Tuesday, November 8, 2011

HUU NI UJUMBE WA JUMANNE YA LEO!!!

JUMANNE NJEMA NDUGU ZANGUNI!!!



6 comments:

ray njau said...

Ecclesiastes 3:1-9

1 For everything there is an appointed time, even a time for every affair under the heavens: 2 a time for birth and a time to die; a time to plant and a time to uproot what was planted; 3 a time to kill and a time to heal; a time to break down and a time to build; 4 a time to weep and a time to laugh; a time to wail and a time to skip about; 5 a time to throw stones away and a time to bring stones together; a time to embrace and a time to keep away from embracing; 6 a time to seek and a time to give up as lost; a time to keep and a time to throw away; 7 a time to rip apart and a time to sew together; a time to keep quiet and a time to speak; 8 a time to love and a time to hate; a time for war and a time for peace. 9 What advantage is there for the doer in what he is working hard at?
==================================
Mhubiri 3:1-9

1 Kuna wakati uliowekwa wa kila kitu, hata kuna wakati wa kila jambo chini ya mbingu: 2 wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa; wakati wa kupanda na wakati wa kung’oa kilichopandwa; 3 wakati wa kuua na wakati wa kuponya; wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga; 4 wakati wa kulia na wakati wa kucheka; wakati wa kuomboleza na wakati wa kurukaruka; 5 wakati wa kutupa mawe na wakati wa kukusanya mawe; wakati wa kukumbatia na wakati wa kuepuka kukumbatia; 6 wakati wa kutafuta na wakati wa kuacha kutafuta kilichopotea; wakati wa kuweka na wakati wa kutupa; 7 wakati wa kupasua na wakati wa kushona, wakati wa kukaa kimya na wakati wa kusema; 8 wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia; wakati wa vita na wakati wa amani. 9 Mtendaji ana faida gani katika jambo analofanyia kazi ngumu?

ray njau said...

Mada iliyopo hapa kibarazani leo ni yenye manufaa sana kwetu sote katika kutambua thamani ya muda maishani.Baadhi yetu hatuna ratiba katika utendaji wetu kwa kuonyesha mambo muhimu yenye umuhimu wa kipekee na yale ya ziada.Huu ndiyo msingi wa kuzuka kwa vijiwe ambavyo mwisho wa siku hugeuka kuwa mikikimikiki bila maisha na mafanikio.
===================================
"SIKU HAZINGANDI LAKINI ZINAYEYUKA"
===================================

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Ray!"Tatizo muda kila jambo na wakati wake" kuna wengi wana haraka sana kupata mafanikio katika maisha wanataka tu kuamka na kila kitu kiwe. Au kama kama hii kuwa kupata mtoto, kujenga nyumba, kupata kazi nk kila kitu kina wakati wake..bila kusahau kumwomba Mwenyezi Mungu. kama ulivyonukuu katika Mhubiri katika hiyo sura na hiyo mistari. Ahsante..

Unknown said...

Kweli kila jambo na wakati wake,
na muda ukishapita hauwezi kurudi tena.

ray njau said...

Yakobo 4:1-17

1 Vita vinatoka chanzo gani na mapigano yanatoka chanzo gani katikati yenu? Je, havitoki katika chanzo hiki, yaani, katika tamaa zenu za mwili zinazoendeleza pambano katika viungo vyenu? 2 Mnatamani, na bado hamna kitu. Mnaendelea kuua na kutamani kwa wivu, na bado hamwezi kupata. Mnaendelea kupigana na kufanya vita. Hamna kitu kwa sababu hamwombi. 3 Mnaomba, na bado hampokei, kwa sababu mnaomba kwa kusudi baya, ili mvitumie kwa tamaa zenu za mwili.

4 Enyi wazinzi, je, hamjui kwamba urafiki na ulimwengu ni uadui na Mungu? Kwa hiyo, yeyote anayetaka kuwa rafiki ya ulimwengu anajifanya kuwa adui ya Mungu. 5 Au je, inaonekana kwenu kwamba andiko linasema hivi bila kusudi lolote: “Roho ambayo imefanya makao ndani yetu hutamani kuwa na mwelekeo wa kuona wivu”? 6 Hata hivyo, fadhili zisizostahiliwa ambazo yeye hutoa ni kubwa zaidi. Kwa hiyo, hilo linasema: “Mungu huwapinga wenye majivuno, lakini huwapa wanyenyekevu fadhili zisizostahiliwa.”

7 Basi, jitiisheni kwa Mungu; lakini mpingeni Ibilisi, naye atawakimbia ninyi. 8 Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Safisheni mikono yenu, ninyi watenda-dhambi, na takaseni mioyo yenu, ninyi wenye kusitasita. 9 Iweni na taabu na kuomboleza na kulia. Kicheko chenu na kigeuzwe kuwa maombolezo, na shangwe yenu kuwa huzuni. 10 Jinyenyekezeni machoni pa Yehova, naye atawainua ninyi.

11 Mwache kusemana wenyewe, akina ndugu. Yeye anayesema vibaya juu ya ndugu au anayemhukumu ndugu yake husema vibaya juu ya sheria na kuihukumu sheria. Na ikiwa unaihukumu sheria, basi wewe si mtendaji wa sheria, bali ni mwamuzi. 12 Kuna mmoja ambaye ni mpaji-sheria na mwamuzi, ambaye anaweza kuokoa na kuangamiza. Lakini wewe ni nani ili uwe ukimhukumu jirani yako?

13 Haya, basi, ninyi ambao husema: “Leo au kesho tutasafiri kwenda jiji fulani nasi tutakaa mwaka mmoja huko, tutafanya biashara na kupata faida,” 14 ingawa hamjui uzima wenu utakuwa namna gani kesho. Kwa maana ninyi ni ukungu unaotokea kwa muda kidogo na kisha kutoweka. 15 Badala yake, mnapaswa kusema: “Yehova akipenda, tutaishi na pia kufanya hili au lile.” 16 Lakini sasa mnajivunia kujigamba kwenu kwa kujidai. Majivuno yote ya namna hiyo ni maovu. 17 Kwa hiyo, ikiwa mtu anajua jinsi ya kufanya yaliyo sawa na bado hayafanyi, hiyo ni dhambi kwake.

Salehe Msanda said...

Ni ujumbe mzuri,zaidi ya muda ni suala la kuamua na kutenda kw dhati kuhusu kile unachohitaji.

Kila la kheri