Monday, November 14, 2011

TUANZE JUMATATU HII NA UJUMBE HUU:- TAMAA MBAYA



Tuliza moyo wako,kubali mapungufu yako. Rahisisha mahitaji yako, ongeza kipato chako. Chunga tamaaa mbaya…Sifa ya macho kuona yaani kutazama kinachoonekana. Ila sio kila unachokiona ukazani kupata inawezekana. Nyumbani kuna msichana njiani utaona wengi wasichana. Bora kuishia kutazama kuliko kujifanya unaweza sana. Siri ya maisha yako iko kwa muumba, mbuzi ni mbuzi hawezi kuwa simba… hawezi kuonekana eti wala hawezi kuimba bora kutulia ama kupiga malipa utasikia pia .....Chunga tamaa mbaya..... Ni baadhi ya maneno yaliyo tamkwa kwenye wimbo huu....ni ujumbe mzuri sana kwa jamii nami nimeona ni vema nikiwashirikisha wenzangu...

3 comments:

ray njau said...

TAMAA MBAYA:
-----------
Sanaa ni nini?
Sanaa ni hitimisho la mawazo ya msanii.Mtunzi wa wimbo baada ya kufanya utafiti na akagundua udhaifu ndani ya jamii yake ameamua kutoa onyo kupitia muziki huu.Swali kwetu sote ni hili;Je wewe na mimi tuna tamaa mbaya?

Simon Kitururu said...

Jumatatu njema kwako pia Yasinta!
Na asante kwa ujumbe kibonge!

Yasinta Ngonyani said...

Ahsanten kaka Ray na kaka Simon kwa kutochoka kutembelea maisha na mafanikio na kuacha kitu pia ahsanteni wote mpitao.