Friday, March 15, 2013

NIMEPENDA WIMBO/NYIMBO HII/UJUMBE HUU KUHUSU KUPENDA..UNAWEZA KUSIKILIZA UKIPATA WASAA!!!

NACHUKUA NAFASI HII NA KUWATAKIENI WAOTE MCHANA, JIONI,ASUBUHI AU USIKU NJEMA YA IJUMAA HII..NA IWE YA UPENDO NA AMANI.TUPO PAMOJA DAIMA!!!

6 comments:

ray njau said...

"Upendo hufunika wingi wa dhambi".

emuthree said...

Upendo ni amani...tupo pamoja mpendwa

Yasinta Ngonyani said...

Naungana na waliotangulia ..upendo ni funiko la wingi wa dhambi na upendo ni amani... labda niongezee kidogo:- UPENDO: fumbo la ajabu, ni jambo la kuitoa nafsi yako. Upendo kidogo ni kama jua, ambalo ni rafiki yetu wa daima. Hufukuza baridi, huimarisha mazao yetu na kuyaivisha. Hivyo ndivyo ufanyavyo upendo kama jua.

Kachiki upoooowewe unapenda kuimba na sijui kadado naye yupo..Wivu wa kupenda unatuangaishaX4
Wewe uyoo hukuniamini, usipo niamini ina manaana na wewe hujiaminix3
eeeh punguza hasira usifute maneno na ugomvi si sehemu ya Upendo.......duh naona koo limekauka ngoja ninywa maji kwanza...

sam mbogo said...

nyimbo nyingi zimeimbwa kuhusu wivu wa mapenzi.kila mwanamuziki kajaribu kuelezea hisia zake ju ya jambo hili. mimi kunawimbo huwa nikiusikia siachi kufika mbali kwa kuutafakari ju ya ujumbe au maneno ya wimbo huo.JELA YA MAPENZI kamasikosei watakuwa walikuwa ni WESTENI JAZZ. Ila kipengere hiki nikigumu sana (wivu wa mapenzi) na madhara /matokeo yake huwa si mzuri, mimi huita hali hii ya wivu wa mapenzi kuwa ni ubinafsi.ambao unahitaji hali ya ju kabisa ya ufahamu kukabiliana nao,usikivu,uvumilivu,busala,upendo,kuwa nakiasi,na wakaati mwingine utakapo jipenda na kujithamini wewe binafsi na kukubali matokeo,waweza kwa kiasi fulani kuto sumbuliwa na wivu wa mapenzi. kaka s.

ray njau said...

Jinsi Upendo Usivyo
===========================
• “Upendo hauna wivu.” Wivu usiofaa unaweza kutufanya tuwaonee wengine kijicho kwa sababu ya vitu walivyo navyo—mali zao, mapendeleo yao, au vipawa vyao. Wivu huo ni hisia hatari sana ya ubinafsi ambayo inaweza kuvuruga amani ya kutaniko isipodhibitiwa. Ni nini kitakachotusaidia tukinze “mwelekeo wa kuhusudu”? (Yakobo 4:5) Ni upendo. Sifa hiyo muhimu sana itatufanya tushangilie pamoja na wale ambao wana mapendeleo fulani ambayo hatuna. (Waroma 12:15) Upendo hutuzuia kukasirika mtu fulani anapopongezwa kwa sababu ya kuwa na kipawa fulani cha pekee au kwa kutimiza jambo fulani kubwa.
• ‘Upendo haujigambi, haujitutumui.’ Upendo hutuzuia kujigamba kwa sababu ya vipawa vyetu au mafanikio yetu. Ikiwa tunawapenda ndugu zetu kikweli, je, tutajigamba daima kwa sababu ya mafanikio yetu katika huduma au kwa sababu ya mapendeleo yetu kutanikoni? Kujigamba kwa njia hiyo kunaweza kuwavunja wengine moyo, na kuwafanya wajione hawafai. Upendo hutuzuia kujigamba kwa sababu ya mapendeleo ya utumishi ambayo Mungu ametupatia. (1 Wakorintho 3:5-9) Zaidi ya hayo, upendo “haujitutumui,” au kama tafsiri moja inavyosema ‘haujioni kuwa bora.’ Upendo hutuzuia kujiona kuwa bora.—Waroma 12:3.
• ‘Upendo haujiendeshi bila adabu.’ Mtu asiye na adabu anatenda kwa njia mbaya sana au yenye kuudhi. Mtu anayejiendesha hivyo hana upendo kwa sababu hajali hisia na hali njema ya wengine. Kinyume chake, upendo ni wenye fadhili na unatuchochea kuwajali wengine. Tukiwa na upendo tutakuwa na adabu, tutajiendesha kwa njia inayompendeza Mungu, na tutawaheshimu waamini wenzetu. Kwa hiyo, tukiwa na upendo tutaepuka “mwenendo wa aibu,” au tabia yoyote ile ambayo itawashtua au kuwaudhi ndugu zetu Wakristo.—Waefeso 5:3, 4.
• ‘Upendo hautafuti masilahi yao wenyewe.’ Tafsiri nyingine inasema hivi: “Upendo hausisitizi kufuata njia yake.” Mtu mwenye upendo hasisitizi kila jambo lifanywe jinsi anavyopenda, kana kwamba maoni yake ni sawa sikuzote. Hawashawishi wengine ili kuwashurutisha wenye maoni tofauti wafuate maoni yake. Ukaidi wa aina hiyo unaonyesha kwamba ana kiasi fulani cha kiburi, na Biblia inasema: “Kiburi hutangulia uangamivu.” (Mithali 16:18) Ikiwa tunawapenda kikweli ndugu zetu, tutaheshimu maoni yao, na tutakuwa tayari kuyakubali inapowezekana. Maneno haya ya Paulo yanatutia moyo kuwa na roho hiyo: “Acheni kila mmoja afulize kutafuta sana, si faida yake mwenyewe, bali ya mtu yule mwingine.”—1 Wakorintho 10:24.
• ‘Upendo hauchokozeki, hauweki hesabu ya ubaya.’ Upendo haukasirishwi ovyoovyo na mambo ambayo wengine wanasema au kufanya. Ni jambo la kawaida kukasirika tunapokosewa. Lakini hata tukiwa na sababu nzuri ya kukasirika, hatutaendelea kuchokozeka ikiwa tuna upendo. (Waefeso 4:26, 27) Hatutaweka hesabu ya maneno au matendo yenye kuumiza kana kwamba tunayaandika katika kitabu ili tusiyasahau. Badala yake, upendo unatuchochea kumwiga Mungu wetu mwenye upendo. Kama tulivyoona katika Sura ya 26, Yehova husamehe kunapokuwa na sababu nzuri ya kufanya hivyo. Yeye husamehe na kusahau, yaani, hatuadhibu baadaye kwa sababu ya dhambi hizo. Je, hatushukuru kwamba Yehova haweki hesabu ya ubaya?
• ‘Upendo haushangilii ukosefu wa uadilifu.’ Tafsiri nyingine inasema: “Upendo . . . haushangilii dhambi za wengine.” Tafsiri ya Moffat yasema: “Upendo haufurahii kamwe wengine wanapokosea.” Upendo haufurahii uovu, kwa hiyo tunakataa kabisa ukosefu wowote wa adili. Tunahisije mwamini mwenzetu anapotenda dhambi na kupata madhara? Tukiwa na upendo hatutashangilia kana kwamba tunasema, ‘Shauri yake! Asiyesikia la mkuu huvunjika guu!’ (Mithali 17:5) Hata hivyo, tunashangilia ndugu aliyetenda dhambi anapochukua hatua zifaazo za kujirekebisha na kufanya maendeleo ya kiroho.

sam mbogo said...

Unapo changanya maandiko na kuhusisha na maisha halisia kwa hakika kila binaadamu ana jinsi anavyo tafsiri upendo kwake yeye ninini,?NDUGU YANGU NJAU upendo uliopo katika vitabu vitakatifu ukijaribu kufuata na kuutekeleza katika maisha yako ya kila siku lazima uwe nimtu uliye kata shauri kuishi hivyo. wengi upendo tulio nao ni ule wa kuwaangalia watu wanasemaje kuhusu wewe,yaani wa kufurahisha watu,lakini ukifuatilia kwa undani sikweli uko au tuko hivyo kwa ndani. ugumu unakuja pale unapoambiwa,MPENDE JIRANI YAKO KAMAUNAVYO JIPENDA.ukitafakali neno hili utajuwa nini maana ya upendo. kaka s