Monday, April 15, 2013

EBU LEO TUANGALIA BAADHI YA MAKUNDI MBALIMBALI YA WATU HAPA DUNIANI...

Katika hii dunia kuna watu wa aina mbalimbali...
kundi la kwanza: Kuna watu wanajua lakini hawajui kwamba wanajua. Hawa wanaitwa wasahaulifu na sisi tunatakiwa tuwakumbushe.

kundi la pili:- Kundi hili ni kwamba wengine ni maskini wa Mungu hawajui lakini Mungu amewabariki wanajua kwamba hawajui . Hao ni wajinga na sisi inabidi tuwaelimishe.

kundi la tatu:- Hawa wengine wao wanajua na wanajua kwamba wanajua. hawa waelevu nasi tunahitaji kujifunza toka kwao kwa vile wao ni waelevu.

Na kundi la nne: Wengine hawajui na wao hawajui kwamba hawajui wabishi. Hawa ni wapumbavu ..hawa inabidi tuachane nao kabisa. Mhhhh..najiuliza sijui ni kundi gani nipo???
JUMATATU NJEMA KWA WOTE...

3 comments:

Anonymous said...

Na kuna makundi mengine ya kuchumia matumbo, hasa ya naunga hoja mia kwa mia bungeni. By Salumu

Mija Shija Sayi said...

Raha ya haya makundi ni mtu mwingine akupime kuliko kujipima mwenyewe.

Kaka yangu Salumu hapo juu umeona mbali mwenzetu!

Rachel Siwa said...

Duuh Asante sana KADALA..Kwa Shuke hii.