Saturday, October 31, 2009

MUZIKI NI MOJA YA STAREHE KATIKA MAISHA


JUMAMOSI NJEMA KWA WOTE KUMBUKENI SIO UGIMBI/ULANZI MWINGI:-)!!!!!

7 comments:

Chacha Wambura said...

Ugimbi/Ulanzi a.k.a pingu-baha ni sunna bibi...lol

Uwe mwingi ama mchache ni ugimbi tu. Ama ni wakati gani unajua nimekunywa ugimbi mwingi ama mchache?...lol

nyahbingi worrior. said...

sio tu starehe,Muziki ni ujumbe,je ni ujembe wa aina gani?

Chacha Wambura said...

Nyabhingi, ujumbe gani? Hilo ni swali murua...

kwa mfano mimi ninaposikiliza nyimbo za injili huwa sisikilizi maneno bali midundo ya sebene na ndombolo ya solo...lol


kwa hiyo si ujumbe hapo napata bali sebeneee...lol

twenty 4 seven said...

nasikia raha ya ullanzi lazima ulale siku kadhaa baada ya kugemwa wadau mnisaidie...

Yasinta Ngonyani said...

Chacha na wewe kwa ugimbi tu:-)

Nyahbingi warrior! umenena kweli muziki ni ujumbe pia na unaweza kuwa ujumbe wa dini, mapenzi, maisha, au hata kama unataka kumwambia mtu kitu basi unaweza kuimba.

Chib:-)

Chacha! basi anza kusikiliza maneno pia utaona ni ujumbe gani unapata.

Mishemishe! nimeshindwa kukujibu swali lako kwani siju ila nahisi kuna wataalamu watakujibu basi itakuwa wewe na mimi pia tumeelewa hilo

John Mwaipopo said...

Mishemishe na Yansinta
ingawaje mie si mzaliwa wa iringa, nilipata bahati ya kusoma malangali. Ulanzi (wenyewe wanaia ulaasi) uko wa aina tatu:

1. mtogwa: huu ni ule uliogemwa leoleo. kwa kawaida huu huwa mtamu na unapendeza mdomoni. kuna ladha iliyochanganyika na ya maji ya dafu vile. ni mzuri kwa kunywa kidogo tu, pia kwa watu wanatamani kujifunza. si vema kunywa mwingi kwa anayeanza kwa kuwa unalewesha baadae sana.

2. mkangafu: huu umegemwa jana ama juzi. uko katika kipindi cha mpito kutoka mtogwa kuelekea anina ya tatu ntakayoielezea hapa chini. ni mchungu kwa ladha. sio uchungu wa klorokwini. hapana. ni ladha nzuri. unavutia zaidi ukichanganywa na mtogwa kwa uwiano ya mtogwa 1: mkangagu 2. unafaa wa wazoefu wa kati na wale wazoefu wa vilevi vingine wanaohitaji kubadilisha ulevi japo kwa muda.

3. mdindifu: huu ni kiboko. waweza kuwa umegemwa wiki moja, mbili hata zaidi na kuhifadhiwa vema usiharibike. mwingine waweza kuhifadhiwa kunako vyungu vikuuubwa vilivyofunikwa vyema mdomoni na vyungu hivyo kuchimbiwa chini ya ardhi. huu huanza kuifadhiwa chini ya ardhi majira yakielekea katika ukame ili uwafae wakati wa kiangazi. unaweza kukaa hata miezi 6. ni mkali kwelikweli na unafaa kwa 'wale wenye nguvu' ya kunywa pombe kwelikweli na mara nyingi hupendwa na watu wanaoogopa 'kuendesha' wakinnywa aina ya kwanza na ya pili.


LOL nadhani kuna watu mate yanawadongoka kama mimi. how i wish time could turn back!

Yasinta Ngonyani said...

Mwaipopo! loo, darasa zuri sana la ulanzi unajua bibi yangu alikuwa na vitindi vya ulanzi lakini mie sikujali kujifunza hayo yote. Na halafu nimeishi sana kule ubenani Madaba-Matetereka pia sikujali kufuatilia upi ni upi nilikuwa nasikia majina tu na sikujua kutofautisha. Mbaya zaidi sijawahi onja ila najua wengi hawataniamini...lol. Kwa maelezo hayo kaka Mwaipopo nakuamni unatamani siku zirusi nyuma.