Friday, June 1, 2012

IJUMAA HII YA MWEZI MPYA NIMEONA TUANZE HIVI!!!

ONENI UZURI WA AJABU WA UUMBAJI WA MUNGU
Chuki huzusha ugomvi, lakini upendo hufunika makosa yote. Na kwamba Hila imo mioyoni mwao wafikirio uovu. Bali wafanyao mashauri ya zamani kwao kuna furaha.
 au LABDA TU KAKA SUMA LEE AMALIZIE NA HAKUNAGA

IJUMAA NJEMA KWA WOTE NA KILA LA KHERI KWA KUUANZA MWEZI MPYA NA PIA    MWISHO WA JUMA UWE MWEMA.!!!!!

5 comments:

ray njau said...

Asante sana na uwe na wikiendi njema!!

ray njau said...

Ayubu 39:1-30
-----------------------

1 “Je, umepata kujua wakati uliowekwa wa mbuzi wa milimani kuzaa?

Je, unaangalia wakati ule paa wanapozaa kwa uchungu?

2 Je, wewe huhesabu miezi ambayo wao hutimiza,
Au, je, umepata kujua wakati uliowekwa ambapo wao huzaa?

3 Wao huinama wanapotoa watoto wao,
Wanapoondoa uchungu wao.

4 Wana wao huwa wenye nguvu, huwa wakubwa porini;
Kwa kweli wao huenda zao wala hawarudi kwao.

5 Ni nani aliyemwachilia punda-milia awe huru,
Na ni nani aliyevifungua vifungo vya punda-mwitu,

6 Ambao nimeweka nchi tambarare ya jangwa kuwa nyumba yao
Na ambao makao yao ni nchi ya chumvi?

7 Yeye huyacheka machafuko ya mji;
Naye hasikii kelele za mwindaji.

8 Yeye hutafuta-tafuta malisho yake milimani
Naye hutafuta kila namna ya mmea wa kijani.

9 Je, ng’ombe-mwitu hutaka kukutumikia,
Au, je, atalala usiku kwenye hori yako?

10 Je, utamfunga imara ng’ombe-mwitu kwa kamba zake katika mtaro,
Au, je, yeye atalima nchi tambarare za chini nyuma yako?

11 Je, utamtegemea kwa kuwa ana nguvu nyingi,
Na, je, utamwachia yeye kazi yako ngumu?

12 Je, utamtegemea kwamba atarudisha mbegu zako
Na kwamba atakusanya kwenye uwanja wako wa kupuria?

13 Je, bawa la mbuni-jike limepiga-piga kwa shangwe,
Au, je, yeye ana mbawa za korongo na manyoya?

14 Kwa maana yeye huyaacha mayai yake katika nchi
Naye huyatia joto katika mavumbi,

15 Naye husahau kwamba mguu fulani unaweza kuyavunja
Au hata mnyama wa mwituni anaweza kuyakanyaga.

16 Yeye huwatendea wanawe kwa ukali, kana kwamba si wake—
Kazi yake ngumu ni ya ubatili kwa sababu yeye hana hofu.

17 Kwa maana Mungu amemfanya asahau hekima,
Naye hakumpa fungu katika uelewaji.

18 Wakati anapopiga-piga mabawa yake juu,
Yeye humcheka farasi na mpandaji wake.

19 Je, unaweza kumpa farasi nguvu?
Je, unaweza kuivika shingo yake manyoya yanayotetema?

20 Je, unaweza kumfanya aruke kama nzige?
Fahari ya kukoroma kwake ni yenye kutisha.

21 Yeye huparapara katika nchi tambarare ya chini na kufurahia nguvu;
Husonga mbele kukutana na silaha.

22 Huicheka hofu, naye hatishiki;
Wala harudi nyuma kwa sababu ya upanga.

23 Podo hupiga kelele juu yake,
Kichwa cha mkuki na pia fumo.

24 Yeye huimeza nchi kwa mwendo wa kishindo na msisimuko,
Wala haamini kwamba ni sauti ya baragumu.

25 Mara tu baragumu inapopiga yeye husema Aha!
Naye hunusa harufu ya pigano kutoka mbali sana,

Mshindo wa wakuu na kelele za vita.

26 Je, ni kwa sababu ya uelewaji wako kwamba kipanga hupaa juu,
Kwamba yeye hunyoosha mabawa yake kuuelekea upepo wa kusini?

27 Au, je, ni kwa agizo lako
kwamba tai huruka kuelekea juu
Na kwamba hujenga kiota chake huko juu,

28 Kwamba yeye hukaa kwenye mwamba na wakati wa usiku hukaa
Juu ya ncha ya mwamba na mahali pasipoweza kufikiwa?

29 Kutoka hapo yeye hutafuta chakula;
Macho yake huendelea kutazama mbali sana.

30 Na watoto wake huendelea kunywa damu;
Na mahali walipo wale waliouawa, yeye yupo hapo.”
YaliyomoSuraInayotanguliaInayofuata

Interestedtips said...

Asante sana mpendwa, hao wanyama walivyo tu inaashiria upendo na amani, kila heri iwe nawe dada

Rachel Siwa said...

Hakunaga dada Kadala!!!!!!

Salehe Msanda said...

Hongera;
Kwa kuenzi utajiri wetu wa maliasili na wanyama.
Kila la kheri