Thursday, April 2, 2009

NAMTAFUTA DADA PRIMROSE KALUNGI TUMEPOTEANA TANGU MWAKA 1999


Tulikuwa tunaishi vizuri sana hapa Sweden yeye ni mtu wa Uganda. Mwaka 1999 alihama hapa na kuhamia UK mtaa wa Croydon , tangu hapa hatujaonana tena isipokuwa nimeongea naye kwenye simu mwaka 2003 mara ya mwisho. Lakini kila nikijaribu kuwasiliana naye simpati. Kama kuna mtu anamfahamu au kama wewe mwenyewe utasoma hapa basi naomba uwasiliane nami. Primrose ni huyo dada aliyesimama upande wa kushoto na amevaa jeans ya bluu.

3 comments:

Anonymous said...

mhh, hayo sio mahindi ya mandulutulu?

Yasinta Ngonyani said...

Usiye na jina haya ndiyo mahindi ya huku ya ugali na kutafuna. labda unaweza kufanya mandulutulu.

Anonymous said...

du, sio mchezo huo ndio ugali gani tena au ndio ile yanga nini? lakini mazoea, maana sisi huku bongo ugali wetu ni mweupe, huo huwa tunakula wakati wa njaa. cha ajabu ni kwamba hao watu ukiwapa ugali mweupe wanaweza kugoma kula! du, nimeyatamani mandulutulu, ndoja niagize toka litumbandyosi!!