Sunday, April 28, 2013

JUMAPILI YA LEO NI MAARUFU BINTI YETU CAMILLA ANAPATA KIPAIMARA..HONGERA..

picha ya pamoja baada ya kupata kipaimara Da ´Camilla  hapo katikatika na nywele nyeusi
 
nipo na rafiki
watu walivyofurika

baadhi ya wageni waliokujha kumpongeza Camilla
baadhi ya msosi

 
baada ya misa , sasa hapa nu nyumbani

keki ya karoti
 
kufungua zawadi
Jumapili hii imekuwa ndefu na nyenya baraka nyingi sana katika nyumba yetu ...TUNAMSHUKURU MUNGU KWA SIKU HII...nimeona niwe pamoja nanyi katika siku hii njema, AHSANTE MUNGU....NA HONGERA SANA BINTI CAMILLA

24 comments:

Rachel Siwa said...

Hongera sana da'Camilla..MUNGU akulinde na ukue mwili na roho katika Imani....pia Hongereni wazazi kwa malezi na kumuongoza binti katika IMANI.

Yasinta Ngonyani said...

Rachel..Kachiki wangu ..Da`Camilla anashukuru sana na anasema AHASANTE KWA BARAKA

Mija Shija Sayi said...

Hii ni hatua kubwa sana katika imani, hongereni sana wazazi kwa kumlea Camilla katika misingi ya kumjua Mungu..

Halafu Yasinta una kabinti kazuri..!!

Hongera sana Camilla!!

Anonymous said...

Hongera sana Camilla, na wazazi pia. Mungu azidi kukusaidia kumjua yeye zaidi na zaidi. Da Yasinta hujatuwekea picha ulizopiga na Camilla au ulivyoonekana wewe siku hiyo. Tunahamu sana kukuona pia.

Yasinta Ngonyani said...

Da' Mija! Ahsante ndugu yangu.

Usiye na jina! Kwanza ahsante. Pili naomba samahani pilika zilinizidia nikadahau kupiga picha naye . Ila ntapiha naye tu untaniona. Ahsante kunikumbusha

Anonymous said...

Mh jamani! Hukupiga naye picha hata moja? Hukumtendea haki! Haya tunasubiria.

emuthree said...

Hongera Camilla na Hongereni wazazi wa Camilla kwa malezi yaliyobora. Mubarikiwe sana

MARKUS MPANGALA said...

Hongera sana mwanangu Camilla, mwenyezi mungu akuajalie afya njema na uwajali wazazi pia kama ilivyo desturi yako.

Anonymous said...

Haya Da Yasinta nazisubiria hizo picha utkazopiga naye, sijui leo? au utarewind tena akivaa gauni yake nyeupe itapendeza sana sana.

Yasinta Ngonyani said...

Usiye na jina..kuwa na subira

Emu3 ahsante ndugu wangu salamu zimefika

Markus! Usengwili sana na chilawu mewawa.

Usiye na jina kuwa na subira ntamwomba binti akokubali utaona. Maans huwa hapendi lupigwa picha. Yaani nilipitiwa mno....

sam mbogoa said...

mpe hongera sanii mtoto . na akuwe kwa imani hiyohiyo ya kumtumainia mungu, na bwana yesu kama mwakozi wetu /wake . naikubuka siku hii! we achatu kaka s

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Sam...usikonde salam za hongera zimepokelewa..ilikuwsje siku yako kana hii?

EDNA said...

Hongera sana Camilla.Ulipendeza pia.

Anonymous said...

Mwambie Dada Camilla kwa niaba ya dada aliyecomment humu naomba avae ileile gauni yake na viatu vilevile,nywele style ilelile ili mpige naye picha, hata kama hapendi najua atakubali ombi toka humu kwenye blog ya mama yake. Mwambie hayuko peke yake mie mwenyewe sipendi kupigwa picha na hata mwanangu ndio kabisaaaaaa! Sijui kwa nini inatokea hivyo mtu hupendi kupigwa picha! Mie sipendi napiga picha mara chache chache mno. Msalimu Camilla mwambie amekuwa dada na anazidi kupendeza. Kama anajua kiswahili asome mwenyewe hapa.

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Du kumbe mwana amekua! Ajue kupata kipaimara ni kuwa imara katika imani, nidhamu, kujitambua na kutambua mabadiliko katika majukumu hata kuwajibika.
Hongera mwana na wavyele.

Yasinta Ngonyani said...

Edna! Karibu Tena Camilla anasema ahsante mama mdogo...
Usiye na jina ingekuwa vizuri kama ungesema jina lako Camilla anasema..ila usikonde iko siko utaona hizo picha Mungu akipenda.

Mwal. Mhango..Yaani siku zinakimbia kama nini karibuni tu tutakuwa bibi na babu..LOL Ahsante na chilawu mewawa..

Nachukua nafasi hii na kuwashukuruni wote..Si kwamba nafunga mada hapana karibu kuendelea.

Penina Simon said...

Hongera Camilla!

Matha Malima said...

asante kwapicha nzuri za baby mwambie hongera sana

Emmanuel Mhagama said...

Hata kama nimechelewa, wacha niseme tu. Shangazi yangu Camila pokea pongezi nyingi kwa kupata Sakramenti hii ya kipaimara. Ni hatua ya msingi katika ukuaji wa maisha ya kiroho. Roho Mtakatifu uliyempokea akujalie kuwa imara katika kumjua, kumpenda, kumtumikia na kumwamini Mungu. HONGERA SANA.

Anonymous said...

TUONGEZEE PICHA ZA CAMILLA KAMA ZIPO NA ZINGINE.

Yasinta Ngonyani said...

Da´Penina ahsante Hongera zimepokelewa.

Matha.. Ahsante amezipokea hongera.

Kwa niaba ya Camilla Mjomba Mhagama..Ahsante nitatekeleza hayo.

Usiye na jina! :-)

Anonymous said...

Yasinta naona mbio zangu za sakafuni za kutaka picha picha sasa zinaishia ukingoni. Mana kila wakati narudi humu kucheck picha za kama umeweka zaidi nakuta hakuna! Niwie radhi Yasinta napenda sana kutazama picha. Ubarikiwe.

Interestedtips said...

jamani nimepitwa na sherehe ya Camilla, kulala sana nako i hasara hadi nimechelewa kumpongeza........... Hongera sana dada Camilla, unakua kiroho zaidi Mungu aendelee kukulinda na mapaji yake uliyoyapokea siku hiyo. Amen

Yasinta Ngonyani said...

Usiye na jina ! :-D

Kwa niaba ya Camilla-: Mama mdogo Ester wala hujachelewa. Halafu nakukumbuka sana. Ahsante sana nitatekeleza maagizo