biblia

Usidhani kwamba mambo hayo ni ndoto tu. Mungu ameahidi kwamba atatimiza mambo hayo, na Biblia inaeleza jinsi atakavyofanya hivyo.

Hata hivyo, Biblia ina faida nyingine nyingi. Inaweza kukusaidia kuwa na maisha yenye kuridhisha hata sasa. Hebu tua kidogo, ufikirie mahangaiko na matatizo yako mwenyewe. Huenda yanatia ndani ukosefu wa pesa, matatizo ya familia, matatizo ya afya, au kifo cha mpendwa. Biblia inaweza kukusaidia kushughulika na matatizo leo na inaweza kukufariji kwa kujibu maswali kama haya:

Kwa nini tunateseka?
Tunawezaje kushughulika na mahangaiko ya maisha?
Tunawezaje kufanya maisha ya familia yetu yawe yenye furaha zaidi?
Inakuwaje tunapokufa?
Je, tutapata kuwaona wapendwa wetu waliokufa?
Tunawezaje kuwa na hakika kwamba Mungu atatimiza ahadi zake kuhusu wakati ujao?

Kusoma kitabu hiki kunaonyesha kwamba ungependa kujua yale ambayo Biblia inafundisha. Kitabu hiki kitakusaidia. Sehemu ya chini ya kurasa kuna maswali yanayoambatana na mafungu. Mamilioni ya watu wamefurahia kuwa na mazungumzo ya Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova kwa njia ya maswali na majibu. Tunatumaini kwamba wewe pia utafurahia kufanya hivyo. Mungu na akubariki unapochukua hatua hiyo yenye kusisimua na kuridhisha ya kujifunza mambo ambayo Biblia inafundisha hasa!
IJUE BIBLIA YAKO

chib said...

Na kwako pia.

Yasinta Ngonyani said...

Samahani jamani majukumu yaliizidia..Nawashukuruni wote kwa kutochoka kupita hapa. Natumaini nanyi mmekuwa na wakati mwema. PAMAOJA DAIMA!!