Monday, April 2, 2012

NAONA TUIANZA JUMATATU HII YA KWANZA YA MWEZI HUU WA NNE NA KUTAFAKARI PICHA HII!!!

Kaazi kwelikweli, sijua nikikia itanilazimu kuoa ...au sijui itakuaje? Tutafakari pamoja naye jamani.....

3 comments:

ray njau said...

Mungu anahisije kuhusu mambo yanayoendelea ulimwenguni na maishani mwako? Kwanza kabisa, Biblia inafundisha kwamba Mungu ni “mpenda-haki.” (Zaburi 37:28) Kwa hiyo anapendezwa sana na mambo yanayofaa na kuchukizwa na mambo yasiyofaa. Anachukia ukosefu wa haki wa kila namna. Biblia inasema kwamba Mungu ‘aliumia moyoni mwake’ uovu ulipokuwa mwingi duniani wakati uliopita. (Mwanzo 6:5, 6) Mungu hajabadilika. (Malaki 3:6) Bado anachukia kuona mateso yanayoendelea ulimwenguni pote. Pia, Mungu anachukia kuona watu wakiteseka. Biblia inasema, “yeye anawajali ninyi.”—1 Petro 5:7.

12 Tunawezaje kuwa na hakika kwamba Mungu anachukia kuona watu wakiteseka? Uthibitisho mwingine ndio huu. Biblia inafundisha kwamba Mungu alimuumba mtu kwa mfano wake. (Mwanzo 1:26) Kwa hiyo, tuna sifa nzuri kwa sababu Mungu ana sifa nzuri. Kwa mfano, je, wewe husumbuka unapowaona watu wasio na hatia wakiteseka? Ikiwa unasumbuka kwa sababu ya ukosefu huo wa haki, uwe na hakika kwamba Mungu husumbuka hata zaidi.

13 Jambo moja la pekee kuhusu wanadamu ni kwamba tuna uwezo wa kuonyesha upendo. Mungu pia ana sifa hiyo. Biblia inafundisha kwamba “Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:8) Tuna upendo kwa sababu Mungu ana upendo. Je, upendo ungekuchochea kukomesha mateso na ukosefu wa haki unaoona ulimwenguni? Kama ungekuwa na uwezo wa kufanya hivyo, je, ungeyakomesha? Bila shaka ungeyakomesha! Uwe na hakika kwamba Mungu atakomesha mateso na ukosefu wa haki. Ahadi zinazotajwa katika utangulizi wa kitabu hiki si ndoto tu au matumaini yasiyo na msingi. Bila shaka ahadi za Mungu zitatimia! Hata hivyo, ili kuamini ahadi hizo, unahitaji kujua mengi zaidi kumhusu Mungu anayezitoa.

Seleman Awadh said...

Mtoto huyu hatafakakari juu ya kuoa kama alivyoandikwa hapo chini.kwanza mtoto huyu anonekana hana nguo za kumkinga na baridi wala viatu (yaani hana matunzo kwa ujumla).Ushauri wangu tuzae idadi ya watoto ambao tutaweza kuwapa mahitaji yote muhimu(chakula,mavazi,malazi, malezi ya baba na mama na elimu bora).

Anonymous said...

Picha ya mwaka hii ni kushinda zawadi kubwa sana.